Call / WhatsApp +255673378129

Aug 1, 2016

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI STARTIMES


Wateja wengi wa Startimes wanakumbwa na kadhia hii,kutokujua utaratibu kwa kutaka kuhama kutoka kifurushi kimoja kwenda kingine hivyo kwa post hii utaelewa vema jinsi ya kuhama kifurushi na utaondokana na ile adhabu ya kufanya malipio kwa lengo la kupata mwezi mzima matokeo yake unapata kuona kwa muda wa wiki 1 tu!
Kwanza vijue Vifurushi vya Startimes kwa kubofya Hapa
Ikitokea umelipia kifurushi cha Smart Tsh 18,000 na mwezi umeshaisha unataka kulipia kifurushi cha Smart+SportPlus Tsh 32,000 unaweza kufanya hivyo kwa kufata utaratibi huu:-
Kabla ya kufanya malipo chukua simu yako bonyeza *150*63# kisha piga utapata ujumbe huu
Karibu StarTimes
Chagua:
  1. Kiswahili <
  2. English
( Tunachagua kiswahili,una bofya OK )
  1. Kujua salio
  2. Kulipia kwa vocha
  3. Sajili dekoda yako mpya
  4. Q and A ( Swali na Jibu )
  5. Chagua kifurushi <
( Unachagua "chagua kifurush,una bofya OK" )

Ujumbe utakaoupata ni:-
  • 1.DTT ( Antenna )
  • 2.DTH ( Dish ) <
Chagua kulingana na king'amuzi unachotumia,hapa nitachagua cha Dish

Ujumbe utakaoupata ni:-
  • Tafadhali ingiza tarakimu 11 za smati kadi yako iliyochomekwa upande wa kulia wa dekoda yako (mfano 02139xxxxxx )
( Weka namba za Smartcard yako zenye tarakimu 11,kisha una bofya OK ) 

Ujumbe utakaoupata ni:-
  1. Smart-18k
  2. Smart+SportPlus-32k <
  3. Super-48k
( Unachagua unachotaka kulipia mfano tumechagua namba 2,una bofya OK ) 

Ujumbe utakaoupata ni:-
Asante.Utapokea majibu hivi punde.StarTimes

NB:Niwe tu mkweli nilichelewa kuiweka hii post kwakuwa maelekezo yake kampuni husika imeshindwa kuyakamilisha hivyo najua ambacho mtapata ni usumbufu kwa maana hiyo utakapokwama huna budi kupiga +255764700800 ili uhamishwe kifurushi.

Share:

12 Unasemaje..??:

Unknown said...

nawezaje kuangalia channel za bure ata kama sijalipia please nisaidie usawa magu mgumu mpaka watu tuna shindwa kununua vifurush

Unknown said...

Tafadhali mutuwekee channel za bure jaman kama mulivyo tuahid awali....

Unknown said...

Mmenikatia chanel za bure soze wakati TCRA walisema vyandani hawakati

Unknown said...

Daaah hapa nimeingiza voucher ya 10000 masaa yanazidi kuyoyoma tuu sujui ndo

Unknown said...

Nashindwa kuelewa hawa star times mpaka sasa hawataki kuniunganisha vocha nimeweka 10000 mnataka na hela nyingine tena?

Unknown said...

Sawa, imeeleweka

Unknown said...

Jmny mbn mmetoa wildflower

Ramdhani Mwakaje said...

Kifurushi cha mboga hakijawekwa hivyo inakuwa mgumu Kubadili Kifurushi.

Unknown said...

Ukipiga hiyo namba haipokelewi, pia wana namba ya tigo nayo haipokelewi, ukienda mahali pa kubadilisha hupati kifurushi cha nyota, wahuni hawa watu sasa

Unknown said...

Wizi mtupu

filmtech said...

Shikamo kaka

Unknown said...

Habari natumia king'amuzi cha Antenna ila kinaniandikia kadi maalumu imekosewa lakini kadi nimeweka sahihi kabisa na nimelipia kifurushi cha 12000 lakini sasa ni nusu saa sipati Chanel. So naomba msaada by Mwaipopo

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita