Call / WhatsApp +255673378129

Apr 15, 2016

AV CABLE NI NINI!?


A inasimama badala ya Audio - Sauti
V inasimama badala ya Video - Picha
Zinakuwa nyaya tatu zenye rangi tatu tofauti:-


Nyekundu - Sauti Kulia
Nyeupe - Sauti Kushoto
Nyano - Picha


Hivyo tafsiri nyepesi ni kwamba AV CABLE ni waya unaosafirisha Sauti na Picha kutoka kwenye kifaa chochote kinachoweza kutoa picha na sauti na kuingiza kwenye TV, kifaa hicho kinaweza kuwa DVD, King'amuzi, game n.k.
Mfumo wa picha unaoonekana kwa kutumia AV cable hujulikana kama SD - Standard Definition 
 

Cable hii hutumika kwenye TV yenye AV Port yaani ile sehemu ya kuchomekea AV ambapo napo unachomeka kwa kufata rangi kama uvyoona hapo chini!


Zipo tv ambazo hazina AV port ama hicho kifaa ambacho unataka kutumia AV cable hakina AV Port ufanye nini ili uweze kuendelea kutumia AV cable ama Cable nyengine?
Unapaswa uangalie TV/DVD/King'amuzi kina Port gani badala ya AV Port?
Ufanye nini ikiwa TV yako ina AV port moja ama mbili nawe una vifaa zaidi ya viwili unataka kutumia pasipo kuchomoa chomoa AV cable?
Unapaswa kutumia kifaa kinachoitwa AV SELECTOR
mustaphamadish@gmail.com
+255789476655
Share:

Apr 12, 2016

KOPO HALISAIDII CHOCHOTE KWENYE DISH


Leo nimeonelea niongelee hili jambo kwakuwa ukiachilia kuliona sehemu mbali mbali pia nimekuwa nikulizwa kama kuna umuhimu wa wenye ving'amuzi vya madish kuweka makopo?
 Jambo la awali la kuzingatia king'amuzi kiwe cha Dish ama Antenna kina namna ya ufungaji wake kwa kutumia vifaa vyote vilivyomo kwenye set ya king'amuzi hicho,ikitokea kimojawapo umekiacha ndipo unajikuta nafasi ya kile ulichokiacha inachukuliwa na KOPO!
Kutumia KOPO kunatokana na sababu hizi:-
  • Tuanze kiufundi
- Fundi hupaswi kuacha kutumia kitu chochote kati ya ulivyovikuta kwenye set ya Dish kwakuwa vyote vina kazi yake na ni muhimu sana.

Hapa unamshawishi mteja atafute kopo lilipo ili aweze kufunika akiamini atasaidia angalau kuepusha gharama za kuita ita fundi.

Ukifunga hivi ni kipi ambacho kitamshawishi mteja aongezee ufundi wake wa kuweka kopo?
Fikra za watanzania wengi wanaamini wakifunika na kopo husaidia:-
  • Huzuia kunguru kufanya uharibifu
  • Husaidia picha kutokupotea wakati wa mvua
Niseme tu ukweli KOPO halisaidii chochoteikiwa fundi amefanyakazi safi.
Kupotea kwa Picha kwa dish ndogo kipindi cha mvua ni kawaida kutokana na uwezo mdogo ili kuepuka hili inakulazimu kutumia Dish kubwa ama lnb maalum na kuhusu kunguru fundi akifanyakazi yake vema kunguru hata abembee vipi hawezi kufanya uharibifu!
mustaphamadish@gmail.com
Share:

UMELIPIA NA BADO HUPATI PICHA!?


Hili ni janga kubwa karibia kwa wateja wote wa ving'amuzi vya kulipia,unafanya malipo lakini hupati picha kwa wakti ama hupati picha kabisa!
Njia za kufanya ili usipate usumbufu wakati wa kufanya malipo ya mwezi:-
> Kabla ya kufanya malipo hakikisha unajua bei ya kifurushi unachotaka kulipia
> King'amuzi chako umekiwasha kabla hujafanya malipo
> Ikiwa unalipia kifurushi ambacho ni tofauti na cha awali huna budi kupiga simu ama kufata njia zilizoelekezwa ili kubadili kifurushi
> King'amuzi chako kina Signal ya kutosha

Nini ufanye ikiwa umeshalipia na hukufata njia hizo:-
> Washa king'amuzi chako
> Hakikisha kina Signal kwa kuangalia channel ambayo ipo bure ( mf:ya matangazo )
> Piga simu kwenye kampuni husika ya king'amuzi unachotumia ili ufunguliwe ama upewe maelekezo zaidi na ikitokea umekosa msaada namba hii ni msaada kwako +255789476655
mustaphamadish@gmail.com
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita