Call / WhatsApp +255673378129

Dec 19, 2010

EURO MIND Antenna

Si wanainchi wote ambao wana uwezo wa kufunga Dish ama king'amuzi kutokana na hali ya maisha jinsi ilivyo na kwa upande wa pili pia si channel zote za nyumbani zinazopatikana kwenye Satellite Dish ama hata penye king'amuzi pia,hivyo swala la Antenna linabaki pale pale kwamba ni la muhimu si uwezo ijapokuwa linahusika pia.
Kwa wapatao tabu kuhusu Antenna ipi inaweza ikawasaidia kuona picha clear kutokana na eneo waishilo,jibu ni moja tu EURO MIND Antenna na ikitokea haishiki basi ujue eneo lako halistahili Antenna.
Kwa wale wenzangu na mimi wa uswazi kuna zile tube ambazo unazifanyia mambo na kuwa bonge la Antenna.
Share:

6 Unasemaje..??:

Anonymous said...

Mkubwa umejuaje kama tupo watu wa Tube...!!!
Eeehee na hiyo euromind c ndio milaki..??
Eti mkuu nikuulize zamaani nilikuwa nasikia eti mtu ukifunga dish unaweza ukaona hata mtu akiwa chooni hapo jirani yako,je ni dish aina gani hizooo....!!
Au ilikuwa ni fix...!!

Mustapha MaDish said...

Ahahahaa...!!
sio kwamba nakucheka bali umenichekesha hiyo issue ya ukifunga dish hata wa chooni unamuona si kweli maana kila ukifunga dish unaweka frequency maalumu kwa satellite husika,huduma hiyo ni mitambo mengine kama CCTV..!!
EUROMIND wala sio kama udhaniavyo mkuu.

Anonymous said...

mi nipo na ile wanaita soneti na inaonyesha baadhi vizuri tu lakini kama tbc1,channel10,na c2c sizipati vizuri,inakuwa mpaka tuzungushe,je hiyo euromind itaonyesha clear zote hizo.....??

Mustapha MaDish said...

kiukweli ambacho naweza kusema euromind imeiacha soneti hatua 3 nyuma,nikiwa na maana euromind ipo juu ya soneti kwa ubora...!!
Lakini siwezi kusema kama ukifunga euromind hizo channel usemazo zitaonyesha clear kama utakavyo..!!
Sijui upo maeneo gani?
Ila mpaka hapo nadhani umenisoma...!!

Anonymous said...

Kaka mimi nimeuziwa hii EURO MIND isipokuwa hakuna nafuu yeyote nipo maneo ya mbezi.

Anonymous said...

Nitajuaje kama Original or Fake??

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita