Call / WhatsApp +255673378129

Jun 30, 2016

KUFUNGA DISH NDOGO ( KU DISH INSTALLATION )

Kwakuwa karibu Ving'amuzi vyote Tanzania vinatumia Dish ndogo leo niwape kasomo haka alau mwenye kujaribu na ajaribu atakapopata wasaa!!
Fanya haya ili uweze kufunga Dish ndogo:-

1.Dish Antenna Assembly:
- Unganisha kifaa kimoja kimoja kama karatasi ya maelekezi inavyoonyesha ili kulikamilisha dish lako bila kuacha hata kimoja kwakuwa kila kimoja kina kazi na umuhimu pia.

2.Unganisha stendi yako ya kubeba dish.





3.Angalia sehemu nzuri ya kufunga Dish ili uanze kufunga stendi yako:
- Hakikisha sehemu unayoifunga mbele hakuna miti itakayozuia kupokea signal.
- Sehemu imara itakayoweza kukaa Dish bila kucheza.
- Unashauriwa kuifunga juu ya usawa wa nyuma/jengo ili isipate kuguswa guswa.

4. Funga stendi yako ya dish sehemu ulipoona panafaa.
5. Funga Dish lako kwenye stendi kwa kulielekezea Satellite uliyoikusudia ( Muelekeo wa king'amuzi husika )
6. Unganisha Coaxial cable ( Signal cable ) kwenye king'amuzi chako kwa nyuma sehemu iliyoandikwa LNB IN kisha unganisha kwenye either kwenye Dish sehemu ya LNB ama kama utakuwa na kitafuta signal (Signal  Finder ),kama utatumia Finder lazima uwe na Test cable ( Kipande cha cable ambacho utachomeka toka kwenye finder mpaka kwenye dish ( LNB ) - Nimetoa mfano wa Finder hii kwakuwa ni rahisi kupatikana na hata bei yake ni ya kawaida ila kuna finder nyengine hazihitaji Test cale.
7. Upo tayari kwa kuanza kutafuta signal. Jinsi ya kutafuta signal ntawaletea somo hilo katika post nyengine!
Tuangalie kwenye video hapo chini!



+255 789 476 655
Share:

5 Unasemaje..??:

Unknown said...

VP unaweza kutumia dish moja kwa ving'amuzi mbili tofauti mfano Azam na startime

Buly's blog said...

Ndio unaweza but unabadili uelekeo kwa ninavojuwa

Unknown said...

Kuangalia signo ya statement unaongezea kurugenzi gan

Unknown said...

Mi mzoefu wa kufunga king'amuzi cha azam ila zuku bado sijawahi ninanomba msaada wa uelekeo wa dish

Unknown said...

Msaada jins ya kufunga dish la zuku

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita