Call / WhatsApp +255673378129

Showing posts with label Dstv. Show all posts
Showing posts with label Dstv. Show all posts

Nov 3, 2014

USISUMBUKE | PIGA +255658046655 | TUNAKUFATA ULIPO

Nilichogundua ni kwamba nina wadau wengi sana ambao haipiti siku bila kutembelea haka kablog chetu na kupata mawili matatu kuhusu ukanda huu..
Wengi mnataka kujua habari za ving'amuzi na huduma kwa ujumla..
Ufumbuzi wa ving'amuzi vyote upo kwenye haka kablog,maana yake ukishindwa kuelewa simu inahusika,ukipiga tu jua shida yako imeisha!


KWA KUWAJALI WATU WANGU...
Nimeanzisha huduma ambayo haikupi usumbufu na ni rahisi kwako!
Natekeleza maana ya huduma mtandaoni,kama tujuavyo huu ni wakati wa Digital hivyo lazima twende kidigital zaidi...
Swali unapenda/unataka king'amuzi gani kati ya hivi:-
DStv/Azam tv/Digitek/Continental/Zuku tv/Star times.
Piga simu sema unataka kipi,tunakupa ushauri na kisha utaletewa mpaka ulipo
Tukifika unalipia na kufungiwa papo hapo!
Ila hii ni kwa wakazi wa Dar es salaam tu!
Piga sasa +255784378129
TUMEBOBEA KUFUNGA KWENYE:-
HOTEL/APARTMENT/MAOFISINI NA MAJUMBANI.
BAADHI YA WALIONUFAIKA NA HUDUMA ZA MUSTAPHA MADISH:-
TRANSIT MOTEL/JB BELMONT/GERRAFE VIEW HOTEL/IKULU-OFFICE YA WAZIRI MKUU/PSPF/BAHARI BEACH LODGE/N.K.
Share:

Nov 1, 2014

HDMI CABLE


Imenipelekea kuandika post hii kutokana na simu niliyoipokea hivi karibuni kutoka Dodoma,lakini kabla ya simu hiyo kuwaelewesha wadau wangu kuhusu HDMI CABLE ni kawaida tu ila kwenye hii blog yetu leo wacha nitoe kile kidogo nilichonacho kwa wadau wangu!
Unapozungumzi HD
lazima ushirikishe cable inayoitwa HDMI CABLE,kwasababu ili uone picha katika mfumo wa HD ( Ubora wa picha wa hali ya juu ) ni lazima utumie HDMI CABLE,cable ambayo inatoa picha kutoka kwenye inaweza kuwa DVD/Receiver/King'amuzi ama chochote chenye uwezo wa kutoa HD na kupeleka kwenye tv ambayo nayo ikiwa ina uwezo wa kupokea HD.



Hii cable inachomekwa kwenye tundu lililoandikwa HDMI.
Ili kujua kama tv/DVD ama king'amuzi chako ni HD unapaswa kuangalia kwa umakini je kuna tundu lililoandikwa HDMI,kama lipo hilo jua kifaa chako hicho ni HD.
Je unavijua ving'amuzi vilivyo kwenye mfumo wa HD hapa Tanzania..??

  Una swali  piga +255789476655
Share:

Oct 27, 2014

VING'AMUZI VISIVYO NA MALIPO

Nilichogundua ni kwamba watanzania wengi wanapenda ving'amuzi rahisi,rahisi kwenye kununua na katika ulipaji wa kila mwezi na pindi linapotokea swala la kutokuwa na malipo ya mwezi inakuwa ndio unafuu zaidi,kwasababu wanzania wengi wenzangu na mie...
DIGITEK

Hiki hakina malipo ya mwezi kwa mujibu wa wao wenyewe,ukinunua kwa tsh 110,000/= 
Inakuwa umemaliza labda gharama yako itazidi ikiwa unahitaji na Antenna.
CONTINENTAL

Hiki nacho sio kama hakina ila kipo hivi,ukinunua unaangalia na kuanza kulipia baada ya miezi 12 yaani mwaka mmoja,ingawaje mpaka sasa malipo hayajaanza kufanyika.
Ya Antenna tsh 75000/=
Ya Dish tsh 105000/=

TULIPOTOKEA....
TING pia haikuwa na malipo ya mwezi ilikuwa ukinunua umenunua,lakini sasa malipo mwanzo mwisho...

MAONI | USHAURI | HUDUMA | +255789476655
Share:

Oct 16, 2014

UWEZO BINAFSI

Ijapokuwa imepita miezi ipatayo 10 ila hili ni moja kati ya niyakumbukayo na ya kujivunia pia na sababu napokea simu mpaka wakati mwengine naona imepitiliza ila kwakuwa ndo kazi yangu sinabudi kumaliza shida za wadau wangu...
Nakumbuka ni maeneo ya sinza pale kumekucha kwa mzee moja hivii wa kihindi nilifunga Azam tv,kama ilivyoada kulipua kwangu ni mwiko nikafanya yangu na kanuni zangu kisha nikakabidhi kazi kwa mteja wangu!
Mteja cha kwanza kuniambia "nimependa kazi yako,umechukua muda mfupi na kazi safi" kwa kulithibitisha hilo wakamtoka wekundu wekundu pale nje ya malipo ya king'amuzi,hii alitoa kama pongezi yake kwang,nami kwakuwa nimetumwa helaa aaah nikashukuru pale wekundu wangu mfukoni kisha nikachapa mwendo!
ilipita kama wiki mbili alipata tatizo la king'amuzi maana kulikuwa na fundi akaleta ufundi nyumbani kwake hivyo alitaka msaada wa fundi,ilimlazimu afike ofisini na kwa bahati mbaya sikuwepo..fundi aliyepo akachukua nafasi yake akaenda na mteja kuangalia tatizo...
Tatizo alilimaliza na mteja akaendelea pata burudani kama kawaida...
Ikapita kama siku kadhaa tu mbele akaja tena ofisini kwa kununua king'amuzi kingine ila kwasasa alitaka zuku lakini safari hii pia hakunikuta,alidai aondoke na vifaa vyake ila kufungiwa anataka afungiwe na Mustapha,nilijaribu kupigiwa simu nami nilisema ukweli ni kama baada ya siku nne ndipo nitakuwa na muda,kitu ambacho kila mmoja pale ofisini alishangaa kuona mteja anakubali kuningoja..
Haikuchukua siku nne bali yule mteja alingoja kama wiki na siku tatu ndipo nikapata muda wa kwenda kumfungia Zuku yake..
Na hapo ndipo nikapata malalamiko ya fundi aliyeenda kufanya repair baada ya kupita mimi..
Hakukuwa na maelewano mazuri,lugha ya biashara haikutumika hapa ila nilichofanya ni kumtaka radhi kisha nikampa burudani kama ilivyo ada!
Matokeo yake hataki fundi yeyote zaidi Mustapha.
Hapa tunazungumzia uwezo binafsi si kama najua saana,ijapokuwa najua vilivyo vingi ukanda wangu na hata aliyefanya hivyo ni mwanafunzi wangu kati ya wanafunzi wangu wengi tu ila alishindwa ama wanashindwa kufata ile misingi husika..
Mafanikio huja kwa kupenda unachofanya!
Ukipenda unachofanya,utakifanya kwa uwezo wako wote na hii lazima ufanikiwe..
Upo facebook Bofya hapa like page yangu kupata mapya ya ving'amuzi vyote Tanzania
Share:

Oct 10, 2010

GERAFFE VIEW HOTEL - DAR

Kwenye ukumbi ambao upo baharini wanapaita JET 1,kilichotakiwa hapa ni kufunga Flat Screen na Dstv,nami bila hiyana kama kawaida ile mikono salama ukafanya yake!
* Geraffe View Hotel (DSTV)


 Katika ukumbi huu wa JET 0ne As usually.





 Nafunga Dish sasa!! 

 

 Hapa natafuta signal baada ya kufunga Dish.

  Ni DSTV kama inavyoonekana katika FLAT SCREEN hii. 

+255784378129| Technical Support
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita