Call / WhatsApp +255673378129

Dec 29, 2010

Mbio za funga mwaka ndani ya bwaga moyo.....!!

Tunahesabu siku tu kuelekea mwaka mupya mupya kabisa 2011,huku tukiumalizia malizia mwaka huu 2010,ukiniacha na kumbukumbu nzuri ya kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa kwa namba za kipekee ambazo kamwe hazitajirejea 10.10.10 maana nilizaliwa miaka kadhaa nyuma ikiwa ni tarehe 10 mwezi wa 10.
Tukiyaacha hayo leo nipo bwagamoyo na nadhani nitakuwepo huku mpaka kesho ama kesho kutwa na hakuna kilichonileta huku zaidi ya kazi na na7bisha kama kawa yangu.....!!
Share:

Dec 28, 2010

Kuelekea 2011 yapi mazuri na ya kupongeza 2010....!!

Kwa kuanza tu naweza nikasema kwa mwaka huu 2010 ni mwaka mgumu sana hasa kwa vijana,yananitoka haya kutokana na mazungumzo yao pale unapokaa nao,maana wenyewe wanakwambia hakuna njia kama milango inazidi kufungwa ili watu wasitoke,hivyo kipindi wao wanasema hivyo sijui wewe unasema aje kuhusu mwaka huu unaoishia.....!!
Upande wa kazi banaa jua halikuwa kali saana maana ushindani ulikuwepo ila si mkali sana ni wa kawaida tu,ilizaliwa kampuni inayojulikana kama star times ambayo kuna mkono wa TBC na wachina,ambao wamekuja tofauti kidogo,badala ya kutumia dish wao walitumia Antenna na decoder,ni kitu kizuri na watanzania wamekipokea ila si kama ambavyo walidhani hasa baada kufa GTV na kusemekana inakuja kampuni ambayo itakuwa inafanana na GTV ili kuleta ushindani na DSTV katika swala la mpira kuhusu malipo ya mwezi,sitaki kuelezea sana ila tukaitambua star time na utofauti wa kutumia antenna ila yenyewe si ya kwanza ilitangulia EASY TV ambayo mpaka sasa bado ipo na inafanya vizuri pia.
Pia ATN nao wametoa ving'amuzi vyao ikiwa hawana tofauti na star time ila wao wapo kidini zaidi na channel zao,hii ina maana kwamba kwa mwaka ujao 2011 kutakuwa na mapokezi ya vingamuzi vyengine toka kwa wamiliki wa makampuni ya habari Tanzania,ugomvi wa kibiashara ndio sababu ya kuwaumiza watanzania kwa kuwalazimisha kujaza decoder majumbani kwao.......!!
Star times ilitosha kabisa kukidhi mahitaji ya watanzania ijapokuwa Easy tv nao walikidhi ila sijui sababu ni nini mpaka wakatolewa maana na TBC kuamua kuanzisha ya kwao ambayo channel zote za Mengi hazipo,ikisemekana hawataungana maana wana ugomvi wa kibiashara,huku easy tv ikiwa na channel zote za local mpaka TVZ.....!!
Ni meengi sana kipindi tunaendelea kukumbuka lichukue hili...!!
Share:

Dec 26, 2010

Boxing day nime7babisha like this......!!!

Ikiwa ni siku 1 baada ya kusherehekea sikukuu ya x-mass,kilichofuata ni kupeana zawadi kwa kwenda mbele nami nina wangu wa kuwapa banaa...!!
Unadhani zawadi kwangu itakuwa ni nini kama si ku7bisha ili wengine wafurahie na familia zao na maisha yaweze kusonga mbele kama ilivyo ada ili kuutengeneza mchana na usiku,leo ni jumapili saafi kabisa nami nipo nafanya haya ambayo nimejaaliwa kufanya siku hii ya leo...!!
Unajua watu wanashindwa kuelewa kuna watu duniani wamezaliwa kwa ajili ya kuja kufurahisha watu wengine tu duniani nami nikiwa mmojawapo na kama hukulijua hilo ichukue hii na utembee nayo,ili siku ukipata bahati ya kukutana na mimi nawe uweze kufurahishwa pia....!!
Hii ni nyumba ya mtu,ambaye ana tv mbili sitting room na bed room na alitaka kuona picha clear kote kwa kutumia Satellite Dish Antenna na kila mtu kuangalia channel aipendayo kwa wakati mmoja bila kumuudhi mwengine,nami nika install FTA channel za Local na Gospel,Dish 1 ila Receiver 2,pia nikafanya Extra view upande wa DSTV na boxing day kwangu ikaishia hivii....!!
Share:

Dec 25, 2010

Near at Bondeni Hotel Magomeni mapipa

Hapa ufundi ukiendelea
Mcheza kwao hutunzwa na ndivyo ilivyo kila siku ziendazo kwa mungu,hapa ni Magomeni mapipa yaani ni mitaa ya nyumbani wenyewe wanasema mitaa ya kujidai ni karibu na Bondeni hotel ambayo inaonekana kwa mbele kule yenye rangi nyeupe kwa wenye macho....!!
Hapa banaa ilikuwa tatizo local channel hii dish ilifungwa kitambo isipokuwa ilihama tu kidogo kwenye position yake,hivyo nikafanya nilichokifanya ikawa heee watu wanaona wabongo na wazungu wazungu,nami nikachukua vyangu nikachapa mwendo kujiandaa kula chakutoka cha x-mass....!!
Share:

Dec 24, 2010

Tuanaendeleza mbio kama kawaida....!!

Unaambiwa kimbia kipindi wenzio wanatembea....!!
Ila mbio ukimbiazo isije ikawa upo nje ya mstari kiasi kwamba unachoka kabla ya kufika utakapo...!!
Mda huo yule aliyekuwa ananyata anakupita kama anamsukuma mlevi vile...!!
Nashukuru mpaka kufikia hapa ila kiukweli nipo bize sana wale walionitumia email then sijarepply si kwamba nimewapotezea laa hasha ubize ndo unao7bisha na ambacho naweza kusema tupo pa1 daima zaidi ya yote nawatakia sikukuu njema...!!
Share:

Dec 21, 2010

Nawatakia x-mass njema wadau...!!

2010 inaishia na sikukuu nazo ndivyo hivyo zinamalizika malizika kwa mwaka huu...!!
Kila mtu,kila nyumba,maofisi nk. watu wana mishe mishe za sikukuu ya x-mass na mwaka mpya,si mbaya nami nikawatakia maandalizi mema mpaka kufikia sikukuu wadau wote popote mlipo...!!
La msingi nawasihi msherehekee kwa amani na utulivu,huku mkijiuliza je mwaka unaishia huu lipi ambalo ulipanga kufanya limefanikiwa na kwa kiasi gani? ili mwaka unaoanza 2011 uanze na kila ulichokiacha,tufanye hivyo ili tufanikishe ujenzi wa Taifa letu pendwa Tanzania.
Share:

MAFUNDI WA DSTV NA DISH NYENGINE ZA BURE!!

 Je umewahi kukutana na usumbufu wa Mafundi wenye uwezo mdogo ama usumbfu wowote!!??
Je unahitaji kufunga DSTV mpya kwa bei halali bila kuongeza cha juu!!??
Je unahitaji kufunga Dish yenye channel za bure na ukaondokana na usumbufu wa kila siku kuita ita fundi!!?
 
 Fund dish akifunga Dish ya channel za bure
 
 Umeionaje hapa
 
Kwa Mafundi wa Dish Antenna aina zote na bei nafuu hapa ndipo mahala pake!!
Uzoefu usiokipimo na utapata ushauri bureee!!
Ufunge popote pale iwe Hotelini,Ofisini,Nyumbani na popote upendapo ndani ya Tanzania!!
Kuwa miongoni mwa walionufaika na huduma bora!!
0659161111
Share:

Dec 20, 2010

Zijue channel za nyumbani zinazopatikana kwenye Dish..!!








Hizi ndizo channel za Tanzania zinazopatikana kwenye Satellite Dish,ambayo inaanzia ft6 na kuendelea kwa kutumia C band lnb 1.
Unaweza ukajiuliza inakuwaje mtu anafunga dish kwa channel hizo tu,ila ambacho kitakuongezea ni channel za nje zikiwemo habari,movie na mengineyo...!!
Idadi ya channel inakuwa nyingi ama chache kutokana na idadi ya lnb na ukubwa wa dish pia lakini dish inayoanzia ft6 unaweza ukaona channel zaidi ya 60 zikiwepo na hizo hapo juu za channel Tanzania.
Share:

Dec 19, 2010

Dish hii haina uwezo....!!

Dish ndogo ( ku satellite dish ) haina uwezo wa kukamata channel zilizopo cband kama kwa mfano channel za Tanzania,pia haina uwezo wa kuondoa chenga zilizopo kwenye Antenna uliyofunga kwa ajili ya local kwani haina muingiliano wowote na channel zilizopo kwenye transmetter zaidi ya yote inatumia lnb ndogo tu.
Kwa kuongezea ukifunga Dish huwezi kumuona jirani yako akiwa anafanya mambo yake,maana wapo wanaoamini na kutoa soga za kwamba ukifunga dish ndo kila kitu hata mwizi wako unamuona jamani jamani si hivyo hayo mambo ni ya CCTV camera,nadhani nimesomeka......!!

Share:

Watu wanavyotafuta pesa......!!!

Ili mkono uende kinywani na hata ukikosa kicheko basi likutoke tabasamu ni lazima pesa zikutembelee,hata zikiwa za msimu na kwa kulijua hilo ndo maana watu wanaamka asubuhi wanajituma sana ilihali ankala ipatikane na maisha yaweze kwenda as usually banaa....!!
Kipindi wewe unaumia kutafuta pesa mwengine anaumia jinsi gani atakavyokuchukulia kiulaini na kuondoka nazo,akikuacha kwenye majuto ya ningejua ningenunua hata nanii... ila inakuwa ushachelewa wenye kazi zao washachukua mahela yao...!!
Kiukweli nilichogundua tunapenda sana shortcut ya maisha ila tunasahau misemo ya wazungu yenye maana kubwa sana,NO PAIN NO HONEY au NO GANE WITHOUT PAIN sasa iweje tupende vizuri bila kutaabika...??
Maisha ni magumu sana tena na bila kujituma kamwe hauwezi kutoka na kupenda shorcut madhara yake ni makubwa sana,pesa bila kufanya kazi ni sawa na kulipwa kabla ya kazi maana kazi utakuja ifanya tu siku za usoni,tena inaweza ikawa ni ngumu kuliko malipo ambayo ulikwishapokea,kuwa makini especially vijana wenzangu..!!
 Hii ni picha tu ambayo najua itakuwa imewatamanisha wengi na kudhani nina zaidi ya hizo kwenye akiba yangu kumbe ni picha tu wanaharakati wenzangu....!!
Nimeandika hii kutokana na jamaa fulani ambao waliwahi kunipigia simu kitambo kidogo,wakidai kunifahamu sana na kudai kuna wazungu wamefikia hotel hapa dar na walitaka kufanya biashara hivyo hawana mwenyeji,jamaa mmojawapo katika mtandao huo ambaye alijifanya yupo mkoa na ndiye ananijua mimi kwa maelezo yake,akaomba mimi niwe mwenyeji na kuna madawa ya mazao ama kitu kama mifugo ambayo yanapatikana s.group hivyo niwe kama mtu wa kati then nitapata % fulani....!!
Kusema kweli alivyokuwa ameanza huyo jamaa ndipo alipokosea na nikagudua hanijui bali alipata contact zangu kutoka mtandaoni ama kwa mtu hivyo hata dili yenyewe ilikuwa ya uongo kama jinsi alivyoanza nami nikawapotezea.....!!
Baada ya muda jamaa yangu mmoja nae akanihadithia kama ambavyo mimi nilikumbana nayo ila yeye ikawa wamefika kwenye suala la kutakiwa kutoa pesa kidogo ili apate kingi....!!
Kama ni watanzania ama wageni tunaenda wapi....???
Umakini katika pesa iwe wa hali ya juu otherwise mtalia jamani.....!!
Share:

EURO MIND Antenna

Si wanainchi wote ambao wana uwezo wa kufunga Dish ama king'amuzi kutokana na hali ya maisha jinsi ilivyo na kwa upande wa pili pia si channel zote za nyumbani zinazopatikana kwenye Satellite Dish ama hata penye king'amuzi pia,hivyo swala la Antenna linabaki pale pale kwamba ni la muhimu si uwezo ijapokuwa linahusika pia.
Kwa wapatao tabu kuhusu Antenna ipi inaweza ikawasaidia kuona picha clear kutokana na eneo waishilo,jibu ni moja tu EURO MIND Antenna na ikitokea haishiki basi ujue eneo lako halistahili Antenna.
Kwa wale wenzangu na mimi wa uswazi kuna zile tube ambazo unazifanyia mambo na kuwa bonge la Antenna.
Share:

KU na minara dam dam....!!

 Lau ingelikuwa nainstall C band hakika ningekesha bila kuwa na single solution cable kwa kuwa kungekuwa na kitu kinaitwa interference maana uwapo mnara either wa simu ama mitambo mitambo Satellite Dish hasa C band linakuwa kama linakingwa hivi ama kupungua uwezo wake wa kukamata sawia satellite husika,baada ya wataalamu kulijua hilo wakatutengenezea kifaa ambacho kinaweza kuimili mikiki hiyo nayo ni SINGLE SOLUTION CABLE hii ni kwa Dish kubwa tu...!!
Kwa dish ndogo ni nadra sana kutokea interference hata kama kuna mnara mbele kama nilivyoinstall hiyo DSTV maeneo ya Afri center na mambo yakawa swaafiii...!!!
Ukienda mbali zaidi zipo lnb za dish ndogo ambazo nazo kazi yake ni kukabiliana na interference....!!
Share:

DSTV OFFER IMEFANYA USIKU KUWA MCHANA...!!

Hapa ni maeneo ya sinza karibu na shule ya msingi GRACE,nyumbani kwa mdada mmoja hivi anafanyia kazi pale tigo mliman city,kutokana na ratiba kuwa ngumu katika kipindi cha offer ikatufanya tufike saa 12 jioni na kutulazimu tusababishe ili watu waone walicholipia na usiku ukatukutia hapo.......!!
Lakini pamoja na hayo mpaka kwenye saa mbili kasoro ikawa wanaume tunachapa mwendo na siku ikawa bulubulu kama zege halikulala maana ingeharibu ratiba ya kesho.....!! 

 Kutoboa matundu na drill ili kufunga stend ya Dish ya DSTV

 Hapa kutafuta signal ya DSTV

 Stend imekaa inavyotakiwa

 
 Hapa signal ya kutosha picha inaonekana


Finder inafanya kazi nyakati zote kutokana na mazingira nikiwa na maana ya kuwa hata usiku pasipokutumia taa yenyewe ina taa ambayo inaweza kujiteemea hata kwenye giza totoloo....!!
Share:

Dec 18, 2010

AV selector

Kuna TV nyingi ambazo zina AV moja ama mbili na mtumiaji akawa ana vya kuchomeka zaidi ya viwili.
Mf: ana DVD,Receiver,Decoder,King'amuzi na Game labda,hapo hapo TV yako ina AV moja ama mbili hivyo itakuwa inakulazimu kuchomoa na kuchomeka kila muda ambao unataka kuangalia kimojawapo kati ya hivyo,ambapo itakuwa usumbufu licha ya hivyo pia ile kuchomoa chomoa kila wakati AV cable ni rahisi kukatika.
Napenda kukujuza ambacho labda ulikuwa hukijui....!!
kuna kitu kinaitwa AV selector kazi yake ni kuunganisha vyote kwa wakati mmoja,nikiwa na maana ya kuwa kama ni DVD,Receiver,Decoder,King'amuzi na hata Game na vyote ukaona bila kuchomoa chomoa...!!


Kazi yako itakuwa ni kubadili kwa kubonyeza AV selector yenyewe kwa namba husika kwani katika kuchomeka kwako kutakuwa na namba kwa kila ambacho utachomeka kama DVD no.1,Receiver no.2 na vilivyobakia kwa mtindo huo huo hivyo itakuwa ukibonyeza namba 1 itaonyesha DVD,namba 2 Receiver na vyote kulingana na jinsi utakavyobadili.
Kuna AV selector ambazo zinatumia remote na zisizotumia,kuna za umeme na zisizotumia umeme,kuna kuanzia njia tatu na kuendelea.

Share:

Segerea ilikuwa pangu pa kavu....!!

Offer bado inaendelea nami nazidi kusababisha watu wafurahie maisha,nilikuwa maeneo maeneo wanapaita segerea ambapo nyuma ya nyumba hizi ndipo ilipo gereza la segerea.....!!
Hapa tatizo kubwa lilikuwa ni pa kufunga dish maana nyumba ilikuwa imejengwa kiaina yake,kwa kawaida ili dish likae kwa uzuri na usimwite fundi kila baada ya muda ni lazima tudrill ukutani lakini sometimes inakuwa haina jinsi kama ilivyo hapa na ndio tukaamua tufunge kwenye mbao ili tu mwenye yake aweze kuona kama yalivyo matakwa yake......!!
 Tumeangalia ubora wa mbao kama kweli unaweza kubeba dish na ndipo tukafunga maana unaweza ukafunga ile unaondoka tu unapigiwa simu ya kwamba dish lipo chini....!!









Share:

Dec 17, 2010

IZUNGUKE DUNIA UKIWA NA TV YAKO NYUMBANI.......!!

Unaweza kuona channel ya taifa lolote ambayo ipo katika satellite katika ukanda huu wa Africa mashariki,tunakuwezesha kupata kujua na kuona kila kinachoendelea up to date kana kwamba upo nchi husika,tunakufanya usiichoke TV yako zaidi ya yote utamani kuibeba ba kutembea nayo popote uendapo...!!
Kuwa wa kwanza kupata habari kwa kuangalia vituo vya kimataifa vya habari na utaweza kuburudika na kujifunza zaidi kwa channel za ndani na za nje clear bila chenga....!!


Share:

Dec 13, 2010

Buriani DR REMMY..........!!!

Kiukweli kila kukicha tunapoteza wakongwe katika fani,inasikitisha ila mwisho wa yote inakuwa hatuna jinsi kwa7bu tumezaliwa ni lazima tutakufa isipokuwa tunachogopa ni kutangulia tu....!!
Kifo cha DR REMMY kamwe hakitasahaulika na hakuna wa kuziba pengo lake,kila mtu atakumbuka kwa style yake ila kwangu mimi ni zaidi ya ambavyo wengi wanadhani...!!
Mimi ni kati ya wale watanzania wachache waliopata bahati ya kuzaliwa mjini tena ni maeneo ya sinza pale nyuma ya shule ya Mashujaa kiasi kwamba ukitoka tu nje unakutana na kanisa....!!
Hivyo nikisema hivyo wale ambao wanakumbukumbu nzuri watakumbuka enzi hizo yaani nyumba za hapo kulikuwa na muingilianowa watoto sana yaani hakukuwa na mipaka kwa jinsi tulivyoishi enzi hizo so watoto wa DR REMMY walikuwa home hawapungui nasi kwao kama kawa...!!
Ila tulikuja kuhama sinza mwaka 1993 ambapo ndo ukawepo umbali,kiukweli nimesikitishwa sana poleni sana wana wa familia ya DR REMMY na wapenzi wote wa mkongwe huyu ambaye alikuwa JEMBE.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi,Ameen.
Share:

Dec 12, 2010

c channel zote zinazopatikana kwenye Dish

Swali ambalo daily nakutana nalo kwa kila ninapoinstall Dish hasa kwenye makazi ya watu....!!
Unafunga dish ndogo channel za Emanuel gospel mtu anaulizia local zinapatikana ngapi...??
Unafunga futi sita local mtu asipoiona C2C anahoji kunani...??
Hivyo ni vema ukajua unachotaka na utakachopata kabla hujahudumiwa....!!
Nimegundua ya kuwa wateja design hii ni wale ambao wameenda nyumba ya fulani kaona channel fulani nae wakati anataka huduma anataja ile channel aliyoipenda na kuiona bila hata kujua zimefungwa dish ngapi nje,na ndo maana tunaamua kutoa darasa kabla ya kumuhudumia mteja nawe kuwa huru kuuliza...!!
Share:

Week end ndo inaishia hivyo...!!

Muda huu ndo week end inaishia kwangu mimi ila najua kwa wengine ndo kwanza wanaamka sasa na kutafuta pa kwenda,ila kiukweli kila mtu na starehe yake............!!!
Leo nilikuwa sehemu 1 wanapaita mbezi salasala nika7babisha watu waone DSTV then nikajirejesha home na ndo nipo mpaka sasa natuma post hii....
maana yake sina mpango wa kutoka tena kwenda popote najiandaa kuianza Monday.....!!

Share:

Dec 10, 2010

ROYAL PUB....!!

Kiukweli mimi sio mpenzi wa mpira ila afanyae vizuri stahili zake pongezi,leo nilikuwa hapa Royal pub ambapo nilifunga DSTV pamoja na projecter si leo ni muda sasa ila leo nilikuwa hapa kuhakikisha mpira wa leo unaonekana vema pasipo kutokea tatizo lolote na ndicho kilichotokea watanzania wameangalia vema jinsi time ya Tanzania iilivyoichakaza Uganda....!!
Bao lilopatikana kwa njia ya penati,ambapo Juma kaseja ameweza kudaka penati 1 huku kipa wa timu ya uganda kutoambulia hata penati 1...
Share:

Hali ya hewa c shwari dar.....!!!

Kiukweli ikiwa kijijini wanaomba mvua mjini tunaichukia mvua kwa kuona ya kuwa haina faida yeyote kwetu kutokana na ukweli kwamba shughuli nyingi zinasimama ama kuchelewa kutokana na hali ya mvua ila mwisho wa siku inakuwa haina jinsi sababu ndio kudra ya m'mungu analopanga binadamu hawezi pangua....!!!
Kwa upande wa DSTV usishangae upo ndani unaangalia huku mvua kubwa unanyesha unaona inakatakata mfano wa CD iliyochunika,ukataka kumwita fundi wala usisumbuke kwani ndo kawaida ila ikikata mvua nayo inatulia kama kawaida,ila kwa madish ya free haina kukata huendelea kuonyesha vizuri muda wote...!!!
Kipindi hiki ndo kipindi cha kujua ubovu wa Dish lako kwako kama pembe la ng'ombe halifichiki....!!!
Share:

Dec 9, 2010

UHURU DAY ilivyokuwa......!!

Tarehe kama ya leo ila miaka 49 iliyopita hayati mwalimu J.K.Nyerere na viongozi wengine walisababisha siku hii iwe tunaikumbuka kila mwaka na kuifanya siku ya kihistoria,kwanini kwasababu ndo siku tulyopata uhuru toka kwa watawala wetu ambao ni wakoloni,ulikuwa uhuru wa Tanganyika ambayo sasa inajulikana kama Tanzania.
Leo ni mapumziko na kila mtu anaifurahia kwa mtindo wake,ambapo kitaifa ilifanyika uwanja wa taifa wenye nafasi walienda lakini mimi nilikuwa kazini kama kawa na haya ndo niliyoya7babisha leo uhuru day.....!!!












 Unaweza ukashangaa vipi Dish la DSTV lakini kuna Reciveiver ya Media com badala ya Decoder ya DSTV,hapa bana nimeinstall channel za Gospel ambazo ni free zipo 30,hazina uhusiano wowote na DSTV ila kwasababu dish zinaingiliana ndo maana tukatumia hilo.....!!!
Share:

Dec 3, 2010

Mfumuko wa VING'AMUZI Tanzania....!!

Watanzia tulizoea ili picha ya TV ionekane clear na uweze kupata channel za nyumbani na za nje kwa kutumia Decoder/Receiver sambamba na Satellite Dish Antenna,ila sasa ni tofauti maana unaweza ukatumia Decoder na Antenna ukapata channel clear kabisa.
Ilianza EASY TV ijapokuwa hawajajitangaza vema ila kiukweli wamekuja vizuri na bado wanafanya vizuri maana unapata local channel karibu zote yaani zile zilizo kwenye transmeter na zilizo kwenye satellite,pia unapata channel nyengine za mataifa ya nje yakiwemo habari.( hawa ni wachina )
Hata mwaka bado toka tutamburishwe STAR TIMES nayo ina channel za local ambazo hazifiki hata tano,pia channel za mataifa ya nje yakiwemo habari.( hawa ni wachina na TBC )
Tena imekuja ATN nao wana vinga'amuzi vyao ambao wapo sana kidini.
Hii inaonyesha kwamba kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo ongezeko la ving'amuzi linakuwa kubwa kutahamaki ukitaka TBC ununue king'amuzi,ATN ununue king'amuzi,STAR TV ununue king'amuzi,ITV ununue king'amuzi na nyenginezo......!!
Share:

UFUNDI si uchafu bali ni tabia ya mtu.....!!!

Hii inatokana na ukweli kwamba mshangao umekuwa mkubwa sana mtu nikimwambia mimi fundi.....!! 
hata nikimwambia habari ya kuhusu madish anadhani ya kuwa labda mimi ni sales yaani nitaongea nae then wafungaji wataenda wengine mwisho wa siku inakuwa tofauti na adhaniavyo...!!
wananikuta ni mimi nikiwa na team yangu eneo la tukio tukisababisha,nimegundua kwamba ni kutokana na muonekano wangu,umri na mengineyo ila kikubwa ni kazi.
Napenda kuwaambia mafundi wenzangu kwamba hatuna tofauti na madaktari,hivyo hatuna budi kujithamini ili wengine watuthamini na kuwa katika hali ya usafi muda wote.
Share:

CRDB bank na pita pita zangu....!!!

Katika mwaka huu banaa nimepata wasaa ya kupita pita katika matawi kadhaa ya CRDB bank,nilianzia pale Mliman city branch,nikaja pale Azikiwe branch na leo nipo hapa Mikocheni branch.
Hili bana ni tawi jipya,hapa ilifungwa DSTV ila ikawa kesi kubwa ni kupoteza signal,katika kutafuta 7bu nikagundua ya kuwa ilipofungwa ilikuwa si sehemu sahihi kutokana na kuwa na movement nyingi eneo hilo la mafundi wa AC.Hivyo nikaona solution ni kulihamisha kutoka chini na kuliweka juu na ilikuwa kama ifuatavyo:-

Hii inaonekana imekaa vema ila tatizo likawa inaguswa guswa,mfano tulikuta ngazi ya mafundi wa AC na ndo ambao walifanya tuitwe baada ya kuigonga na ngazi yao hiyo ya mabomba bomba.



 Ili tatizo liishe nikaona ni vema kuihamisha na kuiweka juu ambapo ni ukutani.




Hapa wafanyakazi pamoja na wateja wanasafisha macho kwenye hii flat.
nami kipindi hicho nakusanya kilicho changu na kuchapa mwendo.....!!

Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita