Call / WhatsApp +255673378129

Showing posts with label Dstv. Show all posts
Showing posts with label Dstv. Show all posts

Jan 3, 2018

UNAZIJUA BEI NA OFFER ZA VING'AMUZI 2018!?


Biashara ushindani hivyo kuna maboresho kila kukicha kwenye swala la kukidhi haja za wateja na leo nakuletea list ya bei za ving'amuzi kwa mwaka 2017 na jinsi ya kununua kwa bei hii:-
  • Azam tv inauzwa Tsh 135,000/= Hii bila kifurushi wala Ufundi! Ila ina Offer katika malipo! Kwa maelezo zaidi Bofya Hapa
  • Digitek inauzwa Tsh .......
  • DStv inauzwa Tsh 79,000/=  Hii bila Ufundi ila ina Offer ya vifurushi vya miezi miwili! Kwa maelezo zaidi Bofya Hapa
  • Continental inauzwa Tsh .... ya Dish na Tsh 40,000/= ya Antenna. Hii bila ufundi ina Offer ya kifurushi cha miezi..! Kwa maelezo zaidi Bofya Hapa
  • StarTimes inauzwa ya Dish Tsh 78,000/= na ya Antenna Tsh 34,000/= Hii bila ya Ufundi ina Offer ya kifurushi cha miezi...! Kwa maelezo zaidi Bofya Hapa
  • Ting HD inauzwa ya Dish Tsh 100,000/= na ya Antenna Tsh 35,000 ina Offer ya kifurushi cha miezi..! Hii bila Ufundi Bofya Hapa
  • Zuku tv   inauzwa Tsh 88,000/= Hii bila Ufundi ila ina Offer ya kifurushi cha miezi...! Kwa maelezo zaidi Bofya Hapa 
  • NB: Bei zote zina mabadiliko kujua bei mpya check Whatsapp+255784378129
Zijue bei za vifurushi kwenye ving'amuzi kwa mwaka 2018 
Jinsi ya kuhama kifurushi
Kuepuka Dish lako kupata kutu
Kupata Mafundi Professional
Share:

Nov 27, 2017

ZIJUE OFFER ZA VING'AMUZI 2017 KUELEKEA 2018

Tunaelekea katika kumaliza mwaka 2017 na tunategemea kuingia mwaka 2018, yapo mengi ambayo kupitia blog hii umefaidika kwa hali yeyote ile kama ndivyo tunashukuru kwakuwa ndio lengo letu, lakini pia nadhani yapo yaliyokukera kupitia blog hii kama ndivyo tunasikitika na kukuomba radhi pia maana sio lengo letu na ukizingatia hata kama itatokea unafanya jambo zuri vipi sio wote watakaopendezwa nalo kwa kuzingatia wapo ambao lengo lao ni kuharibu tu ama kutengeneza njia ya kufanya vibaya.. Zaidi ya yote shukrani kwa wale wote walio pamoja nasi kwa mwaka mzima na hata hapo miaka ya nyuma maana bila ninyi wala mimi na team yangu tusingefika hapa na isingezaliwa MADISH TECHNOLOGY.
Leo nawaletea orodha ya ving'amuzi vyenye offer katika msimu huu wa kumaliza mwaka 2017:-
 Bofya king'amuzi ambacho unataka kujua offer yake na utapata maelezo ya kina kuhusu offer hizo!
+255789476655 
Whatsapp+255784378129
Insta @mustaphamadish 
Share:

Aug 29, 2017

DSTV YASHUSHA BEI ZAIDI | VIFURUSHI 2018


Habari njema kwa wadau wa kabumbu na wateja wote wa DStv kiujumla! Hii ni bei ilianza tarehe 1 mwezi wa 9 mwaka 2017 bei ambayo ni kama ifatavyo kwa Vifurushi vyote vya DStv:-
1.Premium kutoka 184000 mpaka 169000/= tu!
2.Compact Plus kutoka 122500/= mpaka 109000/= tu!
3.Compact kutoka 82,500/= mpaka 69,000/= tu!
4. Family kutoka 42,900/= mpaka 39,000/= tu!
5.Bomba kutoka 19,975/= mpaka 19,000/= tu!
Kwa Maelezo zaidi +255789476655
Whatsapp +255784378129
Share:

May 31, 2017

UFUNDI UNAHITAJI UMAKINI

Kwanza ukishakuwa Fundi moja kwa moja unaaminika kwa taaluma uliyonayo hivyo mteja ama jamii kwa ujumla wanajikuta wanaona unachofanya ama kusema ndicho sahihi kutokana na wadhifa wako hata kama ni cha uongo… Binafsi niwape angalizo wateja na mafundi kiujumla kwanza nianze na Wateja

Wateja – Nichukue nafasi hii kuwapongeza na kuwashukuru wale wote wanaoheshimu na kuthamini uwepo wa Mafundi . Pia nichukue nafasi hii kuwapa angalizo wale wateja wote wenye Dharau kwa kuona Mafundi si chochote ama kudharau kile tufanyacho,Mfano mteja anahitaji fundi mnazungumza habari za gharama na mnakubaliana,fundi anafika kwako na anafanyakazi yake kwa muda mchache anamaliza kutengeneza..Mteja kwenye malipo unataka upunguziwe kwakuwa kazi yenyewe ndogo tu ,hii ndo dharau nisiyoipenda hata kuisikia.. sasa kama kazi ni ndogo tu kwanini hukufanya mwenyewe!? Hivi hujui kwanini imekuwa kazi ndogo tu!? Kwakuwa ni Fundi ( Ufundi ni taaluma ) si kila mtu ana taaluma na ndo maana ukahitaji Fundi.. Hivyo tumia lugha nyengine katika kutafuta unafuu wa malipo lakini si kudharau kazi za watu. Mpe uhuru fundi afanye kazi yake si kumbana hata anakosa kuwa comfortable maana fundi akiamua kukufanyia uhuni hata ukienda nae mguu kwa mguu ana nafasi 99% ya kukufanyia uhuni.

Mafundi – Lazima ujielewe kama si kuelewa thamani yako,ujue uwezo wako pia maana kuwa Fundi si kigezo cha kujua kila kitu ingawaje wapo mafundi kwa taaluma yake anajua kila kinachomuhusu.. hii maana yake kama umekutana na Technical issue ambayo kwako ni ngeni omba msaada kwa mafundi waliokuzidi ama ukikosa msaada mwambie mteja wako ukweli kwamba hilo tatizo huwezi kulisolve.. Kamwe usiseme uongo ili tu upate pesa.. Hakikisha unakuwa makini katika kazi yako,akili yako uiweke kwenye kazi uifanyayo wakati wa kazi ili isitokee ukafanya usahaulifu wowote maana utakuwa ni uzembe na matokeo yake itakucost ila zaidi itamcost mteja wako… mfano hii picha hapa chini


Kosa dogo alilofanya limesababisha huu mkono wa dish la DStv kuliwa na kutu kwakuwa hakuweka kifuniko ambacho kinazuia maji kuingia ndani ya mkono huu wa kushika Lnb..

 hili ni kosa dogo kimtazamo ila kiufundi ni kosa kubwa sana linaweza likawa limefanywa na fundi kwa bahati mbaya ama kwa makusudi kwa kudharau vile vifuniko vya kufunikia hii mikono.. Amedril vizuri na amefunga cable vizuri lakini kilichomshusha vyeo kuonekana ni fundi kalipua ni kosa moja tu…


Tuna Mafundi wataalamu wa kufunga

  •   Azam TV
  •   DStv
  •   Zuku Tv
  •   StarTimes
  •   Continental
  •   Ting
  •   Flat Screen
  •   Projector
  •   CCTV Cameras

Waliobobea kufunga kwenye:


  •       Hotel
  •       Apartment
  •       Bar
  •       Restaurant
  •       Office
  •     Majumbani

 Tunapatikana Dar es salaam, Magomeni Mapipa.. isipokuwa mkoa wowote Tanzania tunakuja.. inategemea unataka huduma gani toka kwetu!


Piga +255678476655
Share:

Dec 26, 2016

TUNAAGA 2016 | KWA KUJITUMA ZAIDI


Mafanikio hayana njia ya mkato,ukipata kauli za wengi wa liofanikiwa watakwambia njia walipitia na kamwe hakuna njia ya mkato.. nimejifunza kutokutamani mafanikio ya mtu bila kuwa tayari kupitia hatua za kufikia mafaniko..
Mafanikio yanahitaji:-
  • Kupenda unachofanya
  • Kukijua ama jifunze zaidi ili ukijue
  • Kuheshimu na kukitetea unachofanya
  • Kujitoa
  • Kujituma
  • Juhudi binafsi
  • Kujiongeza ( kuwa mbunifu )
  • Kuwa na heshima na Pesa
  • Kutokuwa mnyimi  ama mbinafsi 
  • Na mengineyo...
Nipo kwenye ukanda huu yapata mwaka wa nane sasa nina uzoefu wa kutosha kuhusu makampuni yote ya ving'amuzi Tanzania na watumiaji wake pia ile kiundani zaidi..
Najua nimesaidia wengi ndani na nje ya Tanzania,nimetengeneza BASE kubwa mno mpaka binafsi kama siamini hivii ila hii yote kutokana na Kupenda nilichamua kufanya n nashukuru Alhamdullah!
Mwaka unaishi na tunategemea kuingia mwaka mpya 2017
mimi na team yangu ile mikono salama #FundiMakini tunakuletea kitu kizuri sana kwenye ulimwengu wa Digital Tv... Kubwa tunashukuru kwa uwepo wenu na kutupa moyo zaidi ya yote tunawaahidi kuwaletea vitu vizuri zaidi ili kila mmoja wenu ahufurahie ulimwengu wa Digita Tv!
+255 789476655
Share:

Dec 2, 2016

TV E TANZANIA | KWENYE KING'AMUZI CHAKO



Siku zote ili ufanye vizuri ni lazima upate mpinzani na ndicho kinachotokea hapa..
Historia inaonyesha Clouds Fm ilifanikiwa kuzipoteza radio ambazo alizikuta katika swala la burudani na kupelekea kuunyanyua kwa kiasi kikubwa music wa Bongo Flavour,mpaka ikafikia hatua hata kwa wasanii wa music huo ukienda kinyume na matakwa ya uongozi wa radio hiyo kinachotokea ni kupotea katika game ya Bongo Flavour hapo hapo bado kuna malalamiko mengi ya kwamba kuna unyonyaji!
E - Fm radio,ndio radio pekee inayoonekana imekuja kuleta upinzania mkubwa kwa radio Clouds Fm katika swala zima la burudani.. E - Fm radio wamefanikiwa kuufanya music wa Singeli kuwa biashara.. ukiacha hilo kwa mtazamo wa haraka haraka tu ni kwamba mmiliki wa E - Fm anakijua sana anachokifanya kwakuwa yupo kwenye ukanda huo muda mrefu hivyo alichoangalia udhaifu wa wengine nae akaongeza ubunifu na ndicho kinachompa na kitakachompa mafaniko zaidi..
E - Fm imepelekea kuzalisha TvE - Tanzania ni hatua nzuri sana na ya kupongeza mno..
TvE - Tanzania inapatikana kwenye ving'amuzi vifatavyo kwa sasa:-
  • Azam Tv - channel namba 115
  • DStv - channel namba 295
  • StarTimes channel namba 115
Binafsi nawatakia kila la heri katika kuboresha ili kutuongezea machaguo wapi tuangalie ama kusikiza
+255789476655
Share:

Oct 25, 2016

MAFUNDI WA VING'AMUZI TANZANIA


Mafundi wa uhakika wa king'amuzi chako unachotumia limekuwa tatizo kubwa hasa kwa baadhi ya maeneo,hii imepelekea baadhi ya wateja kuona yakwamba king'amuzi anachotumia ni tatizo kwakuwa hakupata Fundi makini ambaye angeweza kumfungia ama kumrekebishia ipasavyo.. Matokeo yake picha kuganda ganda ama kupotea ni jambo la kawaida sana..
Fundi Makini anapaswa kuwa na vifaa vilivyo kamilika ukiachilia spana zote muhimu pia anapaswa kuwa na Drill machine kwa ajili ya kutombolea na kingine anapaswa kuwa na kifaa cha kutafutia Signal ambacho kinaitwa Signal Finder!!
Fundi Makini akikufungia ama kukurekebishia atakupa uhakika wa miezi mitatu,maana yake ndani ya miezi mitatu baada ya kukitibu king'amuzi chako kikisumbua atakuja na kukurekebishia bure pasipo malizo yeyote!
Fundi Makini ni mwepesi kuja pale unapomuhitaji,tofauti na akina Fundi Kalipua ambao huwa ni ngumu sana kurudi ambapo ameshafanya kazi chafu!
Unatumia King'amuzi gani!!??
Kutana na Fundi wako hapo chini:-
Msaada zaidi wasiliana nasi:- Call  0784378129
                                                  Whatsapp / Call 0658046655
Share:

Oct 1, 2016

MSIMU WA OFFER 2016 | VING'AMUZI TANZANIA

 

Tunaelekea kumaliza mwaka 2016 na kutokana na ushindani uliopo katika ukanda wa Digital tv,makampuni ya Ving'amuzi yanajitahidi kutafuta namna ya kushawishi wateja wapya na kujiunga na ving'amuzi vyao huku wakiwafanya wateja walionao kutowapoteza kwa kuboresha huduma zao na kutoa OFFER!!
Vijue Ving'amuzi vilivyo na OFFER na Offer zao kwasasa:-
  1. Azam Tv
  2. DStv
  3. StarTimes
  4. Zuku Tv
Kwa msaada kiufundi na maelezo zaidi kuhusu King'amuzi chako piga:-
+255789476655 Kuanzia saa 08:30 - 18:00 Kila siku.
Share:

Sep 7, 2016

KUTANA NA MAFUNDI WA DSTV #fundimakini



Wewe ni mteja wa DStv!?
Una tatizo la kiufundi ama unahitaji Ushauri wa kiufundi?
Kupata mawasiliano ya Mafundi wa uhakika..

 Je unataka kujiunga na DStv?
Unataka kupata Mafundi wa uhakika na wazoefu?
Piga +255789476655
Ukifungiwa nasi:-
  • Unapata miezi mitatu bure baada ya kufungiwa kama itasumbua
  • Unapata ushauri wa kiufundi kabla hujahudumiwa
  • Unapata Fundi Makini na mwenye vifaa vyote muhimu
Share:

Jul 1, 2016

KUEPUKA DISH YAKO KUPATA KUTU

Niwe mkweli katika hili usipopata fundi makini uwezekano wa kuepuka hili ni mdogo sana vinginevyo muhusika uwe makini sana na Fundi wako ingawaje mara nyingi muhusika inakuwia vigumu kuona jinsi fundi wako alivyofunga Dish huko juu ya paa!!

Sababu zinazopelekea Dish kupata kutu kwa haraka:-

Sababu zisizoepukika:-

> Ikiwa Dish inafungwa ufukweni.

> Ikiwa Dish ni FAKE.

Sababu zinazoepukika:-

> Kutokuweka vinavyozuia maji kuingia.


Tuone madhara ya kutotumia vinavyozuia maji kuingia ndani na kukosa pa kutokea!
1
Hii ni Stendi ya kubeba Dish,hiki ni kikalio ( Chini ) ambapo kwa kutokufunika juu,imesababisha maji yameingia na kwakuwa hakuna sehemu maalumu ya kutokea maji yanapoingia,yenyewe yakatafuta njia kwa kutafuna kidogo kidogo mpaka kupata njia kama muonavyo!

2
Huu ni mkono wa kushika LNB,upo mfano wa V,mkono huu ni bomba maana yake kati lipo wazi,upande wa mbele inafungwa LNB ambapo inazima maji kuingia na upande wa nyuma kuna ya kukipachika ili kuzuia maji yasiingie kama ilivyoonyeshwa picha namba ( 5 ) kwakuwa yakiingia kinachotokea pale kwenye mkunjo ndipo maji yatajitengenezea njia kama muonavyo hapo juu!
3
Matokeo yake ile V inageuka vipande viwili baada ya kuliwa na kutu!
4
Ufungwaji Dish wa namna hii ndio unaopelekea madhara tuliyoyaona hapo juu kwenye picha ( 1 - 3 ) jinsi maji yalivyosababisha kutu,ambapo kama fundi angetumia vifaa vyote ipasavyo yasingetokea madhara hayo yaliyotokea!
5
Hivi ndivyo unavyopaswa kufunga Dish yako kwa kutumia Plastic cover ili kuzuia maji yasiingia kwenye bomba ya Stend na mkono wa kushika LNB!

Nadhani kwa uchache umeambulia kidogo kwa maelezo zaidi
+255789476655 
NB:Kupiga kuanzia saa 08:30 - 18:00 
Share:

Jun 30, 2016

KUFUNGA DISH NDOGO ( KU DISH INSTALLATION )

Kwakuwa karibu Ving'amuzi vyote Tanzania vinatumia Dish ndogo leo niwape kasomo haka alau mwenye kujaribu na ajaribu atakapopata wasaa!!
Fanya haya ili uweze kufunga Dish ndogo:-

1.Dish Antenna Assembly:
- Unganisha kifaa kimoja kimoja kama karatasi ya maelekezi inavyoonyesha ili kulikamilisha dish lako bila kuacha hata kimoja kwakuwa kila kimoja kina kazi na umuhimu pia.

2.Unganisha stendi yako ya kubeba dish.





3.Angalia sehemu nzuri ya kufunga Dish ili uanze kufunga stendi yako:
- Hakikisha sehemu unayoifunga mbele hakuna miti itakayozuia kupokea signal.
- Sehemu imara itakayoweza kukaa Dish bila kucheza.
- Unashauriwa kuifunga juu ya usawa wa nyuma/jengo ili isipate kuguswa guswa.

4. Funga stendi yako ya dish sehemu ulipoona panafaa.
5. Funga Dish lako kwenye stendi kwa kulielekezea Satellite uliyoikusudia ( Muelekeo wa king'amuzi husika )
6. Unganisha Coaxial cable ( Signal cable ) kwenye king'amuzi chako kwa nyuma sehemu iliyoandikwa LNB IN kisha unganisha kwenye either kwenye Dish sehemu ya LNB ama kama utakuwa na kitafuta signal (Signal  Finder ),kama utatumia Finder lazima uwe na Test cable ( Kipande cha cable ambacho utachomeka toka kwenye finder mpaka kwenye dish ( LNB ) - Nimetoa mfano wa Finder hii kwakuwa ni rahisi kupatikana na hata bei yake ni ya kawaida ila kuna finder nyengine hazihitaji Test cale.
7. Upo tayari kwa kuanza kutafuta signal. Jinsi ya kutafuta signal ntawaletea somo hilo katika post nyengine!
Tuangalie kwenye video hapo chini!



+255 789 476 655
Share:

Jun 13, 2016

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI KWENYE KING'AMUZI CHAKO


Pata msaada wa haraka na updates za Visimbuzi instagram @mustaphamadish
Hili ni moja kati ya yale ambayo ni kero kwa watumiaji wa ving'amuzi kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha na kukosa sehemu ya kupata maelezo ya kina kama hapa!
Swali la kwanza unatumia king'amuzi gani!?
Ving'amuzi vyote vyenye vifurushi ukilipa kifurushi ambacho si kile ulicholipia mwezi uliopita kama pesa pungufu hakuna picha utakayoiona na ikiwa pesa ni nyingi utaendelea kuona kifurushi kilichoisha,hivyo ili uone kifurushi ambacho umekusudia kutokana na pesa uliyolipa unapaswa kubadili kifurushi kwa kufata mtindo niliouelekeza hapa!
Chagua king'amuzi chako hapo chini ili kupata maelezo ya kina:-
  • Azam tv Bofya Hapa kujua kuhusu jinsi ya kuhama kifurushi!
  • Dstv Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
  • Startimes  Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
  • zuku Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
Kwa maelezo haya nadhani hakuna usumbufu utakaoupata tena
na  kwa maelezo zaidi no.yetu ni ile ile!
+255 789 476 655

Share:

May 15, 2016

JINSI YA KUUNGA COAXIAL CABLE ( SIGNAL CABLE )

Leo nimeonelea tuelekezane jambo hili ambalo limeshakuwa ni tatizo miongoni mwa watumiaji wengi wa ving'amuzi,lengo langu likiwa ni lile lile sote kwa pamoja tuhamie Digital huku tukiwa na ufahamu wa kutosha juu ya ulimwengu huu!
Sio jambo geni kuunga Cable ya Signal,ile Cable inayotoa Signal kutoka kwenye Dish ama Antenna kuleta kwenye king;amuzi chako na kila mtu huwa na sababu yake ya kuunga!
> Sababu zinazopelekea kuungwa kwa Coaxial Cable:-
  • Cable kuwa fupi
  • Cable kuchunika
  • Cable kukatika
Hakuna madhara katika kuunga Cable kikamilifu isipokuwa madhara yanaweza kutokea ikiwa itaungwa ndivyo sivyo,pia inashauriwa kuunga Cable si zaidi ya mara mbili!

A > Uungwaji wa kienyeji usiotakiwa ingawaje unatumiwa na wengi

 No.1

No.2

No.3

Uungwaji huu sio mzuri kiujumla kwakuwa licha ya kuwa na muonekano mbaya pia kuna uhai mdogo wa signal,mbaya zaidi inategemea umeweka wapi muungo huu,ikiwa utaweka kama ilivyo hii picha hapo chini ni dhahili umetengenezea mazingira ya kuingia maji na kupigwa jua hivyo maji yatatengeneza kutu na jua litabandua hiyo gundi hapo hivyo maisha ya Signal huishia hapo.Ingawaje hii wakati mwengine hufanywa na Wateja wenyewe lakini pia kuna mafundi hufanya hivi kusudi huku wakijua kitaaluma hii haipo ni moja kati ya kazi chafu zisizotakiwa.




B > Uungwaji mwengine wa kienyeji usiotakiwa ingawaje unaonekana una nafuu

 No.1

 No.2

 No.3

No.4

Uungwaji huu angalau kimuonekano hauleti picha mbaya na wakati mwengine ni ngumu kuonekana kama umeungwa,uungwaji huu unatofautiana kidogo na wa A huu unahitaji umakini kidogo kwakuwa ukijichanganya kidogo na kusababisha ukagusanisha nyaya hakuna mawasiliano yatakayo pita katika muunganiko huo.Uungaji wa A na B ni kawaida kupunguza signal ikiwa hujaunga vizuri.
NB: muungo A na muungo B unahitaji umakini ili nyaya zisigusane.

SIGNAL QUALITY
Unachopaswa kufanya ni hiki hapa toka kwangu:-

  • Kwanza ni lazima ununue vihusika vifuatavyo

  1. Joint
  2. F connector pic 2
Ambapo thamani yake vyote ni kuanzia 2000 mpaka 3000 ingawaje unaweza ukauziwa hata 10000 inategemea tu unanunua wapi?
  • Chuna Coaxial cable ya vizuri kwa mtindo huu kama inavyoonekana hapo chini
Hakikisha Center conductor haigusani na Outer conductor

Outer conductor unaupindia juu ya jacket kama unavyoona hii picha

Outer conductor inakuja kugusana na Connector utakayoifunga isipokuwa Center conductor haitakiwi igusane na connector
  • Jinsi JOINT inavyofungwa na kufanya kazi






NB:Uungwaji wote wa Cable hakikisha Center conductor haigusani na Outer conductor.

mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

Apr 12, 2016

UMELIPIA NA BADO HUPATI PICHA!?


Hili ni janga kubwa karibia kwa wateja wote wa ving'amuzi vya kulipia,unafanya malipo lakini hupati picha kwa wakti ama hupati picha kabisa!
Njia za kufanya ili usipate usumbufu wakati wa kufanya malipo ya mwezi:-
> Kabla ya kufanya malipo hakikisha unajua bei ya kifurushi unachotaka kulipia
> King'amuzi chako umekiwasha kabla hujafanya malipo
> Ikiwa unalipia kifurushi ambacho ni tofauti na cha awali huna budi kupiga simu ama kufata njia zilizoelekezwa ili kubadili kifurushi
> King'amuzi chako kina Signal ya kutosha

Nini ufanye ikiwa umeshalipia na hukufata njia hizo:-
> Washa king'amuzi chako
> Hakikisha kina Signal kwa kuangalia channel ambayo ipo bure ( mf:ya matangazo )
> Piga simu kwenye kampuni husika ya king'amuzi unachotumia ili ufunguliwe ama upewe maelekezo zaidi na ikitokea umekosa msaada namba hii ni msaada kwako +255789476655
mustaphamadish@gmail.com
Share:

Mar 24, 2016

NINI UFANYE KING'AMUZI CHAKO KIKIPOTEZA SIGNAL!!


Ukiona neno NO SIGNAL ama kwa kukurahisishia ukiona hupati picha kwenye King'amuzi chako na unapata ujumbe ambao hauhusiani na malipo ujue kuna tatizo la Signal lakini utathibitisha vipi kujua kama ni kweli tatizo ni Signal.
> Kila King'amuzi kina channel ya/za bure ( hapa simaanishi Local channel ) ambapo hata ikiwa malipo yako ya mwezi yamekata utaendelea kuangalia tu huwa hazikati,hivyo yakupasa uzijue Channels hizo ili unapoona umepata ujumbe huuelewi jaribu kuweka channels hizo uone zitaonyesha!? Ikiwa zitaonyesha maana yake tatizo sio signal,tatizo litakuwa ni malipo na ikiwa hazitaonyesha jibu lake tatizo ni Signal.Nimejaribu kuwajuza njia hii ya kienyeji kutokana na wengiwetu hizi lugha zilizokuja na ndege ni mtihani nami nimegundua hilo hivyo sitawaacha nitaenda nanyi sambamba!

Cha kufanya ukishajiridhisha kuwa tatizo ni Signal:-
  • Angalia Signal Cable ( waya inayotoka kwenye Dish/Antenna ) ipo sawa?
> Hakuna sehemu iliyochunika/kukatika
> Imechomekwa sawa kwenye King'amuzi chako sehemu ya lnb in/Antenna
> Imechomekwa sawa kwenye Dish/Antenna ya hicho king'amuzi
> Signal Cable ( Coaxial Cable ) Ina nyaya mbili ndani ambazo hazipaswi kugusana ( Siku nitawaeleza kazi za hizo nyaya )

Ikiwa umeona kupo sawa huna budi kuwasiliana na fundi wako ikiwa unamkumbuka ama unaweza kuwasiliana na kampuni husika ya king'amuzi ukikosa msaada piga namba hii +255789476655.

Tatizo linaweza likawa ni nini baada ya hatua za awali kuzifata?
> Yaweza kuwa Dish ama Antenna imepoteza muelekeo wake
> Yaweza kuwa kama king'amuzi cha Dish lnb kufa
> Yaweza kuwa AC ya signal kwenye king'amuzi imekufa
Zaidi ya yote ili kupata uhakika wa nini tatizo ni fundi atakapofika sehemu ya tukio!

IKIWA UMEFANYA MALIPO NA HUPATI PICHA Bofya Hapa

mustaphamadish@gmail.com
+255789476655
Share:

Mar 10, 2016

CUSTOMER CARE ZA VING'AMUZI TANZANIA


Katika vitu wanavyofail karibia makampuni yote ya ving'amuzi Tanzania ni CUSTOMER CARE ingawaje baadhi ya makampuni wameboresha lakini si kwa kukidhi mahitji ya wote..
Nilichogundua ni kwamba wateja wengi hawapendi kupokelewa na mashine,muda ambao mteja anasikiliza sauti iliyorekodiwa salio lake linaendelea kuliwa matokeo yake mteja anaweza akatumia zaidi ya 5000 na bado hapati nafasi ya kuongea na mhudumu na mara nyingi simu za makampuni za ving'amuzi huwa ni za mezani ( Landline ).
Kampuni moja tu ya king'amuzi Tanzania ambayo simu zake kama utatumia mtandao unaofanana na hizo namba inakuwa bura huliwi shilingi yako,hili ni zuri na makampuni mengine kama wangetumia utaratibu huu ingekuwa ahueni ijapokuwa tatizo la simu ni moja kati ya matatizo makuu!
Ukiachilia utafutaji wa mtoa huduma kuwa wa tabu pia unapompata huyo mtoa huduma anakuhudumia kana kwamba yeye ndiye aliyekupigia bila kujali kwamba wewe ndiye uliyepiga na huna salio la kutosha na ikitokea simu yako ikakatika pasipo kumaliza tatizo lako hata hawasumbuki kukupigia wakiamini lazima utaweka vocha na kuwapigia tu...
Kuna hili nalo mteja anayekuhudumia unamwambia tatizo lako,inaonyesha uelewa wake mdogo shortcut anaona ni kukwambia ubebe king'amuzi chako na kukipeleka katika ofisi zao,ambapo tatizo hilo linaweza likaelekezeka kwenye simu na tatizo likaisha..
Mbaya kupita zote ni hili la namba za Customer Care kutokuwa hewani muda wa kazi tena inaweza ikawa zaidi ya wiki moja hili ni tatizo!
Kwa leo ni hayo tu!

MUSTAPHA HANYA
mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

Dec 6, 2015

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI DSTV


Wateja wengi wa DStv wanakumbwa na kadhia hii,kutokujua utaratibu kwa kutaka kuhama kutoka kifurushi kimoja kwenda kingine hivyo kwa post hii utaelewa vema jinsi ya kuhama kifurushi!
Kwanza vijue vifurushi vya Dstv kwa Kubofya Hapa
Ikitokea umelipia kifurushi cha DStv Bomba  Tsh 23,500 na mwezi umeshaisha unataka kulipia kifurushi cha DStv Compact  Tsh 84,500 unaweza kufanya hivyo kwa kufata utaratibi huu:-

1 - Washa Decoder yako,kisha weka channel namba 200.
2 - Lipia Tsh 84,500 
3 - Piga nambari 0768988800 ( Atakayepokea mwambie kuwa unahitaji kubadili kifurushi toka DStv Bomba kwenda DStv Compact nae atafanya hivyo na itapokea ndani ya dk 5 tu )

Unaweza kubadili kifurushi kwa kufata utaratibu huu kwa kifurushi chochote kile na unaweza kufanya zoezi hili hata kabla kifurushi chako hakijaisha!

+255789476655
Share:

Aug 9, 2015

EPUKA USUMBUFU | ILI USIJUTE KIFURUSHI ULICHOLIPIA


KUTOKA KWANGU KUJA KWENU:
Imezoeleka hii tabia hasa kwa wateja wa DStv na Azam tv wale ambao wenzangu na mie yaani wachumi sanaa! Ambao sijajua vizuri kuwa wanajua sana thamani ya pesa zao ama ni nini!?
Ila hii nadhani uswahili pia unahusika katika hili!
WATEJA WA AZAM TV:
                         Utakuta kama hakuna mpira mtu haangaiki kulipia king'amuzi chake anangoja inapofikia either kuna mechi kubwa ama ligi inaanza ndipo anataka kulipia hii siwezi kusema si sahihi kwakuwa pengine mapenzi ya mteja ni mpira tuu na ndo maana hakuna malipo ya ziada hata kama hujalipia miezi mingapi ila wanachoanguka wengi ni kushindwa kujua wanapaswa kulipia wakati gani!?
Kama ligi ama mechi unayotaka kuangalia inaanza leo inakupasa ulipia alau siku mbili kabla ya leo ili kuondoa usumbufu kama haitakuwa imefunguka katika kufatilia ili ufunguliwe lakini wengi wenu mnachofanya kama ni mechi leo saa 8 mchana wenyewe mnalipia leo hii hii tena saa 6 mchana kwa kutegemea saa 8 mchana itakuwa imeshafunguka,matokeo yake hakuna ambacho utapata zaidi ya karaha na kujikuta unazungumza maneno yote unamaliza na kuponda huduma za azam tv kwa nguvu zote kumbe uzembe ni wako mwenyewe.
Pengine uliwahi kulipia kwa mtindo huo na ikafunguka si wakati wote itafunguka wakati mwengine system inashindwa kufanya kazi ipasavyo na muda huo simu zote zinakuwa zipo bize kutokana na idadi ya wateja wengi wanafanya ambacho wewe umefanya.
WATEJA WA DSTV:
                         Mfano wa jana tu,simu zangu zote zilikuwa bize kwakuombwa kutoa msaada wa kuwafungulia wateja wa dstv ambao wamelipia lakini hakuna wanachoona,wengine walitoa ya moyoni kuwa tayari wameshajaza wateja kwenye sehemu zao wanazoonyesha mpira lakini bado hakuna kinachoonekana matokeo yake wanalalama watapigwa watu wameshatoa pesa zao!
Hivi kama wewe ni mfanyabiashara wa kuonyesha mpira kwanini usilipie kabla ya siku ya mpira ili kuondoa usumbufu!? Hivi unajua ukiwa mbabaishaji unapoteza hao wateja wako?
Pia kama unahama kifurushi ni lazima ulipia kifurushi unachotaka then unapiga simu ili ubadilishwe hicho kifurushi unachokitaka lakini nawe unangoja siku ya mpira ndo ufanye hivyo!
ANGALIZO:
                Hakuna siku ambayo kampuni za ving'amuzi si DStv si Azam zinakuwa bize kama siku za kuanza kwa mpira,hii si kwenye simu zao hata kwenye ofisi zao na wakati mwengine hata system inaelemewa.
USHAURI WANGU KWAKO:
                                   Lipia king'amuzi chako siku mbili kabla ya mechi ama tukio unalokusudia kuangalia hii itapelekea kuondokana na usumbufu,bila kufanya hivyo utaona huduma za king'amuzi husika hazifai kumbe wewe ndiye hufai.
WhatsApp+255658046655|+255784378129

Share:

May 11, 2015

VING'AMUZI VINAVYOCHUANA | AZAM TV & DSTV | KIPI NI ZAIDI!?


Dstv ni wakongwe hii haina ubishi,ila ukongwe wa dstv haina maana kuwa hakuna king'amuzi ambacho kinaweza kuja na kufanya vizuri zaidi yake,hii inatokana na kwanza kujua mahitaji ya watazamaji kwa ujumla na kuwatimizia kile wanachokihitaji,unafuu wa bei ukizingatiwa.
Azam tv ni king'amuzi kipya kati ya vyote unavyoviona ila ndio king'amuzi kinachokimbizana na wakongwe,kwanini? kwasababu wameangalia watazamaji wanataka nini na kwa unafuu pia..Ingawaje Azam tv haijakidhi mahitaji wa wadau kwa 100% lakini alau wameweza kwa ukubwa.
Wadau wengi ni wapenzi wa mpira hivyo Azam tv wamefanikiwa kwa mpira wa Tanzania na Dstv bado anang'ang'ania ukongwe wake kwa mpira wa nje.
Ving'amuzi hivi vina mapungufu yake na kinachowakera wengi ni haya hapa:-

MAPUNGUFU YA DSTV
-Kubwa linalolalamikiwa na watanzania wengi ni bei kuwa juu,nikimaanisha malipo ya mwezi na hii inachangia na mtindo unaotumika wa kutumia $ badala ya Tsh.
Madhara ya kuwa bei juu kumefanya wadau watafute kila aina ya njia kuona wanapata uhondo wa dstv ila kwa njia isiyo rasmi,na hii inapelekea kupunguza walipaji halali wa malipo ya mwezi.
-Wana local channel,lakini malipo ya mwezi yanapokata hawaziachi zikawa bure.
Hayo ni mapungufu makubwa kwa Dstv.

MAPUNGUFU YA AZAM TV
-System wanayotumia kushindwa kutambua malipo ya mwezi wanayolipia wateja na kufunguka badala yake ukilipia kifurushi ukipendacho mpaka upige simu,hii imekuwa kero kwa wateja wengi wa azam tv,mteja anakaa mpaka wiki mbili na ikitokea hapigi simu unapita mwezi pasi kuona kile kifurushi alicholipia.
-Mawakala na wauzaji wengine wasio mawakala kuuza bei tofauti na bei sahihi.Hii sio tu mikoani ijapokuwa mikoani lawama hizi ni kubwa lakini hata hapa Dar es salaam wapo wanaouza bei juu tofauti na matangazo yalivyo.
-Picha kupotea kipindi cha mvua,king'amuzi ambacho kinaongoza kwa kupotea signal wakati wa mvua ndogo tu,hii ni kero nyengine kubwa kwa wateja wa Azam tv,kitaalamu hii inatokana na signal kuwa chini hivyo ni jukumu la Azam tv kuongeza signal badala ya 60 zifike alau 80 lakini kinachotakiwa mfikishe 100.
Hayo ni mapungufu makubwa kwa Azam tv.
TOFAUTI KUBWA KATI YA DSTV & AZAM TV
Dstv ana huduma zaidi ya moja kama:-
Extra view-Inakuwezesha kuona channel mbili tofauti kwa tv mbili tofauti kwa a/c moja.
Explora-Inakupa fulsa ya kurecodi saa 150 na mengineyo.
Umiliki na utofauti wa channel.
Dstv inaonyesha mpira wa nje na Azam tv mpira wa ndani.

MUSTAPHA MADISH | +255789476655 | mustaphamadish@gmail.com
Share:

Apr 9, 2015

BEI MPYA ZA MALIPO YA MWEZI DSTV

Ikiwa wadau wapo katika kulala na kuomba angalau gharama za malipo ya mwezi zipungua,hali imekuwa tofauti kutokana na gharama za uendeshaji ambapo imepelekea kupanda kwa bei za malipo ya mwezi kwa vifushi vyote vya Dstv kama ifuatavyo:-

BOMBA PACKAGE 
Awali ilkuwa tsh 18,500
Ikabadilika na kuwa tsh 23,500
Ikabadilika tena na kuwa tsh 19,975
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 19,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

FAMILY PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 40,000
Ikabadilika na kuwa  ths 51,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 42,900
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 39,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

COMPACT PACKAGE
 Awali ilkuwa tsh 66,000
Ikabadilika na kuwa  ths 84,500
Ikabadilika tena na kuwa tsh 82,250
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 69,000
kitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

COMPACT PLUS PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 113,000
Ikabadilika na kuwa  ths 147,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 122,500
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 109,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

PREMIUM PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 199,000
Ikabadilika na kuwa  ths 219,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 184,000
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 169,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa


HUDUMA ZA DSTV | MSAADA KIUFUNDI | +255789476655

Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita