Call / WhatsApp +255673378129

Jun 30, 2016

KUFUNGA DISH NDOGO ( KU DISH INSTALLATION )

Kwakuwa karibu Ving'amuzi vyote Tanzania vinatumia Dish ndogo leo niwape kasomo haka alau mwenye kujaribu na ajaribu atakapopata wasaa!!
Fanya haya ili uweze kufunga Dish ndogo:-

1.Dish Antenna Assembly:
- Unganisha kifaa kimoja kimoja kama karatasi ya maelekezi inavyoonyesha ili kulikamilisha dish lako bila kuacha hata kimoja kwakuwa kila kimoja kina kazi na umuhimu pia.

2.Unganisha stendi yako ya kubeba dish.





3.Angalia sehemu nzuri ya kufunga Dish ili uanze kufunga stendi yako:
- Hakikisha sehemu unayoifunga mbele hakuna miti itakayozuia kupokea signal.
- Sehemu imara itakayoweza kukaa Dish bila kucheza.
- Unashauriwa kuifunga juu ya usawa wa nyuma/jengo ili isipate kuguswa guswa.

4. Funga stendi yako ya dish sehemu ulipoona panafaa.
5. Funga Dish lako kwenye stendi kwa kulielekezea Satellite uliyoikusudia ( Muelekeo wa king'amuzi husika )
6. Unganisha Coaxial cable ( Signal cable ) kwenye king'amuzi chako kwa nyuma sehemu iliyoandikwa LNB IN kisha unganisha kwenye either kwenye Dish sehemu ya LNB ama kama utakuwa na kitafuta signal (Signal  Finder ),kama utatumia Finder lazima uwe na Test cable ( Kipande cha cable ambacho utachomeka toka kwenye finder mpaka kwenye dish ( LNB ) - Nimetoa mfano wa Finder hii kwakuwa ni rahisi kupatikana na hata bei yake ni ya kawaida ila kuna finder nyengine hazihitaji Test cale.
7. Upo tayari kwa kuanza kutafuta signal. Jinsi ya kutafuta signal ntawaletea somo hilo katika post nyengine!
Tuangalie kwenye video hapo chini!



+255 789 476 655
Share:

Jun 16, 2016

UNAANGALIAJE MPIRA BILA KULIPIA/MALIPO NAFUU!


Wadau/Wateja wa ving'amuzi wakubwa ni wapenzi wa mpira hii ilikuwa hata kabla Tanzania haijaingia katika makubaliano ya kati ya zile nchi zilizoachana na mfumo wa Analogue tv na kuingia katika mfumo wa Digital tv..Hii inatokana na wapenzi wa mpira kutaka kupata mpira kwa njia yeyote ile,hivyo imekuwa kama ndo biashara ikiwa ni mdau wa ving'amuzi ili ufanye mauzo mazuri ni lazima ujue namna ya kupata kuonyesha mpira hii imepelekea kina sisi kuchangamkia fulsa kwanza kutafuta njia za kupatikana kwa channels zinazoonyesha mpira bure/kwa bei nafuu kwa udi na uvumba ili kuweza kuuza kwa wahitaji ukiachilia kampuni iliyo na idhini ya kuonyesha mpira Multichoice ( DStv ) ambayo hakuna mdau yeyote wa mpira ambaye halalamikii bei za DStv hususani Packeges za Sports,hii inapelekea kila kukicha kubuniwa njia za kuibia channels za DStv!
Post hii itakamilika hivi karibuni karibu....
Share:

Jun 13, 2016

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI KWENYE KING'AMUZI CHAKO


Pata msaada wa haraka na updates za Visimbuzi instagram @mustaphamadish
Hili ni moja kati ya yale ambayo ni kero kwa watumiaji wa ving'amuzi kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha na kukosa sehemu ya kupata maelezo ya kina kama hapa!
Swali la kwanza unatumia king'amuzi gani!?
Ving'amuzi vyote vyenye vifurushi ukilipa kifurushi ambacho si kile ulicholipia mwezi uliopita kama pesa pungufu hakuna picha utakayoiona na ikiwa pesa ni nyingi utaendelea kuona kifurushi kilichoisha,hivyo ili uone kifurushi ambacho umekusudia kutokana na pesa uliyolipa unapaswa kubadili kifurushi kwa kufata mtindo niliouelekeza hapa!
Chagua king'amuzi chako hapo chini ili kupata maelezo ya kina:-
  • Azam tv Bofya Hapa kujua kuhusu jinsi ya kuhama kifurushi!
  • Dstv Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
  • Startimes  Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
  • zuku Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
Kwa maelezo haya nadhani hakuna usumbufu utakaoupata tena
na  kwa maelezo zaidi no.yetu ni ile ile!
+255 789 476 655

Share:

Jun 10, 2016

SI LAZIMA KUTAFUTA FUNDI

Nilikwishasema na leo narejea tena inapotokea king'amuzi chako hakionyeshi la kufanya kwanza Bofya Hapa ukiona bado huelewi hebu fanya jitihada za kulifikia Dish lako ama Antenna yako!! Sasa kama hii Dish fundi atacharge pesa ya signal wakati ilikuwa ni kukata hayo matawi ya mpapai ama kuukata kabisa!
Ushauri wangu watumiaji wa Ving'amuzi mjiongeze mtuhitaji inapolazimika tu sio kwa kazi kama hizi ambazo wenyewe mnaweza kuzifanya,huwa sijisikii vema kufanya kazi ambayo situmii taaluma yangu mfano wa hii hapa!

Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita