Call / WhatsApp +255673378129

Mar 10, 2016

CUSTOMER CARE ZA VING'AMUZI TANZANIA


Katika vitu wanavyofail karibia makampuni yote ya ving'amuzi Tanzania ni CUSTOMER CARE ingawaje baadhi ya makampuni wameboresha lakini si kwa kukidhi mahitji ya wote..
Nilichogundua ni kwamba wateja wengi hawapendi kupokelewa na mashine,muda ambao mteja anasikiliza sauti iliyorekodiwa salio lake linaendelea kuliwa matokeo yake mteja anaweza akatumia zaidi ya 5000 na bado hapati nafasi ya kuongea na mhudumu na mara nyingi simu za makampuni za ving'amuzi huwa ni za mezani ( Landline ).
Kampuni moja tu ya king'amuzi Tanzania ambayo simu zake kama utatumia mtandao unaofanana na hizo namba inakuwa bura huliwi shilingi yako,hili ni zuri na makampuni mengine kama wangetumia utaratibu huu ingekuwa ahueni ijapokuwa tatizo la simu ni moja kati ya matatizo makuu!
Ukiachilia utafutaji wa mtoa huduma kuwa wa tabu pia unapompata huyo mtoa huduma anakuhudumia kana kwamba yeye ndiye aliyekupigia bila kujali kwamba wewe ndiye uliyepiga na huna salio la kutosha na ikitokea simu yako ikakatika pasipo kumaliza tatizo lako hata hawasumbuki kukupigia wakiamini lazima utaweka vocha na kuwapigia tu...
Kuna hili nalo mteja anayekuhudumia unamwambia tatizo lako,inaonyesha uelewa wake mdogo shortcut anaona ni kukwambia ubebe king'amuzi chako na kukipeleka katika ofisi zao,ambapo tatizo hilo linaweza likaelekezeka kwenye simu na tatizo likaisha..
Mbaya kupita zote ni hili la namba za Customer Care kutokuwa hewani muda wa kazi tena inaweza ikawa zaidi ya wiki moja hili ni tatizo!
Kwa leo ni hayo tu!

MUSTAPHA HANYA
mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

2 Unasemaje..??:

Anonymous said...

Hiki ambacho unakisema ni sahihi kabisa kaka ila nadhani ujumbe umewafikishia

Unknown said...

Kila ninapolipia kifurushi napata sms inayonijulisha kuwa Nina balance ya shs 42,200.Nataka kuzitumia kulipa mwezi huu. Nifanyeje

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita