Idadi ya simu ninazopokea kwa takribani wiki tatu mpaka leo hii ni wateja wa baadhi ya ving'amuzi ambavyo vimekata matangazo yao bila taarifa yeyote kwa wateja wao na kitu kibaya zaidi ushirikiano unakuwa sio mzuri kwa mujibu wa wateja wanaonipigia mimi!
Ving'amuzi vilivyokata ni ZUKU tv.
Ijapokuwa ikarejea hewani ila hakukuwa na taarifa yeyote ama kuwataka radhi wateja wao.
TING nao wakapotea hewani mpaka leo hii na mchezo ni ule ule hakukuwa na taarifa wala kuomba radhi kwa kwa nguvu ile wanayotumia kuuza ving'amuzi!
CONTINENTAL pia hawapo hewani!
Ubaya ambao unatokea hapa taarifa na kuwataka radhi wateja hakuna kwa nguvu ile wanayotumia kuuza king'amuzi na kwa bahati mbaya Continental wana nafasi nzuri ya kufikisha ujumbe kwa umma kupitia Startv ama RFA lakini matangazo yanayoendelea ni yale ya kuuza ving'amuzi!
ANGALIZO TOKA KWA MUSTAPHA MADISH:
Tatizo lililopo kwa Continental na Ting ni satellite waliyopo ya Amos 5:-
Jukumu la makampuni waliyopo Satellite hii walitakiwa watoe taarifa kwa wakati kwa wateja wao ili waendelee kuwa na imani nao kwa maana ipo wazi kifundi tunajua Satellite ya Amos 5 haipo tena imepotea hivyo ili Ting na Continental ni lazima wahame Satellite je watahamia Satellite gani hilo wanalijua wahusika.
Yapo matatizo ambayo huwezi kuyazuia kwakuwa najua vema mfumo mzima ulivyo,yapo ya kuepukika na yapo ambayo hayaepukiki,ila kinachopaswa kufanyika ni kutoa taarifa kwa wakati kwa wateja wenu na kwa umma kwa ujumla huku mkiendelea kutatua tatizo kwa wakati,kukaa kimya kwenu ni kupoteza imani kwa wateja wenu,inaonekana mnatoa huduma mbovu na hii inapelekea kufanya maamuzi ya kuamua kununua king'amuzi kingine!
+255789476655