Call / WhatsApp +255673378129

Jun 7, 2014

DSTV YA KUCHAKACHUA!

Maswali yamekuwa meengi kuhusu Receiver gani sahihi ya kuweza kupata DSTV ya wizi!!
Ijapokuwa Receiver ni nyingi na kila kukicha zinakuja namna za kufanya wizi huu yaani kufungua channels ambazo zinalipiwa kwa kupata kwa gharama ya chini sana ambayo kwa lugha nyepesi ni bure lakini jibu hakuna Receiver nzuri ya kuchakachua DSTV ama channels nyengine za kulipia wewe utake kupata bure!
Narejea tena HAKUNA receiver ya uhakika ya kuibia kampuni zinazotoa huduma zao kwa malipo maalum!
Kwa watumiaji wazuri wa wizi huu watakuwa sambamba na mimi kwakuwa toka zilipoanza njia za kupata dstv kwa kuiba zinakuwa hazina uhai!
Miaka kama mitatu nyuma nakumbuka walilia watu wengi sana ambao nawafahamu na wengine kwa kunipigia simu kwa kutaka msaada baada ya kupigwa pesa nyingi ili wapate DSTV ya bure matokeo yake zikazima zote!
Wapo waliopata bahati ya kuona miezi 6 na zaidi ila wengi walipata bahati nzuri zaidi ya kupata kuona dstv ya bure kupitia hivyo vidubwana kwa week moja na wengine siku 4!
Kiukweli kila leo huwa napenda kusema shortcut inagarimu sana!
Muda ambao wewe unaumiza kichwa utaiba vipi,mwenye mali nae anaumiza kichwa atadhibiti vipi wezi msipate nafasi!
Ukifikiri vizuri DSTV wala si bei kubwa kutokana na yaliyomo,pia uzuri wake ina vifurushi kwa wenye uwezo tofauti,kwa uzuri zaidi unweza ukaanza na kifurushi cha bei ya chini na inapotokea mgodi umetema unapata hata kama mwezi haujaisha!
JIUNGE LEO KWA PUNGUZO KUBWA KABISA OFFER YA KOMBE LA DUNIA!!
TSH 129,000/=
UNAPATA KUFUNGIWA NA VIFAA VYOTE VINAVYOHUSIKA!
KISHA UNACHAGUA KIFURUSHI AMBACHO CHA CHINI KABISA NI TSH 165000/=
JIKUNE UNAPOJIWEZA!!
PIGA +255789476655/14973797/659161111 UUNGANISHWE SASA!



Tukiwa katika kuunganisha wateja wapya!

Share:

7 Unasemaje..??:

Anonymous said...

kaka mimi nahitaji hiyo ya kuchakachua hata kama haina uhakika maana yenyewe bei juu sn!

Anonymous said...

Kaka mimi nahitaji hii dstv ya kuchakachua hata kama haina uhakika maana yenyewe bei juu sana je napataje!!??

Anonymous said...

Upo sahihi mimi ni mmojawapo mwa waliopata ushawishi wa kununua q sat lakini tatizo lake ndio hivyo nimeangalia yapata week 2 lakini sasa hakuna kitu,pia ilikuwa inakuwa scramble mara kwa mara ndipo nikaonelea kuwa mwanafamilia wa dstv kwa kufuata taratibu!

Anonymous said...

Mi nataka ya kuchakachua bei gn!?

Anonymous said...

Usitupigie matangazo tutachakachua mpaka kieleweke

Anonymous said...

We need free

Anonymous said...

Continental nao hao! Scrambled toka 15.1.2016

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita