Call / WhatsApp +255673378129

Dec 21, 2010

Nawatakia x-mass njema wadau...!!

2010 inaishia na sikukuu nazo ndivyo hivyo zinamalizika malizika kwa mwaka huu...!!
Kila mtu,kila nyumba,maofisi nk. watu wana mishe mishe za sikukuu ya x-mass na mwaka mpya,si mbaya nami nikawatakia maandalizi mema mpaka kufikia sikukuu wadau wote popote mlipo...!!
La msingi nawasihi msherehekee kwa amani na utulivu,huku mkijiuliza je mwaka unaishia huu lipi ambalo ulipanga kufanya limefanikiwa na kwa kiasi gani? ili mwaka unaoanza 2011 uanze na kila ulichokiacha,tufanye hivyo ili tufanikishe ujenzi wa Taifa letu pendwa Tanzania.
Share:

MAFUNDI WA DSTV NA DISH NYENGINE ZA BURE!!

 Je umewahi kukutana na usumbufu wa Mafundi wenye uwezo mdogo ama usumbfu wowote!!??
Je unahitaji kufunga DSTV mpya kwa bei halali bila kuongeza cha juu!!??
Je unahitaji kufunga Dish yenye channel za bure na ukaondokana na usumbufu wa kila siku kuita ita fundi!!?
 
 Fund dish akifunga Dish ya channel za bure
 
 Umeionaje hapa
 
Kwa Mafundi wa Dish Antenna aina zote na bei nafuu hapa ndipo mahala pake!!
Uzoefu usiokipimo na utapata ushauri bureee!!
Ufunge popote pale iwe Hotelini,Ofisini,Nyumbani na popote upendapo ndani ya Tanzania!!
Kuwa miongoni mwa walionufaika na huduma bora!!
0659161111
Share:

Dec 20, 2010

Zijue channel za nyumbani zinazopatikana kwenye Dish..!!








Hizi ndizo channel za Tanzania zinazopatikana kwenye Satellite Dish,ambayo inaanzia ft6 na kuendelea kwa kutumia C band lnb 1.
Unaweza ukajiuliza inakuwaje mtu anafunga dish kwa channel hizo tu,ila ambacho kitakuongezea ni channel za nje zikiwemo habari,movie na mengineyo...!!
Idadi ya channel inakuwa nyingi ama chache kutokana na idadi ya lnb na ukubwa wa dish pia lakini dish inayoanzia ft6 unaweza ukaona channel zaidi ya 60 zikiwepo na hizo hapo juu za channel Tanzania.
Share:

Dec 19, 2010

Dish hii haina uwezo....!!

Dish ndogo ( ku satellite dish ) haina uwezo wa kukamata channel zilizopo cband kama kwa mfano channel za Tanzania,pia haina uwezo wa kuondoa chenga zilizopo kwenye Antenna uliyofunga kwa ajili ya local kwani haina muingiliano wowote na channel zilizopo kwenye transmetter zaidi ya yote inatumia lnb ndogo tu.
Kwa kuongezea ukifunga Dish huwezi kumuona jirani yako akiwa anafanya mambo yake,maana wapo wanaoamini na kutoa soga za kwamba ukifunga dish ndo kila kitu hata mwizi wako unamuona jamani jamani si hivyo hayo mambo ni ya CCTV camera,nadhani nimesomeka......!!

Share:

Watu wanavyotafuta pesa......!!!

Ili mkono uende kinywani na hata ukikosa kicheko basi likutoke tabasamu ni lazima pesa zikutembelee,hata zikiwa za msimu na kwa kulijua hilo ndo maana watu wanaamka asubuhi wanajituma sana ilihali ankala ipatikane na maisha yaweze kwenda as usually banaa....!!
Kipindi wewe unaumia kutafuta pesa mwengine anaumia jinsi gani atakavyokuchukulia kiulaini na kuondoka nazo,akikuacha kwenye majuto ya ningejua ningenunua hata nanii... ila inakuwa ushachelewa wenye kazi zao washachukua mahela yao...!!
Kiukweli nilichogundua tunapenda sana shortcut ya maisha ila tunasahau misemo ya wazungu yenye maana kubwa sana,NO PAIN NO HONEY au NO GANE WITHOUT PAIN sasa iweje tupende vizuri bila kutaabika...??
Maisha ni magumu sana tena na bila kujituma kamwe hauwezi kutoka na kupenda shorcut madhara yake ni makubwa sana,pesa bila kufanya kazi ni sawa na kulipwa kabla ya kazi maana kazi utakuja ifanya tu siku za usoni,tena inaweza ikawa ni ngumu kuliko malipo ambayo ulikwishapokea,kuwa makini especially vijana wenzangu..!!
 Hii ni picha tu ambayo najua itakuwa imewatamanisha wengi na kudhani nina zaidi ya hizo kwenye akiba yangu kumbe ni picha tu wanaharakati wenzangu....!!
Nimeandika hii kutokana na jamaa fulani ambao waliwahi kunipigia simu kitambo kidogo,wakidai kunifahamu sana na kudai kuna wazungu wamefikia hotel hapa dar na walitaka kufanya biashara hivyo hawana mwenyeji,jamaa mmojawapo katika mtandao huo ambaye alijifanya yupo mkoa na ndiye ananijua mimi kwa maelezo yake,akaomba mimi niwe mwenyeji na kuna madawa ya mazao ama kitu kama mifugo ambayo yanapatikana s.group hivyo niwe kama mtu wa kati then nitapata % fulani....!!
Kusema kweli alivyokuwa ameanza huyo jamaa ndipo alipokosea na nikagudua hanijui bali alipata contact zangu kutoka mtandaoni ama kwa mtu hivyo hata dili yenyewe ilikuwa ya uongo kama jinsi alivyoanza nami nikawapotezea.....!!
Baada ya muda jamaa yangu mmoja nae akanihadithia kama ambavyo mimi nilikumbana nayo ila yeye ikawa wamefika kwenye suala la kutakiwa kutoa pesa kidogo ili apate kingi....!!
Kama ni watanzania ama wageni tunaenda wapi....???
Umakini katika pesa iwe wa hali ya juu otherwise mtalia jamani.....!!
Share:

EURO MIND Antenna

Si wanainchi wote ambao wana uwezo wa kufunga Dish ama king'amuzi kutokana na hali ya maisha jinsi ilivyo na kwa upande wa pili pia si channel zote za nyumbani zinazopatikana kwenye Satellite Dish ama hata penye king'amuzi pia,hivyo swala la Antenna linabaki pale pale kwamba ni la muhimu si uwezo ijapokuwa linahusika pia.
Kwa wapatao tabu kuhusu Antenna ipi inaweza ikawasaidia kuona picha clear kutokana na eneo waishilo,jibu ni moja tu EURO MIND Antenna na ikitokea haishiki basi ujue eneo lako halistahili Antenna.
Kwa wale wenzangu na mimi wa uswazi kuna zile tube ambazo unazifanyia mambo na kuwa bonge la Antenna.
Share:

KU na minara dam dam....!!

 Lau ingelikuwa nainstall C band hakika ningekesha bila kuwa na single solution cable kwa kuwa kungekuwa na kitu kinaitwa interference maana uwapo mnara either wa simu ama mitambo mitambo Satellite Dish hasa C band linakuwa kama linakingwa hivi ama kupungua uwezo wake wa kukamata sawia satellite husika,baada ya wataalamu kulijua hilo wakatutengenezea kifaa ambacho kinaweza kuimili mikiki hiyo nayo ni SINGLE SOLUTION CABLE hii ni kwa Dish kubwa tu...!!
Kwa dish ndogo ni nadra sana kutokea interference hata kama kuna mnara mbele kama nilivyoinstall hiyo DSTV maeneo ya Afri center na mambo yakawa swaafiii...!!!
Ukienda mbali zaidi zipo lnb za dish ndogo ambazo nazo kazi yake ni kukabiliana na interference....!!
Share:

DSTV OFFER IMEFANYA USIKU KUWA MCHANA...!!

Hapa ni maeneo ya sinza karibu na shule ya msingi GRACE,nyumbani kwa mdada mmoja hivi anafanyia kazi pale tigo mliman city,kutokana na ratiba kuwa ngumu katika kipindi cha offer ikatufanya tufike saa 12 jioni na kutulazimu tusababishe ili watu waone walicholipia na usiku ukatukutia hapo.......!!
Lakini pamoja na hayo mpaka kwenye saa mbili kasoro ikawa wanaume tunachapa mwendo na siku ikawa bulubulu kama zege halikulala maana ingeharibu ratiba ya kesho.....!! 

 Kutoboa matundu na drill ili kufunga stend ya Dish ya DSTV

 Hapa kutafuta signal ya DSTV

 Stend imekaa inavyotakiwa

 
 Hapa signal ya kutosha picha inaonekana


Finder inafanya kazi nyakati zote kutokana na mazingira nikiwa na maana ya kuwa hata usiku pasipokutumia taa yenyewe ina taa ambayo inaweza kujiteemea hata kwenye giza totoloo....!!
Share:

Dec 18, 2010

AV selector

Kuna TV nyingi ambazo zina AV moja ama mbili na mtumiaji akawa ana vya kuchomeka zaidi ya viwili.
Mf: ana DVD,Receiver,Decoder,King'amuzi na Game labda,hapo hapo TV yako ina AV moja ama mbili hivyo itakuwa inakulazimu kuchomoa na kuchomeka kila muda ambao unataka kuangalia kimojawapo kati ya hivyo,ambapo itakuwa usumbufu licha ya hivyo pia ile kuchomoa chomoa kila wakati AV cable ni rahisi kukatika.
Napenda kukujuza ambacho labda ulikuwa hukijui....!!
kuna kitu kinaitwa AV selector kazi yake ni kuunganisha vyote kwa wakati mmoja,nikiwa na maana ya kuwa kama ni DVD,Receiver,Decoder,King'amuzi na hata Game na vyote ukaona bila kuchomoa chomoa...!!


Kazi yako itakuwa ni kubadili kwa kubonyeza AV selector yenyewe kwa namba husika kwani katika kuchomeka kwako kutakuwa na namba kwa kila ambacho utachomeka kama DVD no.1,Receiver no.2 na vilivyobakia kwa mtindo huo huo hivyo itakuwa ukibonyeza namba 1 itaonyesha DVD,namba 2 Receiver na vyote kulingana na jinsi utakavyobadili.
Kuna AV selector ambazo zinatumia remote na zisizotumia,kuna za umeme na zisizotumia umeme,kuna kuanzia njia tatu na kuendelea.

Share:

Segerea ilikuwa pangu pa kavu....!!

Offer bado inaendelea nami nazidi kusababisha watu wafurahie maisha,nilikuwa maeneo maeneo wanapaita segerea ambapo nyuma ya nyumba hizi ndipo ilipo gereza la segerea.....!!
Hapa tatizo kubwa lilikuwa ni pa kufunga dish maana nyumba ilikuwa imejengwa kiaina yake,kwa kawaida ili dish likae kwa uzuri na usimwite fundi kila baada ya muda ni lazima tudrill ukutani lakini sometimes inakuwa haina jinsi kama ilivyo hapa na ndio tukaamua tufunge kwenye mbao ili tu mwenye yake aweze kuona kama yalivyo matakwa yake......!!
 Tumeangalia ubora wa mbao kama kweli unaweza kubeba dish na ndipo tukafunga maana unaweza ukafunga ile unaondoka tu unapigiwa simu ya kwamba dish lipo chini....!!









Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita