Call / WhatsApp +255673378129

Showing posts with label Mafundi wa Ting. Show all posts
Showing posts with label Mafundi wa Ting. Show all posts

Jun 30, 2016

KUFUNGA DISH NDOGO ( KU DISH INSTALLATION )

Kwakuwa karibu Ving'amuzi vyote Tanzania vinatumia Dish ndogo leo niwape kasomo haka alau mwenye kujaribu na ajaribu atakapopata wasaa!!
Fanya haya ili uweze kufunga Dish ndogo:-

1.Dish Antenna Assembly:
- Unganisha kifaa kimoja kimoja kama karatasi ya maelekezi inavyoonyesha ili kulikamilisha dish lako bila kuacha hata kimoja kwakuwa kila kimoja kina kazi na umuhimu pia.

2.Unganisha stendi yako ya kubeba dish.





3.Angalia sehemu nzuri ya kufunga Dish ili uanze kufunga stendi yako:
- Hakikisha sehemu unayoifunga mbele hakuna miti itakayozuia kupokea signal.
- Sehemu imara itakayoweza kukaa Dish bila kucheza.
- Unashauriwa kuifunga juu ya usawa wa nyuma/jengo ili isipate kuguswa guswa.

4. Funga stendi yako ya dish sehemu ulipoona panafaa.
5. Funga Dish lako kwenye stendi kwa kulielekezea Satellite uliyoikusudia ( Muelekeo wa king'amuzi husika )
6. Unganisha Coaxial cable ( Signal cable ) kwenye king'amuzi chako kwa nyuma sehemu iliyoandikwa LNB IN kisha unganisha kwenye either kwenye Dish sehemu ya LNB ama kama utakuwa na kitafuta signal (Signal  Finder ),kama utatumia Finder lazima uwe na Test cable ( Kipande cha cable ambacho utachomeka toka kwenye finder mpaka kwenye dish ( LNB ) - Nimetoa mfano wa Finder hii kwakuwa ni rahisi kupatikana na hata bei yake ni ya kawaida ila kuna finder nyengine hazihitaji Test cale.
7. Upo tayari kwa kuanza kutafuta signal. Jinsi ya kutafuta signal ntawaletea somo hilo katika post nyengine!
Tuangalie kwenye video hapo chini!



+255 789 476 655
Share:

Nov 8, 2014

WEWE NI FUNDI MADISH | HII INAKUHUSU SANA


Hapa nazungumzia wale ambao wapo kitambo na ambao wamejiunga hivi karibuni ama hata kama unataka kuingia ukanda huu kwa mikono miwili nakukaribisha na hii post inakuhusu sana zaidi ya yote ukiyachukua yangu na kuyafanyia kazi majibu utanirejeshea!
Ufungaji wa Dish ya Azam tv..
Hivi karibuni nilikuwa pale Tandika Flat,katika ile huduma piga simu tunakufata ulipo..
Ilihitajika Azam tv nasi tukatekeleza,tulipofika kazi ikaanza kwa kuangalia pa kufungia Dish kwanza haikuwa tabu kwakuwa tayari dish nyengine tena zikiwemo Azam tv zimeshafungwa, na ndipo nikapata hii post..






Hii ni kazi ya Fundi ambaye anapewa dhamana kama ambavyo napewa mimi na wateja ila matokeo yake kinachofanyika ni kulipua kama hivi ili tu picha ipatikane ndani biashara imeisha!
Nikaona nifunge hapo hapo ili hata kama naye ni mpitiaji humu aone alichofanya alau nafsi itamsuta na kuona alivyoitendea taaluma ndivyo sivyo na mteja wake pia huku wengine mkijifunza msije kuwa kama mafundi hawa!

Ona kazi ya Mustapha MaDish...


 Tofauti hata kwa macho inaonekana!

 Ugumu upo wapi kufanya hivi..

 Angalia na uyafanyie kazi..

 Tofauti ya kazi zangu na wengine..

 Sababu ya kuitwa Mustapha MaDish..


 Setting zikiendelea..





Baada ya kudrill..

Nikiwa nimeachana na hiyo issue ya Azam tv,nikakumbuka kituko kingine nilikutana nacho Kimara,nikiwa katika huduma yangu ile ile ya PIGA SIMU TUKUFATE ULIPO..
Safari hii sio Azam tv tena...
Ufungaji wa Dish ya DStv...
Kwakweli hii ni kituko,hivi nawe mteja kabisa unakubali kazi ya fundi wako hivi!!??








Ambacho kilichofanya mpaka nianze kumshangaa mteja kwakuwa ndipo mlango wake ulipo maana yake ili aingia nyumbani kwake lazima apitie lilipo hilo dish,jibu lake ameridhika ama!?
Kiukweli kama ningemkuta wala nisingevumilia ningeongea nae mawili matatu kuhusu hilo dish...

Ona kazi ya Mustapha MaDish..






Ustadh nae...

Wale mafundi nonihino wado waliendelea kunishangaza...
Ufungaji wa Dish ya Zuku...
Palee Flat za Ubungo ndipo nilipokutana na ufundi huu..
ukipiga upepo kweli jamani hii Dish haiondoki kweli!!??
Bahati mbaya ama bahati nzuri ukifanyakazi katika hizi flat mara nyingi unapewa mwenyeji wa kuwa nae unapokuwa juu,swali je mwenyeji wa huyu fundi aliifurahia hii kazi!!??

KAZI SAFI | MAFUNDI WAZOEFU | DISH AINA ZOTE | PIGA 0789476655
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita