Call / WhatsApp +255673378129

Jan 1, 2018

JE KOPO LINASAIDIA KIPINDI CHA MVUA!?

"Kwenye Kisimbuzi ( King'amuzi ) kinachotumia Dish kufunika lnb kwa KOPO hakusaidii chochote katika kufanya Kisimbuzi chako kisisumbue wakati wa MVUA..."
Tukirejea nyuma kidogo hata waliotengeneza SET ya dish waliangalia kama maisha ya dish ni ya kukutana na mvua na jua,hivyo wakatengeneza katika kuhimili hali zote mbili bila kushauri ama kuengeneza makopo ili yaweze kufunika lnb..
Binafsi lawama zangu kwa mafundi, kwa kuacha kutumia plastic cover ya lnb ambayo inasaidia kufunika coaxial cable inapofungwa kwenye lnb ili maji yasiweze kuingia kwenye lnb/cable na kusababisha short n.k. 

Kupata ushauri na mambo yote yanayohusu Visimbuzi tukutane Insta
@mustaphamadish Kupata MAFUNDI WA KUFUNGA VISIMBUZI/MADISH aina zote kwenye GUEST, LODGE, HOTEL, APARTMENT, OFFICE na MAJUMBANI kwa usafi na ubunifu wa hali ya juu, wasiliana nasi!
BAADHI YA SEHEMU TULIZOFUNGA NI:-

  • KING D HOTEL
  • TRANSIT MOTEL
  • JB BELMONT HOTEL
  • BONDENI HOTEL
  • TUCTA HQ
  • PSPF HQ
  • IKULU - OFFICE YA WAZIRI MKUU
  • JAMII FORUM OFFICE - Ilipokuwa sinza
  • CRDB BANK - mlimani city, Lumumba, Mikocheni n.k
  • DTB BANK - HQ n Magomeni branch
Uzoefu wa kazi ni zaidi ya miaka 10, tukisimamia kazi safi, 
bei nafuu na ubora ni zaidi ya wengine.
 
MAWASILIANO:-
Call/ Text 0789476655
Whatsapp +255784378129
Instagram @mustaphamadish
Share:

Dec 31, 2017

LNB NI NINI...??

Kwenye Technology kuna vifaa ambavyo kuvitafutia lugha ya kiswahili moja kwa moja hakuna ila nitakachojitahidi kufanya ni kukupa urahisi ili uelewe pasi kutoka nje ya maana yenyewe.



LNB ni nini?
LNB ama kwa kirefu chake ni Low Noise Block downconverter, ni kidubwana,kifaa kidogo kinachokaa kwenye dish ambacho kinapokea signal toka kwenye satellite na kupeleka kwenye satellite receiver ( King'amuzi kinachotumia dish ). Pia huitwa low-noise converter (LNC), au low-noise downconverter (LND), hiki kifaa wakati mwengine kinaitwa low-noise amplifier (LNA).

LNB ni mchanganyiko wa low-noise amplifier, frequency mixer, local oscillator na intermediate frequency (IF) amplifier. Inapokea microwave signal kutoka kwenye satellite iliyokusanywa na Dish, inaimarisha, na inachagua mzunguko wa mzunguko kwenye upeo wa chini wa mzunguko wa kati (IF). Hii downconversion inaruhusu signal kuletwa ndani kwenye Satellite receiver kwa kutumia Coaxial cable. ikiwa Signal ilibaki katika asili yake microwave frequency ingehitaji gharama kubwa na impractical waveguide line.

LNB kwa kawaida ni kisanduku kidogo kinachofungwa mbele ya uso wa dish kwa kutumia mfano wa fimbo ( kibomba/ vibomba ). Microwave signal kutoka kwenye dish inachukuliwa na  feedhorn kwenye LNB na hutolewa kwa sehemu ya waveguide.

LNB hufanyakazi kwa kutumia umeme ambao utatokea kwenye Satellite receiver kwa kutumia coaxial cable na huchomekwa sehemu iliyoandikwa LNB IN ikiwa imetumika pin katika kufanya coaxial cable kufunga kwenye Receiver na kwenye LNB pia.

AINA ZA LNB
  • Ku band 
  • Ka band
  • C band
Post hii itaendelea...
+255789476655
Whatsapp +255784378129

Share:

Dec 21, 2017

KUTUMIA KING'AMUZI KIMOJA KWA TV ZAIDI YA 1


Ving'amuzi vyote unavyovijua wewe iwe vya bure ama vya kulipia, nikiwa na maana vyenye kulipia malipo ya mwezi na visivyo na malipo ya mwezi, unaweza kutumia king'amuzi kimoja kwa tv zaidi ya moja, kwa kutumia king'amuzi kimoja unaweza kugawa picha kwa tv hata zikiwa 100.
Hii inawezekanaje!? kwanza unapaswa kujua ni king'amuzi gani ambacho unataka kugawa picha kwa tv zaidi ya moja,  chagua kwenye orodha hapo chini:-
NB:Nitaweka link kwa kila king'amuzi ambayo itakupeleka mpaka kwenye post ambayo itakuwa na maelezo yote kwa kina.
Kwa Maelezo zaidi hii hapa +255789476655
Whatsapp+255784378129
Share:

Dec 15, 2017

TELEVISION AU RUNINGA NI NINI!?

 Tv ya kijerumani ya mwaka 1956

Neno "televisheni" linatokana na maneno mawili: tele (kutoka Kigiriki: kwa mbali sana) na visio (kutoka Kilatini: mwono; kwa pamoja yanaunda neno la Kiingereza television lililotoholewa katika Kiswahili televisheni.
Televisheni - TV au runinga ni chombo (kifaa) chenye kiwambo au kioo ambacho kinapokea mawasiliano kutoka kituo cha televisheni na kuyabadilisha kuwa picha na sauti.
Kwa kawaida TV inaonekana kama sanduku. TV za zamani kabisa zilikuwa zina kirimba au fremu kubwa ya mbao na zilikuwa zikiwekwa chini kama fanicha. TV za kisasa ziko za namna nyingi kama zilivyo nyingi zaidi. Kuna baadhi ya TV zinaweza kuenea mkononi mwako zikawa zinaendeshwa kwa kutumia betri. TV nyingine zinaweza kuenea ukuta mzima wa nyumba, na inaweza kukaa katika sakafu, au kuna nyingine ambazo zimenyooka (flat) na zinaweza kubandikwa ukutani.
Televisheni inaweza kuonyesha picha kutoka sehemu mbalimbali. Cha kwanza unachotakiwa kufanya ni kutumia kidaka mawasiliano au antena (au aerial), hii itaonyesha yale yote yanayorushwa na kituo cha matangazo ya televisheni.
Vituo vya TV vinaweza kuwa mbali kabisa lakini bado matangazo yake yanapatikana kama antena ya kurusha mawimbi yake iko katika umbali wa kilomita 50 hadi 150. Teknolojia mpya zaidi ni kutumia vyombo vya angani kama antena ya kurusha mawimbi haya duniani. TV pia inaweza kuonyesha filamu kutoka katika VCD na DVD au VCR yaani tepu za kawaida. Cable TV na Satellite TV zinaweza zikatoa huduma nyingi za vipindi vya TV kwa mara moja na vilevile kuvirusha hewani. Michezo mingi ya video huunganishwa katika TV ili uweze kuona kile unachokicheza. Kuna baadhi ya tarakilishi au kompyuta ambazo unaweza kutumia TV kama kioo cha kufanyia kazi zako (kiwambo, au kwa jina lingine monita).
Baada ya Vita Kuu ya II, mfumo bora wa utangazaji wa televisheni Black n White ulikuwa maarufu nchini Marekani na Uingereza, na seti za televisheni zilikuwa za kawaida katika nyumba, biashara na taasisi.Katika miaka ya 1950, televisheni ilikuwa katikati ya msingi kwa kushawishi maoni ya umma.  Katikati ya miaka ya 1960, utangazaji wa rangi uliletwa nchini Marekani na nchi nyingi zilizoendelea.. Kawaida ya viwambo vingi (kioo au vioo) huonyesha kuwa vina kona ya mzunguko, lakini kwa sasa vioo vingi hutengenzwa kwa kunyooka na zina ncha pembeni.
Kabla ya miaka ya 1990, TV zote zilikuwa zikitengenezwa kwa umbo moja - zilikuwa kubwa kidogo na kisha zilikuwa ndefu. Kwa mfano, kama kioo kilikuwa cha urefu wa inchi 3, basi lazima kitakuwa na upana wa inchi 4. Au kama kioo kina urefu wa cm 30, lazima kitakuwa kina upana wa cm 40.
Umbo la TV za kisasa linazidi kuwa maarufu na kupata wapenzi wengi zaidi kila siku ziendapo. TV zenye kioo cha upana mkubwa wa mstatili huonekana vizuri katika runinga kubwa (theatre screen) na pia inapendeza wengi zaidi. Hizi huziita kioo kipana (widescreen). Endapo TV ya kioo kipana ina urefu wa cm 30, basi lazima itakuwa ina upana wa cm 53. Ili ifanye kazi vizuri, uonyeshaji wa TV pia unatakiwa ujengwe kwa namna ya upana yaani 'widescreen'. Kioo kipana kinaweza kubadilishika kwa ukubwa wowote unaoutaka, lakini suala la umbo linabaki kuwa vilevile kama lilivyo (widescreen).
Tangu mwaka 2010, kwa uvumbuzi wa smart television, internet television imeongeza upatikanaji wa programu za televisheni na sinema kupitia mtandao kupitia huduma za video za Streaming kama vile Netflix, Amazon Video, iPlayer, Hulu, Roku na Chromecast.
Aina za tv

Siku za usoni nitakuja kuzungumzia kwa kina kuhusu yaliyo hapa chini:
Broadcast Systems 
  • Terrestrial Television
  • Cable Television
  • Satellite Television
  • Internet Television
Display Technologies
  • Disk
  • CRT
  • DLP
  • Plasma
  • LCD
  • OLED
  • LDTV
  • SDTV
  • HDTV
  • UHDTV
 Imeandikwa na Mustapha Hanya
Whatsapp+255784378129
Share:

Dec 14, 2017

UTAJUAJE KAMA TV YAKO INA KING'AMUZI NDANI?


Swali la wengi kwasasa ni hili kutokana na ukweli kwamba uondoshwaji wa local channels kwa baadhi ya Visimbuzi imekuwa kama janga hivi.. Sasa niwape namna ya kujua jinsi gani ya kupata local channels kupitia tv ikiwa ina kisimbuzi ndani, inaweza ukatumia Antenna ama Dish inategemea na uwezo wa tv:-
Utajuaje kama tv yako ina kisimbuzi ndani?
  • Ingia kwenye INPUTs inategemea na brand, zipo ambazo zinatumia SOURCE, INPUT n.k unabonyeza na itakuletea orodha ya input zote mfano:-
AV
HDMI1
VGA
USB
ATV
DTV
Ukiona ina DTV ujue ina kisimbuzi.
  • Njia nyengine unachukua remote yako unabonyesha kwenye SETTING unaenda kwenye SEARCH hii nayo inategemea na tv, tv nyengine hutumia tune n.k hapa unaweza ukaweka AUTO SEARCH itakuletea Analogue tv na Digital tv ikikuletea hizo chaguo ujue tv yako ina kisimbuzi ila kama itakuletea Analogue tv pekee ujue haina kisimuzi..
 Ikiwa tv yako ina DTV maana yake inapokea matangazo ya Digital hivyo unapaswa kutafuta Antenna na kuchomeka muelekea wa Startimes/Ting ama Continental na kufanya search kama kila kitu kikiwa sawa channels zitaingia..
Kuna DVB T1/ T2 hii ni kwa ajili ya antenna.
Kuna DVB S1/ S2 hii kwa ajili ya dish.

Insta @mustaphamadish
Whatsapp+255784378129

Share:

Dec 13, 2017

UNALIPIA LAKINI INAKATA KABLA MWEZI KUISHA


Hii inaweza kutokea kwenye ving'amuzi vyote na hutokea makosa ya mtandao ama kama kifurushi ulichopo sio sahihi hivyo hakiwezi kufika mwezi kwa baadhi ya ving'amuzi! Mara chache mno hutokea kwa ving'amuzi kama cha Azam tv,DStv,Zuku, n.k. na huwa mara zote ni kufail kwa system tu na unachopaswa kufanya ni kutoa taarifa ili uweze kusaidiwa kwa kurudishiwa huduma. Tatizo hili limekuwa kubwa sana kwa upande waking'amuzi cha Startimes na huwa tofauti na ving'amuzi vyengine ili kujua zaidi Bofya hapa
Whatsapp+255784378129

Follow Insta @mustaphamadish
Share:

Dec 2, 2017

KING'AMUZI KISICHO NA MALIPO YA MWEZI


Awali tulikuwa na ving'amuzi viwili ambavyo havikuwa na malipo ya mwezi, kulikuwa na Digitek na Continental, baadae Continental wakaanza mfumo wa kulipia na kuwa na Vifurushi pia kutaka kujua zaidi kuhusu Continental decoder bofya hapa, tukabaki na Digitek ambapo ni king'amuzi pekee ambacho hakina malipo ya mwezi. Kwa kutokuwa na malipo ya mwezi kwenye king'amuzi cha Digitek kumefanya kwenye zile Tv ambazo zinauwezo wa kupokea matangazo ya Digital pasi kutumia king'amuzi kuwezesha kupata channels za Tanzania bila malipo yeyote na bila kutumia king'amuzi cha nje kwakuwa ndani ya tv kwa lugha nyepesi tunasema ina king'amuzi.

Kwa maelezo zaidi +255789476655
Share:

Nov 27, 2017

ZIJUE OFFER ZA VING'AMUZI 2017 KUELEKEA 2018

Tunaelekea katika kumaliza mwaka 2017 na tunategemea kuingia mwaka 2018, yapo mengi ambayo kupitia blog hii umefaidika kwa hali yeyote ile kama ndivyo tunashukuru kwakuwa ndio lengo letu, lakini pia nadhani yapo yaliyokukera kupitia blog hii kama ndivyo tunasikitika na kukuomba radhi pia maana sio lengo letu na ukizingatia hata kama itatokea unafanya jambo zuri vipi sio wote watakaopendezwa nalo kwa kuzingatia wapo ambao lengo lao ni kuharibu tu ama kutengeneza njia ya kufanya vibaya.. Zaidi ya yote shukrani kwa wale wote walio pamoja nasi kwa mwaka mzima na hata hapo miaka ya nyuma maana bila ninyi wala mimi na team yangu tusingefika hapa na isingezaliwa MADISH TECHNOLOGY.
Leo nawaletea orodha ya ving'amuzi vyenye offer katika msimu huu wa kumaliza mwaka 2017:-
 Bofya king'amuzi ambacho unataka kujua offer yake na utapata maelezo ya kina kuhusu offer hizo!
+255789476655 
Whatsapp+255784378129
Insta @mustaphamadish 
Share:

Nov 23, 2017

DISH 3 | DECODER & RECEIVER 18 | CHANNELS 18 | KWA KILA TV


Hotel - Tv system installation:- 
Hii ni hotel ina flow zipatazo tano ina zaidi ya room 50, ina ukumbi wa mikutano,sherehe, ina restaurant, ina bar na kuna sehemu ya Disco pia. Hapa tulichofanya ni kufunga tv ambazo ni zaidi ya 60 tv ambazo kila moja inapokea channels 18 na kila tv inajitegemea,nikiwa na maana mtumiaji anaweza akabadili channel bila kumuingilia mwengine ( tv nyengine ).




Mfumo uliotumika
  Baadhi ya Vifaa vilivyotumika:-
  • Dish ya FTA
  • Receiver kwa channel za Free
  • Dish ya DStv
  • Decoder za DStv
  • Dish ya Azam tv
  • Decoder za Azam tv
  • Signal Ampl.
  • Splitters
  • Multiswitch
  • Cable 
  • Connectors


Dish zimefungwa tatu, mbili zikiwa ni za kulipia na moja ikiwa ni ya channel za bure,Signal inayotoka kwenye Dish inaingia moja kwa moja kwenye chumba maalum, ambapo tunaita control room, sehemu ambayo decoder na receiver zote 18 zinafungwa hapo na sehemu kubwa ya mfumo mzima unafungwa hapo, kisha zinatoka cable ambazo zinakuwa zimebeba channel 18 na zote zinaishia kwenye tv ambazo zipo vyumbani na kwengineko kwenye jengo la hotel.

Hii ni Control Room sehemu ambayo ile connection muhimu yote tumeimaliza hapa

Kwa maelezo zaidi +255789476655
Whatsapp+255784378129
Face Book


Share:

Nov 11, 2017

TUNATENGENEZA UTOFAUTI NA WENGINE

Mwaka unaishia yapo yaliyoenda sawa na yapo ambayo yamezidi kwenda kombo, hapa nazungumzia ulimwengu mzima wa Digital tv, ulimwengu ambao umekuja na fursa kwa namba kubwa kwetu sisi vijana lakini pia kuna changamoto ambhata ambazo zinawakabili wote wanaohusika na mulimwengu huu wa Digital tv... zipo zilizopata utatuzi na zipo ambazo zinaonekana zinaenda kutatuliwa na hapo hapo zipo ambazo hata dalili kama zitakuja kutatuliwa hakuna... Mimi na team yangu kila kukicha tunajitahidi kuwa tofauti na wengine, yaweza kuwa walitutangulia ama wametukuta.. tumelifanya hili kwa uchache ingawaje pongezi tunazozipata inaonyesha walionufaika ni wengi sana kupitia uwanja huu..
Panapo majaaliwa mwakani tutafanya makubwa zaidi na kuwafikia hata ambao hawana uwezo wa kufika humu sisi tutawafikia.!!


 #MustaphaMaDish na zao lake #FundiMakini
Hivi kweli Fundi unafanyaje kazi chafu kama hii!!?? kuna baadhi ya mafundi wengine wamepata ajira kabisa makampuni makubwa yenye kuendesha huduma hizi za Digital tv lakini wanafanya kazi chafu na wanafikia hatua ya kupiga picha na kuzipost kwenye mitandao... mimi ama sisi huwa tunawaita kina #FundiKalipua mbioni kuja na Signal Quality tv
 








Aliyefunga hapa ni #FundiKalipua sio #FundiMakini Toka #MaDishTechnology
Whatsapp +255784378129
Share:

WAKATI MWENGINE TUNAZUNGUMZIA KAZI KWA SURA NYENGINE

 Eneo ni Hotel ya Sea Cliff ndani ya mgahawa wa Karambezi, robo 3 ya wateja wa mgahawa huu ni ngozi nyeupe na lugha itumikayo kwa wengi wa wateja wa hapa ni kiingereza na hivyo hata mazingira huwa kama sio Tanzania hivi...
Kwa mwezi wa 10 imekuwa ni sehemu ambayo nimetembelea zaidi ya mara 12 kwa nyakati tofauti ingawaje ilikuwa tunakula na kunywa lakini kikubwa ilikuwa ni kwa mazungumzo maalumu ya kikazi zaidi isipokuwa kwa sura nyengine na siku ya 12 mtu wa mwisho kufanya nae mazungumzo alikuwa ni Gabo na Deo.
Naweza kusema kila jambo ama hatua upigayo shukuru Mungu kwakuwa yeye ndiye anayekuwezesha!
Alhamdullah!



mustaphamadish@gmail.com

Share:

Nov 5, 2017

OFFER YA STARTIMES 2017 KUELEKEA 2018


MFALME WA BURUDANI ZA FAMILIA
Offer hii inakupa unafuu kama ifatavyo:-
  • Kwa Tsh 78,000 StarTimes ya Dish - Unapata vifaa pamoja na kifurushi cha mwezi mmoja.
  • Kwa Tsh 34,000 Decoder ya Antenna.
  • Ufundi Tsh 30,000 Startimes ya Dish.
  • Ufundi Tsh 20,000 Startimes ya Antenna.
  • Vifurushi vya Startimes Bofya Hapa
King'amuzi cha Startimes kinafanya vizuri sana kwa Offer mara kwa mara hutoa offer na zawadi kem kem hii ni katika kufanya wateja na wanaotaka king'amuzi hiki kupata ahueni!
Kwa Maelezo zaidi +255789476655 
Whatsapp+255784378129
Share:

Nov 1, 2017

OFFER YA ZUKU TV


Katika kumbukumbu yangu ilikuwa ili umiliki king'amuzi cha Zuku tv ni lazima ilikuwa uwe na Tsh150,000/= Bei ikashuka ikawa Tsh 105,000/=! Ikashuka tena kwa Tsh 95,000/=
Kwa sasa OFFER iliyopo ni tsh 88,000/= unapata Dish,Decoder,Kufungiwa na miezi mitatu bure!
Bei hii inakuwa ni bila ya ufundi, ufundi ni Tsh 20,000/=
Whatsapp+255784378129
mustaphamadish@gmail.com
NB:Usikubali kulipa zaidi!

Share:

Oct 31, 2017

TUMEFUNGA TV 15 | DISH 1 | MUHIMBILI HOSPITAL

Ilikuwa ni kazi ya siku moja ama 2 ila kutokana na mazingira yalivyo imetuchukua wiki 2 ama 3.. hii ni sehemu ambayo haitakiwi kelele na inapotokea idadi ya wagonjwa ni kubwa hakuna nafasi ya kina sie kufanya tulichokifanya hivyo ikawa tunachagua siku maalumu katika wiki ili kulitimiza hili tulilolifanya..
Huu ni mfumo ambao umetumia Dish 1 Decoder 1 lakini picha imeenda kwenye tv 15 na zote zikiwa saaaafi huku tukiacha wagonjwa wakipata alau taarifa ya habari...!


Tupigie +255789476655
Whatsapp+255784378129
Share:

Oct 30, 2017

STARTIMES UNALIPIA KIFURUSHI HAKIFIKI MWEZI!?

Jinsi inavyokuwa:- Kuna aina tofauti ya vifurushi kwa king'amuzi cha Antenna na Dish pia
Watumiaji wengi wa king'amuzi cha StarTimes hulipia pengine 9,000 ama 6,000 na kutegemea kifurushi alicholipia kiishi kwa muda wa mwezi mmoja,matokeo yake kinaenda wiki moja ama hata wakati mwengine hakifiki wiki malipo yanaisha na mtumiaji kutakiwa kulipia tena,hapa ndipo wateja wengi hutamani kukibeba king'amuzi na kukipiga chini!!!
Usichokijua ni kwamba:- Kifurushi ulichopo ni cha juu,yawezekana upo kwenye kifurushi cha Tsh 24,000 ama cha Tsh 36,000 hivyo inapotokea umelipia Tsh 9,000 ama Tsh 6,000 itahesabu siku hivyo haitafika mwezi channel zitakata!
Unachopaswa kufanya:- Ikiwa hujua upo kifurushi gani ni bora kufanya jambo moja la msingi upige simu kabla ama baada tu ya kulipia ili uhamishiwe katika kifurushi unachokitaka kikuwezeshe kufika mwezi mzima!
Kwa Maelezo zaidi!
+255789476655
Whatsapp +255784378129



Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita