Call / WhatsApp +255673378129

Oct 18, 2011

Dish thamani yake itabaki pale pale!!

Popote ulipo na popote utakapo unafunga.


Uzuri wa Satellite Dish Antenna ni popote ulipo ama utakapoamua kuweka makazi ukilifunga utakacho kuona utaona ikiwa clear bila chenga,Dish inakaa popote na Signal inaingia lakini lisikingwe ili kupata Satellite husika hii inamaana Dish huwezi kufunga chumbani!!
Kwa kuongeze ukifunga Dish huwezi muona mwanao wakati anaenda shule maana kuna maswali mengi tunakumbana nayo,huko mitaani watu wanadanganyana ya kuwa ukifunga Dish kama nyumba ya pili choo chao vile vya uswazi unaweza ukamuona!!

Jamani jamani sio kweli hiyo ni kazi ya CCTV Camera!!!
Share:

Aug 31, 2011

Savvanah Bar & Restaurant

In Quality centre Dar es salaam....!!!
Mpaka sasa najivunia kuwa na watu ambao wanaheshimu uwepo wangu,wanathamini mchango wangu na mengineyo mazuri kama hayo,hii imepelekea leo kupewa shavu palee kwenye jengo jipya kabisa la Quality centre lililop pugu road,hapa ndani pana kitu kipya pia kinaitwa Nivvanah bar & restaurant...!!
Hapa tenda ilikuwa ya wenzangu ambao walikuwa wanafunzi wangu na wao ndo waliosababisha mimi kuhitajika hapo kwenda kutoa ambacho nilistahili kukitoa na mwisho wa yoote ikawa kama ambavyo utapata fursa kutembelea na kujionea..!!
Kuna channels za Local na DSTV zaidi ya yote kumepambwa na flat screen ni hayo tu kwa leooo...!!!
Share:

Aug 8, 2011

DSTV offer imeisha..!!

Ilikuwa kama utani na kuacha watu wakajiuliza hee DSTV kunani tena ama ndo wameishiwa,ama wameteteleka kwa sababu ya STAR TIMES...!!!??
Baada ya kutoa bonge la offer kwa 89000/= uliweza kupata full installations..!!
Watu wakajisahau na wengine wakiamini wataendelea kushuka ndipo wao watakapofunga ila mambo yakawa ndivyo sivyo,offer imeisha na wengine wakiitamani hata ile bei ya 89000/= ambayo muda wake umeshaisha..!!
Jamani labda kama itakuwa mmepoteza umakini ni kwamba Multichoice ni kampuni kubwa na ipo serious na kazi zaidi ya yote wanajua wakifanyacho na hata burudani zao za ukweli na ndio maana hata wateja zao ni watu makini na ambao wapo up to date..!!

Share:

Aug 4, 2011

CHANNELS ZA TANZANIA KWENYE DISH..!!




 Swali ambalo nakumbana nalo kila kukicha ya kuwa channel gani na ngapi za Tanzania zinapatikana kwenye S.Dish na kwanini nyengine hazipatikani? huku wengine wakidhani channels zote za Tanzania zinapatikana kwenye S.Dish..!!
Zaidi ya yote kuna ambao mpaka leo hii wanaamini ya kuwa ukifunga S.Dish Antenna hata zile channel ambazo zinatumia Antenna zitakuwa hazina chenga kwa sababu karibu na Antenna hiyo kuna Dish...!!
Channels za Tanzania ambazo zinapatikana kwenye Dish ni zile tu zinazotumia Satellite kurusha matangazo yao mfano:-ITV,CAPITAL,EATV,AGAPE,CHANNEL 10,STAR TV na TBC1.
Pia hakuna ufundi wa kufanya nyengine zionekane kwenye Dish mpaka wahusika watakapoamua kujiunga na Satellite.
Uzuri wa kutumia Dish ni kwamba hata nje ya nchi channel husika inaonekana kwa kutumia dish lakini kama utatumia Transmetter kurusha matangazo itakuwa ni Tanzania tu tena wala si nchi nzima sehemu chache tu za nchi..!!
Hivyo kuna ulazima wa channel zote za Tanzania kujiunga na Satellite kurusha matangazo yao,hii ni kwa faida yao katika kujitangaza zaidi maana itakuwa inaonwa na watu wengi zaidi..!!
C2C,DTV,CTN,TV TUMAINI,CLOUDS.
Hizi hazipo kwenye Satellite hivyo hazipatikani kwenye Dish.
Share:

Jul 14, 2011

MAPIPA COMMISSION AGENCY

Pesa si mbaya ila matumizi ndio ambayo mabaya na hii ndio 1 kati ya matumizi mazuri ya pesa,japo yale mabaya hata wakati unafanya unaamini ni mazuri kwako..!!
Nilikuwa sehemu 1 wanapaita Magomeni Mapipa kuna yard mpya ya kuuza magari imefunguliwa inaitwa MAPIPA COMMISION AGENCY jamaa hawa wanauza gari aina zote mzigo unatoka moja kwa moja toka Japan na bei zao pia ni za kawaida sana..!!
Hapa bana nikawafungia dish mbili za KU (ndogo) lengo ni kuona DSTV na Channels za bure za MBC na lengo likatimia na mambo yakawa kama ambavyo pesa ilitumika kutaka mazuri ndivyo walivyoyapata..!!
Zamani banaa ndo ilikuwa mtaani ama nyumba ikifungwa dish wao wanaume lakini si sasa kwani bei ni za kawaida tu isipokuwa ilikuwa imani za watu tu,kama vipi tugongee nawe uzunguke dunia kama ambavyo wenzio wanavyozunguka wakiwa na TV zao majumbani..!
Share:

Jul 8, 2011

Somewhere in Tabata..!!

Haya ndio kati ya mambo yanayotufanya tuwe bize na heshima iwepo katika jamii na maisha yaweze kwenda mbele..!!
Hii ni sehemu moja wanapaita Tabata jijini Dar es salaam,kilichofanyika ni kuinstall DSTV katika vyumba vyote nyuma nzima pamoja na Local channels,zilizo kwenye Dish na zilizo kwenye Antenna kisha tukachukua vilivyo vyetu mwendo kijumba kinachofuata..!!
Share:

Jul 3, 2011

Tupo pamoja ila Email ni nyingi sana na zote nitazijibu..!!

C kwamba nimewapotezea wadau wangu laa hasha,ila kazi ni nyingi na utulivu unakuwa mdogo sana,yote ni ninyi mnaonifanya mimi niwe bize hivyo nathamini sana uwepo wenu hivyo wote mtapata kile mnachotaka ijapokuwa inaweza ikawa si kwa muda ule utakao ila ukiwa mvumilivu tatizo lako hapa ndipo kwenye solution.
Pamoja sana.
Mustapha MaDish.
Share:

Jun 20, 2011

TUSIUCHUKULIE POA UKIMWI..!!


 Kwa mtazamo wangu kutokana na research ndogo niliyoifanya inaonyesha kwa sasa swala la gonjwa la ukimwi si kama ilivyokuwa kama miaka ya nyuma na kadri siku zinavyozidi kwenda watu wanazidi kuchukulia poa na kuona kama  mtu kuugua mafua na maisha kuendelea kama kawa..!!
Nimetumia neno kuchukulia poa kwasababu katika watu ambao nawakusudia zaidi ni vijana ijapokuwa wote nataka twende sawa ila kwa vijana ni too much..!!
Leo hii NGONO imekuwa ndio inawatumikisha sana watu,utakuta watu wapo bize sana kwa ajili ya kufanya NGONO.wanatafuta pesa,wanaongopa,wanatumia muda mwingi sana na kufanya kila linalowezekana ili tu mwisho wa siku wafanikishe kufanya NGONO.
Siku hizi idadi ya walio wengi wanapenda sana ngono na upendo wa dhati unakuja baada ya kufanya ngono na hii inasababisha idadi ya wanaooa/kuolewa hupungua kila kukicha maana inakuwa ngumu kudumu kwa kutokupata kile ambacho either alikitegemea kabla ama alitaka tu kuona kiundani inakuwa aje..?
Mapenzi yanadumu miezi kadhaa tu then wanaachana ama mtu mmoja anakuwa na zaidi ya mpenzi mmoja na ndo pabaya sana hapa..
Unayemuamini ana wapenzi wawili nawe ukiwa wa tatu,hapo hapo nawe unakiacha unayemuamini unao wengine wa kuzugia pengine watatu,inaweza ikawa mpenzi wako unayemuamini hayuko poa kifedha hivyo kuna wa kukununulia vocha na matumizi mengine huku ukiwalipa kwa penzi lako lakini huna future nao,uliye na future nae ndiye huyo mwenye wapenzi wawili wewe ukiwa wa tatu na yaweza kuwa mmoja tu kati ya hao ndo unatumia kinga tena pia pengine siku za mwanzo mwanzo tu na mkishazoeana inakuwa mpango....!!
Hapa UKIMWI utatukosa ??
Kama ulikuwa hujui automatically kama utamsaliti mpenzi wako jua ya kuwa nawe atakusaliti ama anakusaliti...!!
Jamani,jamani UKIMWI upo tusijisahaulishe kama vipi tuwe na mmoja na yakishindikana hayo TUVAE..!!
Ni hayo tu kwa leo toka kwangu kuja kwenu.
Mustapha E. Hanya
Share:

Jun 17, 2011

CHANNEL ZINAZOPATIKANA EASY TV..!!

Ntawaletea idadi ya channel zote zinazopatikana kwenye ving'amuzi kutokana na maombi yenu ili muweze kuelewa na kufanya maamuzi yaliyo sahihi na leo hii naanza na EASY TV.
EASY TV ina jumla ya channels 32 ila zinazoonyesha ni 30 tu.
Movie 1
Movie 2
Movie3
Movie Arabic
Aljazeerah
CNN
BBC
CCTV4
UBC
Citizen
TBC 1
Star TV
Channel 10
Capital
EATV
TVZ
ITV
Clouds TV
EWTN/TV Tumaini
Mliman TV
Emmanuel TV
Peace TV
Channel V
Xing kong
Ph'x China
JSC document
JSC sport
MTV
Child
Ila kiukweli mfumo wa ving'amuzi wanaujua wenyewe maana channel wanazouza nyingi ni za FREE TO AIR hivyo satellite husika wakihama channel inapotea,hivyo mpaka baada muda ndipo wanairejesha na pengine isilejee tena..!!
Pia wanaweza kuongeza channel pale wanapoona channel ipo ipo tu na inafaa kutazamwa na watanzania wanaibandika..!!
Kwenye easy tv nimemalizia hapa next time ntahamia kwenye STAR TIMES na ntamalizia na TING ni hayo tu kwa leo n nawatakia week end njema wadau..!!

Share:

Jun 6, 2011

Transit Motel Airport

 Baada ya kusababisha Transit Motel ya ukonga kazi ikahamia Transi Motel ya air port na kazi ikawa ni moja tu kufanya TV zionyeshe kwa uzuri ili mteja aweze kidhi haja yake kwa kile anachotaka kukiona..!!

Nikaanza ingia chumba mpaka chumba na hiki ni chumba kimojawapo kati ya vyote vizuri vilivyopo..!!

 Mpaka hapa nikapita,wanapaita RECEPTION kwa niliowaacha ni mapokezi huwezi ingia mpaka upitia hapa


Hapo tayari kwa matumizi ya wageni kama si wenyeji ili maisha yaendelee huku ukiangalia TV ikiwa clear kabisa,ukipuliziwa na AC na pia ukitaka chakula ama kinywaji chochote unapiga tu simu unaletewa chumbani kama hautahitaji kutoka nje..!!
Nami nikachukua kila kilichochangu mwendo nikachapa..!!



Share:

May 31, 2011

TRANSIT MOTEL Ukonga kama kawa kama dawa...!!


 Ilinichukua siku mbili kufanya nilichofanya na kuacha TV za vyumba vyote zikiwa clear kabisa..!!
Inaitwa TRANSIT MOTEL hii ipo ukonga pale njia panda ya kwenda segerea..!!
 Hiki ni chumba kimojawapo kati ya vyote nilivyopita pita na kuacha TV za vyumba vyote vikiwa clear kabisa


Hapa ndipo mapokezi ukifika hapa lugha ambayo utakutana nayo ukiambiwa vyumba vimejaa utajilaumu sana,maana ni mapokezi mazuri na ukarimu ndani yake..!!
Napo kuna TV hivyo nayo pia nikaiweka clear kabisa..!!


 Mito ipo miwili inamaana ukiwa na mwenzako ndo mpango zaidi ila hata ukila alone TV yako itakuburudisha na kukufanya ukajisia uko home..!!

 Hapa ndipo kwenye mlango wa kuingilia...!!!
Imetulia kimuonekano na hata huduma zao na kila chumba kina AC,TV,SIMU vyumba vyote ni self na kama unausafiri utapark ndani ya geti zaidi ya yote bei zao ni kama buree..!!
Tarehe 31 yangu ya leo nimeimalizia hukooo...!!
Share:

May 29, 2011

TUNAUZA | TUNAFUNGA | TUNATOA USHAURI | VING'AMUZI

DISH NA VING'AMUZI AINA ZOTE.
PIGA:+255714973797
Share:

FLAT SCREEN NA TV BRACKET..!!

Mwezi huu tunaumalizia huku kukujuza umuhimu wa flat screen na tv bracket,pengine waweza ikawa wewe ni mmojawapo kati ya wale wanaoshangaa inakuwaje tv inaganda ukutani..!!
Tv inafungwa ukutani kwa kutumia tv bracket,tv bracket inakamata ukuta kwa kudrill na tv husika kwa kufunga na bolt,hii inakuwa salama kwa wezi,watoto ama hata nafasi haichukui nafasi kubwa na inaleta muonekano mzuri..!!
Hapa imeshafungwa ukutani.

Pia waweza kufunga kwenye sehemu kama hii.

Inategemea na utakavyo.


Pia unaweza kuigeuza kwa jinsi unavyotaka.
Hii inaitwa tv bracket.

 Hapa imeshafungwa ukutani bado kupachika tv.

Kiukweli ni nzuri na ya kupendeza iwe nyumbani,ofisini,hotelini na popote pale,zaidi ya yote ni kwa usalama pia..!!
Share:

May 28, 2011

BAHARI LODGE nimesababisha..!!



Ilikuwa Alihamisi na Ijumaa nilikuwa pale maeneo ya Bahari beach,wenyewe wanapaita njia panda ya kwenda bahari beach hotel dar es salaam,hapa kuna lodge moja ya kisasa safi sana inaitwa BAHARI LODGE..!!
Issue ilikuwa Local hazionyeshi kwa TV zote nami nilihitajika kusababisha hilo ili mmiliki na wateja waendelee kula bata kwa furaha kwa kupata walichokihitaji..!!

 Hii ni mojawapo ya room za hapa Bahari Lodge..!!
Ikawa zinapatikana Local channels zifuatazo:-
ITV
EATV
CAPITAL
TBC
TV TUMAINI
AGAPE
STAR TV
CHANNEL TEN
C2C.
Pia na DSTV kama ambavyo niliikuta,nami nikachukua kila kilicho changu na kushaa...!!


Share:

May 26, 2011

ARABISAT..!!

Jana nilikuwa maeneo fulani hivi wanapaita mwinyimkuu magomeni,hapa nilisababisha channels za kiarabu kama zijulikanazo ARABISAT kwenye dish ya c band ft6 na mzee alizipata channels hizi zifuatazo maana ndo mahitaji yake:-
JSC
Syrian TV
Southern Sudan
AD Alouta
Oman TV
Kuwait TV
Saudi TV
Qatar TV
Sharjah TV
Saud-Quran
Sudan TV
Saud-Sunnah
TVE-Internacional
Baada ya hpo nikamfungia na Antenna ya EUROMIND ili aweze kutumia king'amuzi na channels za Local kwenye TV bila kutumia king'amuzi.
Kisha tukasign out na crew yangu..!!
Share:

May 19, 2011

MWENDO NI ULE ULE...!!

 Wa nyumba hadi nyumba jengo hadi jengo ilihali dunia tunaileta nyumbani kwako ukiwa TV yako hata kama black n white utaifurahia...!!


Hapa ni maeneo ya sinza hapa nimeacha channel za gospel zikiendelea kama kawa ila usitishike na hiyo lebo ya DSTV ni dish tu,kutokana na ukweli kwamba dish zinaingiliana..!!

Share:

May 16, 2011

UNAILINDA VIPI DISH YAKO NA MVUA..??

 Ni jambo la kawaida mtu kulinda chake ili kidumu milele,hapa tunaweza kuona jambo ambalo watu wengi ambao wanamiliki madish wanapenda kulifanya kwa kuzuia mvua.....!!
Je wewe unalindaje dish lako...??




Share:

TUHESHIMIANE JAMANI....!!!

 Ni kawaida ya kuwa mtu ukifunga dish lazima nyumba iwe na hadhi fulani hivi ila kwa hapa tutaenda sawa tu ukiambiwa uishi upendavyo huku machannel ya kitu cha Dish yakipatikana kama hivyooo uonavyo....!!
 

Share:

May 14, 2011

Hakuna kinachoshindikana...!!

Share:

May 11, 2011

Mwanaume anasifiwa kazi...!!

Matembezi kwetu ni kama kawaida,hapa tumerejea tena kwa mdada mmoja hivi yupo maeneo ya Mbezi sala sala n mambo yakawa mswano,kana kwamba tunabomoa kumbe ndivyo twatengeneza...!!

Hii ni twin KU lnb kwa ajili ya channel za Gospel.


 Hii ni twin KU na twin C BAND,maana yake utapata channel za Local na Gospel na hiyo dish ndogo ni kwa ajili ya DSTV.

Share:

May 10, 2011

Nyumbani kwangu pia...!!

Icje ikawa ikawa kama fundi nanii yeye anatengenezea wenzie vitanda hali ya kuwa yeye analala chini...!!


Hii ni dish ya DSTV na hapa ni nyumbani kwangu ambapo napata usingizi,hivyo nami maisha yanaendelea kama ambao nawafungia hayo madish..!!
Share:

May 8, 2011

WEEK END KWETU HAINA TOFAUTI NA MONDAY..!!









Week end kwetu ni kama Monday vile maana mbio ndizo zilezile,7bu tupo kwa ajili ya kuwafurahisha wengine,huku yetu yakituendea vema...!!
Hapa ni katika J2 ya leo maeneo ya kulasini nishauza hapo na sasa naelekea sehemu moja wanapaita Tabata pale maeneo ya swiz pub...!!
Share:

May 7, 2011

WENYE KUMBI ZA KUONYESHA MPIRA KUPITIA DSTV IMEKULA KWAO...!!!


 Ni kilio cha watanzania wengi pande mbili kwa wakati mmoja,namaanisha kwa wale wapenzi wa mpira ligi za nje na wale wamiliki kumbi hizo...!!
MULTICHOICE TANZANIA ( DSTV ) kwa sasa ipo katika operations ya kuwafungia wale wote ambao walinunua DSTV kwa matumizi binafsi matokeo yake wakaenda kufanyia biashara kwa kutoza watu kiingilio na kufanya idadi ya wamiliki kumbi za kuonyesha mpira kuongezeka kila kukicha,huku idadi ya wateja wa kawaida kupungua kutokana na wengi kuangalia kupitia kumbi za mpira hizo....!!
Wapo ambao lishawakumba hili na kama wewe bado yakupasa ujiandae kwani wapo njiani,labda itangua ngumu kwa wale wenzangu namie walio ndani ndani,huku mafundi wao wakiwalinda maana ndo watoa taarifa wa kwanza...!!
Je hii ni kweli itaongeza wateja maana hakutakuwa na kumbi za mpira na kuwalazimu wapenzi wa mpira kufunga DSTV majumbani mwao...!!
Share:

May 6, 2011

NIPO KWENYE RESEACH ZAIDI....!!!

 
Kila kukicha yanazaliwa mapya nami naumiza kichwa kwenda sawa katika ukanda wangu huu....!!
Mfano leo Tanzania yetu imekuwa na mfumuko wa ving'amuzi na kufanya pia ufungaji wa madish kupunua ila mwisho wa siku bado dish linskuwa dish na king'amuzi kinabaki kuwa king'amuzi....!!
Ambacho wengi hawajui hata hayo makampuni yenye kuuza vinga'amuzi wanatumia Satellite Dish kukamata hizo channel zote zinazoonekana kwenye ving'amuzi vyenu..!!!
Hii inathibitisha ya kuwa still Dish itakuwa juu na ving'amuzi kufuata..!!
Ila kwa upande wangu nipo kwenye reseach ya kutaka kujua channel zote zilizopo kwenye Satellite ulimwenguni ambazo zinapatikana Africa pia zile zinazotumika na makampuni na kufungwa na kuwa za kulipia....!!
Lengo ni kupanua uwezo wangu katika fani hii na nashukuru mungu nimepata speed ambapo nimefanikiwa kwa kiasi fulani....!!
Share:

May 5, 2011

EWTN yanayoendelea Vatican city...!!


Hii ni Channel inapatikana kwenye C BAND ila sijaifanyia utafiti kama kwenye KU BAND kama inapatikana pia,ni ya dini ya wakristo na kwasasa kuna mambo yanaendelea kule Vatican city kuapishwa nadhani kwa viongozi wao...!!
Jana nilikuwa Bagamoyo pale maeneo ya Zinga kwenye kituo cha masister mahitaji yao ilikuwa ni channel ya EWTN pekee ili waone hayo yanayoendelea huko Vatican city..!!
Awali walikuwa tayari wana Dish ya c band ambayo walikuwa wanaona Local channel na za Gospel,hivyo nikawaongezea LNB ya c band na kusababisha Vatican city kuhamia Bagamoyo kwenye kituo cha masister...!!
  Kwangu ikawa mwazo mzuri kuinstall EWTN pekee kwani mpaka sasa nimepokea order zaidi ya nne kuhusu channel hiyo ambapo week end ntakuwa mzigoni kusababisha EWTN kuhamia majumbani mwa mwatu...!!
Share:

May 3, 2011

HOTEL INSTALLATIONS INAKUWA ILIVYOKUWA...!!

Hii inaitwa Multiswitch na mara nyingi hutumika mahotelini ama kwenye Apartment au hata kwenye nyumba binafsi,ila kazi yake ni kugawa Receiver zaidi ya moja kama uonavyo hapo,hizo cable zote zimeingia kwenye receiver....!!
Share:

Hapa hakuna kinachoonekana kamwe....!!

Satellite Dish ya aina yeyote ukiiona imezibwa hivi jua ya kuwa hakuna kinachoonekana kwenye TV,kwa sababu tunaposet huwa tunalenga kwenye Satellite husika hivyo lazima kuwe na mawasiliano baina ya Dish na Satellite kwa mtindo wa kulenga,hivyo ikizibwa maana yake ni kukata mawasiliano baina ya Dish na Satellite,labda niwape faida wenye madish woote kama ukiona Dish lako halionyeshi la kwanza kufanya ni kuliangalia Dish lako je halijazibwa..?? pili angalia cable haijachomoka..?? vyote vikiwa sawa ndo unapaswa kumwita fundi kwani zaidi ya hapo kutakuwa na issue ya kiufundi zaidi..!!
Share:

May 1, 2011

KOTA ZA BANDARI ILIKUWA BWAAA...!!

 
Ufundi banaa huzidiana yaani kama ubabe...!!
Mbabe wako ndo mnyonge wangu n hilo halina ubishi na ndivyo ilivyotokea hapa..!!
Jamaa alipewa issue ya kuhamisha Dish toka maeneo ya K'koo na kuhamishia Kulasini katika kota za Bandari,Dish ilikuwa ni ya c band zile kuuubwa wenyewe walikuwa wanaangalia Local channel...!!
Ilimchukua siku tatu kucheza nayo lakini wapi wazungu walikataa,ikamlazi jamaa kunitafuta baada ya kukubali matokeo ya kuwa usipokubali kushindwa c mshindani,nami tena kama nimezaliwa nayo hayo madude nikafika eneo la tukio nikasababisha watu wachekecheke na TV yao kisha nikachukua kila kilicho changu bila kusahau nimetumwa pesa kisha nikachapa mwendo...!!
Share:

HOUSE'S TOO CHEAP FOR SALE AT MBEZI LUIS..!!

NYUMBA INAUZWA MBEZI LUIS KWA FUNGO MIL.45
 

Muonekano kwa nje.





   Kwa uwani ndani ya uzio.                                                Kwa nje kupitia getini.   











                   Kwa uwani ndani ya uzio.


 Kwa uwani ndani ya uzio.

Ipo maeneo ya Mbezi luis kwa fungo,unaingia ndani kidogo toka Morogoro rd.Nyumba ni self-3 bed rooms,kitchen,toilet,store,sitting room na ina vyumba vya uwani v3,choo cha nje,pia inauwanja mkubwa wa kujenga nyumba kubwa uliozungushiwa ukuta na parking ya magari ndani ya gate.
Umeme ni LUKU.
Bei ya kuuza ni mil 45.Mazungumzo yapo hapo tutakapokutana na mnunuzi.
 Kwa maelezo zaidi piga simu no.+255659937711/+255763973797 au tuwasiliane  kwa
email: mustaphamadish@gmail.com
                      
                                                                                                                                                     

PLOT FOR SALE AT BAGAMOYO MJINI MIL.3 
Kiwanja kinauzwa kipo maeneo ya Bagamoyo maeneo ya nia njema karibu na shule ya msingi nia njema.Ukubwa wa kiwanja ni robo heka.Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa no. +255659937711

                                                                                                                                                      
  
PLOT FOR SALE AT BAGAMOYO MJINI MIL.3
Kiwanja kinauzwa kipo maeneo ya Bagamoyo kidongo chekundu.Ukubwa wa kiwanja ni robo heka.Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa no.+255659937711

                                                                                                                                                       

HOUSE FOR SALE AT MAGOMENI MAPIPA MIL.250.
Nyumba inauzwa ipo maeneo ya Magomeni mapipa mtaa Idrisa ni muundo wa National housing,ina vyumba 6 ndani,vyumba vitatu vya uwani,jiko,choo na store.Kwa maelezo zaidi piga simu no.+255659937711
Share:

Nawatakia sikukuu njema wajenga nchi wenzangu !

Leo ni tarehere 1 mwezi wa 5,kila tarehe hii imekuwa tunasherehekea sikukuu ya wafanyakazi,lengo na madhumuni ni kuthamini uwepo wa wafanyakazi na kukutana pamoja kuonyesha na kuzunguza ambayo yanaweza yakatupa changamoto wafanyakazi wa kila idara,huu ni mtazamo wangu kwa upeo wangu mdogo nilionao juu ya siku hii ya leo,pengine wewe unajua zaidi ya hii...!!
Hivyo popote mlipo nawatakia sikukuu njema watanzania wenzangu na msio watanzania pia maana lengo ni kujenga nchi huku mkono ukienda kinywani na maisha yakiendelea.
Kwa mwaka huu imefanyika kitaifa Morogoro mgeni rasmi akiwa mkuu wa nchi,binafsi napenda kuchukua nafasi hii kuwahusia vijana wenzangu kufanya kazi kwa bidii huku tukikumbuka ya kuwa "CHEZA NA MSHAHARA NA SI KUCHEZA NA KAZI" maisha mazuri hayaji kiurahisi yatupasa kufanyakazi kwa bidii sana na mliopo shule msome kweli maana kadri siku zinavyozidi kwenda maisha yanazidi kuwa magumu.
Ni hayo tu kwa leo wajameni....!!!
Share:

Apr 9, 2011

CARs FOR SALE....!!!

 Starlet Mil.4,500,000

 Noah Mil.13,500,000

 Vitz Mil.6,500,000

 Spacio Mil.8,600,000

GX110 Mil.13,500,000

For more informations call us +255659937711,mustaphamadish@gmailcom.
Pia tuna gari aina mbali mbali.
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita