Call / WhatsApp +255673378129

Dec 2, 2016

TV E TANZANIA | KWENYE KING'AMUZI CHAKO



Siku zote ili ufanye vizuri ni lazima upate mpinzani na ndicho kinachotokea hapa..
Historia inaonyesha Clouds Fm ilifanikiwa kuzipoteza radio ambazo alizikuta katika swala la burudani na kupelekea kuunyanyua kwa kiasi kikubwa music wa Bongo Flavour,mpaka ikafikia hatua hata kwa wasanii wa music huo ukienda kinyume na matakwa ya uongozi wa radio hiyo kinachotokea ni kupotea katika game ya Bongo Flavour hapo hapo bado kuna malalamiko mengi ya kwamba kuna unyonyaji!
E - Fm radio,ndio radio pekee inayoonekana imekuja kuleta upinzania mkubwa kwa radio Clouds Fm katika swala zima la burudani.. E - Fm radio wamefanikiwa kuufanya music wa Singeli kuwa biashara.. ukiacha hilo kwa mtazamo wa haraka haraka tu ni kwamba mmiliki wa E - Fm anakijua sana anachokifanya kwakuwa yupo kwenye ukanda huo muda mrefu hivyo alichoangalia udhaifu wa wengine nae akaongeza ubunifu na ndicho kinachompa na kitakachompa mafaniko zaidi..
E - Fm imepelekea kuzalisha TvE - Tanzania ni hatua nzuri sana na ya kupongeza mno..
TvE - Tanzania inapatikana kwenye ving'amuzi vifatavyo kwa sasa:-
  • Azam Tv - channel namba 115
  • DStv - channel namba 295
  • StarTimes channel namba 115
Binafsi nawatakia kila la heri katika kuboresha ili kutuongezea machaguo wapi tuangalie ama kusikiza
+255789476655
Share:

6 Unasemaje..??:

Anonymous said...

Nimeiona imekuja vizuri sana na wapotezwe hao Clouds wananyanyasa sana wanamusic wetu big up Dj Majay!

Anonymous said...

mbona kwenye startimes siioni vipii!!

Anonymous said...

Hongera kwake hakika ni faraja kuona ndoto zinatimia big up hawa jamaa wako katika kiwango cha HD kabisa time will tell ila mwonekano wake tu hata kwa kawaida wametisha sana

Emirates stadium said...

Kwenye star times chaneli 115 ni aMC na sio TV E,hebu acheni uongo msitudanganye,ongeeni na star times waiweke chaneli yenu,maana nimeisearch manual na automatically kwa kinga'amuzi yangu bila mafanikio

Unknown said...

Enter your comment...AHSANTENI TV E MMEWEZA KUNIFANYA NING'AE KUPITIA NYIMBO YANGU YAKESHA INAYO ONGOZA KUPIGWA PLOMO KATIKA CHANELI HII KAMA BEN SWAX TAKUWA NANYI PAMOJA NA MUNGU AWABARIKI SANA

Anonymous said...

I am sure this article has touched all the internet users, its
really really fastidious article on building up new blog.

Website: http://herb24.space

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita