Kiukweli muda kidogo sijafanya kazi za local channel,si mpya wala ya kuirudi ya zamani kuwa mpya kutokana na ukweli kwamba ving'amuzi vimekuwa vingi na wadau wengi nawauzia vya malipo ya mwezi tu!
Ila leo imenirejesha kuleee ambapo ilikuwa kwa siku nafunga dish mbili mpaka 3 zikiwa mchanganyika mpya na zile za kuzirejesha kuwa mpya!
Leo nimeamka na Dish la channels za Tanzania za bure na si za Tanzania tu hata za nje zote zikiwa za bure,nikimaanisha hazina malipo ya mwezi!
Jamaa yeye hakutaka Azamtv,wala DSTV,wala Zuku tv,hata startimes kifupi king'amuzi chochote cha kulipia yeye kajichanga na kutaka hili la futi 6!
Ukizingatia ni kazi yetu tukafanya yetu kama kawa then tukachapa mwendo huku tukiacha zile za Mengi ITV,CAPITAL,EATV zikiwemo,CHANNEL 10 nayo,kuna tv ya taifa TBC1,pia wale ndugu zangu wa mwanza STAR TV kwa upande wa tanzania na channels nyingi za nje.
0 Unasemaje..??:
Post a Comment