Call / WhatsApp +255673378129

Showing posts with label easy tv. Show all posts
Showing posts with label easy tv. Show all posts

Mar 10, 2016

CUSTOMER CARE ZA VING'AMUZI TANZANIA


Katika vitu wanavyofail karibia makampuni yote ya ving'amuzi Tanzania ni CUSTOMER CARE ingawaje baadhi ya makampuni wameboresha lakini si kwa kukidhi mahitji ya wote..
Nilichogundua ni kwamba wateja wengi hawapendi kupokelewa na mashine,muda ambao mteja anasikiliza sauti iliyorekodiwa salio lake linaendelea kuliwa matokeo yake mteja anaweza akatumia zaidi ya 5000 na bado hapati nafasi ya kuongea na mhudumu na mara nyingi simu za makampuni za ving'amuzi huwa ni za mezani ( Landline ).
Kampuni moja tu ya king'amuzi Tanzania ambayo simu zake kama utatumia mtandao unaofanana na hizo namba inakuwa bura huliwi shilingi yako,hili ni zuri na makampuni mengine kama wangetumia utaratibu huu ingekuwa ahueni ijapokuwa tatizo la simu ni moja kati ya matatizo makuu!
Ukiachilia utafutaji wa mtoa huduma kuwa wa tabu pia unapompata huyo mtoa huduma anakuhudumia kana kwamba yeye ndiye aliyekupigia bila kujali kwamba wewe ndiye uliyepiga na huna salio la kutosha na ikitokea simu yako ikakatika pasipo kumaliza tatizo lako hata hawasumbuki kukupigia wakiamini lazima utaweka vocha na kuwapigia tu...
Kuna hili nalo mteja anayekuhudumia unamwambia tatizo lako,inaonyesha uelewa wake mdogo shortcut anaona ni kukwambia ubebe king'amuzi chako na kukipeleka katika ofisi zao,ambapo tatizo hilo linaweza likaelekezeka kwenye simu na tatizo likaisha..
Mbaya kupita zote ni hili la namba za Customer Care kutokuwa hewani muda wa kazi tena inaweza ikawa zaidi ya wiki moja hili ni tatizo!
Kwa leo ni hayo tu!

MUSTAPHA HANYA
mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

Oct 16, 2014

UWEZO BINAFSI

Ijapokuwa imepita miezi ipatayo 10 ila hili ni moja kati ya niyakumbukayo na ya kujivunia pia na sababu napokea simu mpaka wakati mwengine naona imepitiliza ila kwakuwa ndo kazi yangu sinabudi kumaliza shida za wadau wangu...
Nakumbuka ni maeneo ya sinza pale kumekucha kwa mzee moja hivii wa kihindi nilifunga Azam tv,kama ilivyoada kulipua kwangu ni mwiko nikafanya yangu na kanuni zangu kisha nikakabidhi kazi kwa mteja wangu!
Mteja cha kwanza kuniambia "nimependa kazi yako,umechukua muda mfupi na kazi safi" kwa kulithibitisha hilo wakamtoka wekundu wekundu pale nje ya malipo ya king'amuzi,hii alitoa kama pongezi yake kwang,nami kwakuwa nimetumwa helaa aaah nikashukuru pale wekundu wangu mfukoni kisha nikachapa mwendo!
ilipita kama wiki mbili alipata tatizo la king'amuzi maana kulikuwa na fundi akaleta ufundi nyumbani kwake hivyo alitaka msaada wa fundi,ilimlazimu afike ofisini na kwa bahati mbaya sikuwepo..fundi aliyepo akachukua nafasi yake akaenda na mteja kuangalia tatizo...
Tatizo alilimaliza na mteja akaendelea pata burudani kama kawaida...
Ikapita kama siku kadhaa tu mbele akaja tena ofisini kwa kununua king'amuzi kingine ila kwasasa alitaka zuku lakini safari hii pia hakunikuta,alidai aondoke na vifaa vyake ila kufungiwa anataka afungiwe na Mustapha,nilijaribu kupigiwa simu nami nilisema ukweli ni kama baada ya siku nne ndipo nitakuwa na muda,kitu ambacho kila mmoja pale ofisini alishangaa kuona mteja anakubali kuningoja..
Haikuchukua siku nne bali yule mteja alingoja kama wiki na siku tatu ndipo nikapata muda wa kwenda kumfungia Zuku yake..
Na hapo ndipo nikapata malalamiko ya fundi aliyeenda kufanya repair baada ya kupita mimi..
Hakukuwa na maelewano mazuri,lugha ya biashara haikutumika hapa ila nilichofanya ni kumtaka radhi kisha nikampa burudani kama ilivyo ada!
Matokeo yake hataki fundi yeyote zaidi Mustapha.
Hapa tunazungumzia uwezo binafsi si kama najua saana,ijapokuwa najua vilivyo vingi ukanda wangu na hata aliyefanya hivyo ni mwanafunzi wangu kati ya wanafunzi wangu wengi tu ila alishindwa ama wanashindwa kufata ile misingi husika..
Mafanikio huja kwa kupenda unachofanya!
Ukipenda unachofanya,utakifanya kwa uwezo wako wote na hii lazima ufanikiwe..
Upo facebook Bofya hapa like page yangu kupata mapya ya ving'amuzi vyote Tanzania
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita