Call / WhatsApp +255673378129

Showing posts with label startimes. Show all posts
Showing posts with label startimes. Show all posts

Nov 27, 2017

ZIJUE OFFER ZA VING'AMUZI 2017 KUELEKEA 2018

Tunaelekea katika kumaliza mwaka 2017 na tunategemea kuingia mwaka 2018, yapo mengi ambayo kupitia blog hii umefaidika kwa hali yeyote ile kama ndivyo tunashukuru kwakuwa ndio lengo letu, lakini pia nadhani yapo yaliyokukera kupitia blog hii kama ndivyo tunasikitika na kukuomba radhi pia maana sio lengo letu na ukizingatia hata kama itatokea unafanya jambo zuri vipi sio wote watakaopendezwa nalo kwa kuzingatia wapo ambao lengo lao ni kuharibu tu ama kutengeneza njia ya kufanya vibaya.. Zaidi ya yote shukrani kwa wale wote walio pamoja nasi kwa mwaka mzima na hata hapo miaka ya nyuma maana bila ninyi wala mimi na team yangu tusingefika hapa na isingezaliwa MADISH TECHNOLOGY.
Leo nawaletea orodha ya ving'amuzi vyenye offer katika msimu huu wa kumaliza mwaka 2017:-
 Bofya king'amuzi ambacho unataka kujua offer yake na utapata maelezo ya kina kuhusu offer hizo!
+255789476655 
Whatsapp+255784378129
Insta @mustaphamadish 
Share:

Aug 26, 2017

KWANINI USILIPIE MAPEMA | KING'AMUZI CHAKO!?


Nimejaribu kufatilia kwa ukaribu sana utaratibu wa kufanya malipo ya king'amuzi kati ya watumiaji wageni nikimaanisha wenzetu rangi nyeupe na sisi ngozi nyeusi ijapokuwa si wote isipokuwa wengi wetu tuna utaratibu mmbovu sana wa kufanya malipo ya ving'amuzi tunavyotumia...!!
Mfano ukute mzungu/ama muhindi utaratibu wake wa kulipia, mfano amelipia king'amuzi anachotumia tarehe 10 mwezi wa 11, atalipia tena siku mbili ama tatu nyuma kwa mwezi unaofata, anaweza akalipia terehe 7 ama 8 ama 9 mwezi wa 12 ambapo hukuti anapata usumbufu kuhusu malipo na uzuri zaidi ving'amuzi karibu vyote vina utaratibu wa kukutumia ujumbe tena kwenye king'amuzi chako ya kwamba kifurushi chako karibu kinaisha hivyo ufanye malipo mapema!
Wengi wetu sie kina ngozi nyeusi kama nimelipia tarehe 10 mwezi wa 11, sitafanya malipo mpaka kifurushi kitakapokata kabisa matokeo yake unatokea usumbufu wa hali ya juu.. wakati mwengine inaweza ikawa kipato hilo ni sawa siwezi lipinga ila hupaswi kungoja mpaka siku ya mpira ndipo ufanye malipo kwa maana mara zote siku za mipira sio Azam sio DStv huwa system zao zina elemewa na matokeo yake unapata maudhi usiyoyategema ambapo ungelipia siku moja ama mbili kabla ya mpira unaotaka kuangalia usingepata usumbufu hata kidogo!
Tujitahidi kubadilika wadau wa ulimwengu huu wa Digital tv... Kwa hili naomba niwe mkweli  ikiwa utalipia siku ya mpira na ukatafuta msaada umekosa hata mimi na managment yangu hatutakuwa na msaada ila kama utalipia siku 2 ama 1 kabla ya mpira msaada utaupata toka kwetu kwa king'amuzi chochote kile.
Kwa maelezo zaidi.....
 +255789476655 
Whatsapp+255784378129
Share:

Dec 26, 2016

TUNAAGA 2016 | KWA KUJITUMA ZAIDI


Mafanikio hayana njia ya mkato,ukipata kauli za wengi wa liofanikiwa watakwambia njia walipitia na kamwe hakuna njia ya mkato.. nimejifunza kutokutamani mafanikio ya mtu bila kuwa tayari kupitia hatua za kufikia mafaniko..
Mafanikio yanahitaji:-
  • Kupenda unachofanya
  • Kukijua ama jifunze zaidi ili ukijue
  • Kuheshimu na kukitetea unachofanya
  • Kujitoa
  • Kujituma
  • Juhudi binafsi
  • Kujiongeza ( kuwa mbunifu )
  • Kuwa na heshima na Pesa
  • Kutokuwa mnyimi  ama mbinafsi 
  • Na mengineyo...
Nipo kwenye ukanda huu yapata mwaka wa nane sasa nina uzoefu wa kutosha kuhusu makampuni yote ya ving'amuzi Tanzania na watumiaji wake pia ile kiundani zaidi..
Najua nimesaidia wengi ndani na nje ya Tanzania,nimetengeneza BASE kubwa mno mpaka binafsi kama siamini hivii ila hii yote kutokana na Kupenda nilichamua kufanya n nashukuru Alhamdullah!
Mwaka unaishi na tunategemea kuingia mwaka mpya 2017
mimi na team yangu ile mikono salama #FundiMakini tunakuletea kitu kizuri sana kwenye ulimwengu wa Digital Tv... Kubwa tunashukuru kwa uwepo wenu na kutupa moyo zaidi ya yote tunawaahidi kuwaletea vitu vizuri zaidi ili kila mmoja wenu ahufurahie ulimwengu wa Digita Tv!
+255 789476655
Share:

Oct 1, 2016

MSIMU WA OFFER 2016 | VING'AMUZI TANZANIA

 

Tunaelekea kumaliza mwaka 2016 na kutokana na ushindani uliopo katika ukanda wa Digital tv,makampuni ya Ving'amuzi yanajitahidi kutafuta namna ya kushawishi wateja wapya na kujiunga na ving'amuzi vyao huku wakiwafanya wateja walionao kutowapoteza kwa kuboresha huduma zao na kutoa OFFER!!
Vijue Ving'amuzi vilivyo na OFFER na Offer zao kwasasa:-
  1. Azam Tv
  2. DStv
  3. StarTimes
  4. Zuku Tv
Kwa msaada kiufundi na maelezo zaidi kuhusu King'amuzi chako piga:-
+255789476655 Kuanzia saa 08:30 - 18:00 Kila siku.
Share:

Jun 13, 2016

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI KWENYE KING'AMUZI CHAKO


Pata msaada wa haraka na updates za Visimbuzi instagram @mustaphamadish
Hili ni moja kati ya yale ambayo ni kero kwa watumiaji wa ving'amuzi kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha na kukosa sehemu ya kupata maelezo ya kina kama hapa!
Swali la kwanza unatumia king'amuzi gani!?
Ving'amuzi vyote vyenye vifurushi ukilipa kifurushi ambacho si kile ulicholipia mwezi uliopita kama pesa pungufu hakuna picha utakayoiona na ikiwa pesa ni nyingi utaendelea kuona kifurushi kilichoisha,hivyo ili uone kifurushi ambacho umekusudia kutokana na pesa uliyolipa unapaswa kubadili kifurushi kwa kufata mtindo niliouelekeza hapa!
Chagua king'amuzi chako hapo chini ili kupata maelezo ya kina:-
  • Azam tv Bofya Hapa kujua kuhusu jinsi ya kuhama kifurushi!
  • Dstv Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
  • Startimes  Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
  • zuku Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
Kwa maelezo haya nadhani hakuna usumbufu utakaoupata tena
na  kwa maelezo zaidi no.yetu ni ile ile!
+255 789 476 655

Share:

May 15, 2016

JINSI YA KUUNGA COAXIAL CABLE ( SIGNAL CABLE )

Leo nimeonelea tuelekezane jambo hili ambalo limeshakuwa ni tatizo miongoni mwa watumiaji wengi wa ving'amuzi,lengo langu likiwa ni lile lile sote kwa pamoja tuhamie Digital huku tukiwa na ufahamu wa kutosha juu ya ulimwengu huu!
Sio jambo geni kuunga Cable ya Signal,ile Cable inayotoa Signal kutoka kwenye Dish ama Antenna kuleta kwenye king;amuzi chako na kila mtu huwa na sababu yake ya kuunga!
> Sababu zinazopelekea kuungwa kwa Coaxial Cable:-
  • Cable kuwa fupi
  • Cable kuchunika
  • Cable kukatika
Hakuna madhara katika kuunga Cable kikamilifu isipokuwa madhara yanaweza kutokea ikiwa itaungwa ndivyo sivyo,pia inashauriwa kuunga Cable si zaidi ya mara mbili!

A > Uungwaji wa kienyeji usiotakiwa ingawaje unatumiwa na wengi

 No.1

No.2

No.3

Uungwaji huu sio mzuri kiujumla kwakuwa licha ya kuwa na muonekano mbaya pia kuna uhai mdogo wa signal,mbaya zaidi inategemea umeweka wapi muungo huu,ikiwa utaweka kama ilivyo hii picha hapo chini ni dhahili umetengenezea mazingira ya kuingia maji na kupigwa jua hivyo maji yatatengeneza kutu na jua litabandua hiyo gundi hapo hivyo maisha ya Signal huishia hapo.Ingawaje hii wakati mwengine hufanywa na Wateja wenyewe lakini pia kuna mafundi hufanya hivi kusudi huku wakijua kitaaluma hii haipo ni moja kati ya kazi chafu zisizotakiwa.




B > Uungwaji mwengine wa kienyeji usiotakiwa ingawaje unaonekana una nafuu

 No.1

 No.2

 No.3

No.4

Uungwaji huu angalau kimuonekano hauleti picha mbaya na wakati mwengine ni ngumu kuonekana kama umeungwa,uungwaji huu unatofautiana kidogo na wa A huu unahitaji umakini kidogo kwakuwa ukijichanganya kidogo na kusababisha ukagusanisha nyaya hakuna mawasiliano yatakayo pita katika muunganiko huo.Uungaji wa A na B ni kawaida kupunguza signal ikiwa hujaunga vizuri.
NB: muungo A na muungo B unahitaji umakini ili nyaya zisigusane.

SIGNAL QUALITY
Unachopaswa kufanya ni hiki hapa toka kwangu:-

  • Kwanza ni lazima ununue vihusika vifuatavyo

  1. Joint
  2. F connector pic 2
Ambapo thamani yake vyote ni kuanzia 2000 mpaka 3000 ingawaje unaweza ukauziwa hata 10000 inategemea tu unanunua wapi?
  • Chuna Coaxial cable ya vizuri kwa mtindo huu kama inavyoonekana hapo chini
Hakikisha Center conductor haigusani na Outer conductor

Outer conductor unaupindia juu ya jacket kama unavyoona hii picha

Outer conductor inakuja kugusana na Connector utakayoifunga isipokuwa Center conductor haitakiwi igusane na connector
  • Jinsi JOINT inavyofungwa na kufanya kazi






NB:Uungwaji wote wa Cable hakikisha Center conductor haigusani na Outer conductor.

mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

Apr 12, 2016

UMELIPIA NA BADO HUPATI PICHA!?


Hili ni janga kubwa karibia kwa wateja wote wa ving'amuzi vya kulipia,unafanya malipo lakini hupati picha kwa wakti ama hupati picha kabisa!
Njia za kufanya ili usipate usumbufu wakati wa kufanya malipo ya mwezi:-
> Kabla ya kufanya malipo hakikisha unajua bei ya kifurushi unachotaka kulipia
> King'amuzi chako umekiwasha kabla hujafanya malipo
> Ikiwa unalipia kifurushi ambacho ni tofauti na cha awali huna budi kupiga simu ama kufata njia zilizoelekezwa ili kubadili kifurushi
> King'amuzi chako kina Signal ya kutosha

Nini ufanye ikiwa umeshalipia na hukufata njia hizo:-
> Washa king'amuzi chako
> Hakikisha kina Signal kwa kuangalia channel ambayo ipo bure ( mf:ya matangazo )
> Piga simu kwenye kampuni husika ya king'amuzi unachotumia ili ufunguliwe ama upewe maelekezo zaidi na ikitokea umekosa msaada namba hii ni msaada kwako +255789476655
mustaphamadish@gmail.com
Share:

Mar 10, 2016

CUSTOMER CARE ZA VING'AMUZI TANZANIA


Katika vitu wanavyofail karibia makampuni yote ya ving'amuzi Tanzania ni CUSTOMER CARE ingawaje baadhi ya makampuni wameboresha lakini si kwa kukidhi mahitji ya wote..
Nilichogundua ni kwamba wateja wengi hawapendi kupokelewa na mashine,muda ambao mteja anasikiliza sauti iliyorekodiwa salio lake linaendelea kuliwa matokeo yake mteja anaweza akatumia zaidi ya 5000 na bado hapati nafasi ya kuongea na mhudumu na mara nyingi simu za makampuni za ving'amuzi huwa ni za mezani ( Landline ).
Kampuni moja tu ya king'amuzi Tanzania ambayo simu zake kama utatumia mtandao unaofanana na hizo namba inakuwa bura huliwi shilingi yako,hili ni zuri na makampuni mengine kama wangetumia utaratibu huu ingekuwa ahueni ijapokuwa tatizo la simu ni moja kati ya matatizo makuu!
Ukiachilia utafutaji wa mtoa huduma kuwa wa tabu pia unapompata huyo mtoa huduma anakuhudumia kana kwamba yeye ndiye aliyekupigia bila kujali kwamba wewe ndiye uliyepiga na huna salio la kutosha na ikitokea simu yako ikakatika pasipo kumaliza tatizo lako hata hawasumbuki kukupigia wakiamini lazima utaweka vocha na kuwapigia tu...
Kuna hili nalo mteja anayekuhudumia unamwambia tatizo lako,inaonyesha uelewa wake mdogo shortcut anaona ni kukwambia ubebe king'amuzi chako na kukipeleka katika ofisi zao,ambapo tatizo hilo linaweza likaelekezeka kwenye simu na tatizo likaisha..
Mbaya kupita zote ni hili la namba za Customer Care kutokuwa hewani muda wa kazi tena inaweza ikawa zaidi ya wiki moja hili ni tatizo!
Kwa leo ni hayo tu!

MUSTAPHA HANYA
mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

Nov 1, 2014

HDMI CABLE


Imenipelekea kuandika post hii kutokana na simu niliyoipokea hivi karibuni kutoka Dodoma,lakini kabla ya simu hiyo kuwaelewesha wadau wangu kuhusu HDMI CABLE ni kawaida tu ila kwenye hii blog yetu leo wacha nitoe kile kidogo nilichonacho kwa wadau wangu!
Unapozungumzi HD
lazima ushirikishe cable inayoitwa HDMI CABLE,kwasababu ili uone picha katika mfumo wa HD ( Ubora wa picha wa hali ya juu ) ni lazima utumie HDMI CABLE,cable ambayo inatoa picha kutoka kwenye inaweza kuwa DVD/Receiver/King'amuzi ama chochote chenye uwezo wa kutoa HD na kupeleka kwenye tv ambayo nayo ikiwa ina uwezo wa kupokea HD.



Hii cable inachomekwa kwenye tundu lililoandikwa HDMI.
Ili kujua kama tv/DVD ama king'amuzi chako ni HD unapaswa kuangalia kwa umakini je kuna tundu lililoandikwa HDMI,kama lipo hilo jua kifaa chako hicho ni HD.
Je unavijua ving'amuzi vilivyo kwenye mfumo wa HD hapa Tanzania..??

  Una swali  piga +255789476655
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita