Call / WhatsApp +255673378129

Dec 29, 2010

Mbio za funga mwaka ndani ya bwaga moyo.....!!

Tunahesabu siku tu kuelekea mwaka mupya mupya kabisa 2011,huku tukiumalizia malizia mwaka huu 2010,ukiniacha na kumbukumbu nzuri ya kusherehekea siku yangu ya kuzaliwa kwa namba za kipekee ambazo kamwe hazitajirejea 10.10.10 maana nilizaliwa miaka kadhaa nyuma ikiwa ni tarehe 10 mwezi wa 10.
Tukiyaacha hayo leo nipo bwagamoyo na nadhani nitakuwepo huku mpaka kesho ama kesho kutwa na hakuna kilichonileta huku zaidi ya kazi na na7bisha kama kawa yangu.....!!
Share:

Dec 28, 2010

Kuelekea 2011 yapi mazuri na ya kupongeza 2010....!!

Kwa kuanza tu naweza nikasema kwa mwaka huu 2010 ni mwaka mgumu sana hasa kwa vijana,yananitoka haya kutokana na mazungumzo yao pale unapokaa nao,maana wenyewe wanakwambia hakuna njia kama milango inazidi kufungwa ili watu wasitoke,hivyo kipindi wao wanasema hivyo sijui wewe unasema aje kuhusu mwaka huu unaoishia.....!!
Upande wa kazi banaa jua halikuwa kali saana maana ushindani ulikuwepo ila si mkali sana ni wa kawaida tu,ilizaliwa kampuni inayojulikana kama star times ambayo kuna mkono wa TBC na wachina,ambao wamekuja tofauti kidogo,badala ya kutumia dish wao walitumia Antenna na decoder,ni kitu kizuri na watanzania wamekipokea ila si kama ambavyo walidhani hasa baada kufa GTV na kusemekana inakuja kampuni ambayo itakuwa inafanana na GTV ili kuleta ushindani na DSTV katika swala la mpira kuhusu malipo ya mwezi,sitaki kuelezea sana ila tukaitambua star time na utofauti wa kutumia antenna ila yenyewe si ya kwanza ilitangulia EASY TV ambayo mpaka sasa bado ipo na inafanya vizuri pia.
Pia ATN nao wametoa ving'amuzi vyao ikiwa hawana tofauti na star time ila wao wapo kidini zaidi na channel zao,hii ina maana kwamba kwa mwaka ujao 2011 kutakuwa na mapokezi ya vingamuzi vyengine toka kwa wamiliki wa makampuni ya habari Tanzania,ugomvi wa kibiashara ndio sababu ya kuwaumiza watanzania kwa kuwalazimisha kujaza decoder majumbani kwao.......!!
Star times ilitosha kabisa kukidhi mahitaji ya watanzania ijapokuwa Easy tv nao walikidhi ila sijui sababu ni nini mpaka wakatolewa maana na TBC kuamua kuanzisha ya kwao ambayo channel zote za Mengi hazipo,ikisemekana hawataungana maana wana ugomvi wa kibiashara,huku easy tv ikiwa na channel zote za local mpaka TVZ.....!!
Ni meengi sana kipindi tunaendelea kukumbuka lichukue hili...!!
Share:

Dec 26, 2010

Boxing day nime7babisha like this......!!!

Ikiwa ni siku 1 baada ya kusherehekea sikukuu ya x-mass,kilichofuata ni kupeana zawadi kwa kwenda mbele nami nina wangu wa kuwapa banaa...!!
Unadhani zawadi kwangu itakuwa ni nini kama si ku7bisha ili wengine wafurahie na familia zao na maisha yaweze kusonga mbele kama ilivyo ada ili kuutengeneza mchana na usiku,leo ni jumapili saafi kabisa nami nipo nafanya haya ambayo nimejaaliwa kufanya siku hii ya leo...!!
Unajua watu wanashindwa kuelewa kuna watu duniani wamezaliwa kwa ajili ya kuja kufurahisha watu wengine tu duniani nami nikiwa mmojawapo na kama hukulijua hilo ichukue hii na utembee nayo,ili siku ukipata bahati ya kukutana na mimi nawe uweze kufurahishwa pia....!!
Hii ni nyumba ya mtu,ambaye ana tv mbili sitting room na bed room na alitaka kuona picha clear kote kwa kutumia Satellite Dish Antenna na kila mtu kuangalia channel aipendayo kwa wakati mmoja bila kumuudhi mwengine,nami nika install FTA channel za Local na Gospel,Dish 1 ila Receiver 2,pia nikafanya Extra view upande wa DSTV na boxing day kwangu ikaishia hivii....!!
Share:

Dec 25, 2010

Near at Bondeni Hotel Magomeni mapipa

Hapa ufundi ukiendelea
Mcheza kwao hutunzwa na ndivyo ilivyo kila siku ziendazo kwa mungu,hapa ni Magomeni mapipa yaani ni mitaa ya nyumbani wenyewe wanasema mitaa ya kujidai ni karibu na Bondeni hotel ambayo inaonekana kwa mbele kule yenye rangi nyeupe kwa wenye macho....!!
Hapa banaa ilikuwa tatizo local channel hii dish ilifungwa kitambo isipokuwa ilihama tu kidogo kwenye position yake,hivyo nikafanya nilichokifanya ikawa heee watu wanaona wabongo na wazungu wazungu,nami nikachukua vyangu nikachapa mwendo kujiandaa kula chakutoka cha x-mass....!!
Share:

Dec 24, 2010

Tuanaendeleza mbio kama kawaida....!!

Unaambiwa kimbia kipindi wenzio wanatembea....!!
Ila mbio ukimbiazo isije ikawa upo nje ya mstari kiasi kwamba unachoka kabla ya kufika utakapo...!!
Mda huo yule aliyekuwa ananyata anakupita kama anamsukuma mlevi vile...!!
Nashukuru mpaka kufikia hapa ila kiukweli nipo bize sana wale walionitumia email then sijarepply si kwamba nimewapotezea laa hasha ubize ndo unao7bisha na ambacho naweza kusema tupo pa1 daima zaidi ya yote nawatakia sikukuu njema...!!
Share:

Dec 21, 2010

Nawatakia x-mass njema wadau...!!

2010 inaishia na sikukuu nazo ndivyo hivyo zinamalizika malizika kwa mwaka huu...!!
Kila mtu,kila nyumba,maofisi nk. watu wana mishe mishe za sikukuu ya x-mass na mwaka mpya,si mbaya nami nikawatakia maandalizi mema mpaka kufikia sikukuu wadau wote popote mlipo...!!
La msingi nawasihi msherehekee kwa amani na utulivu,huku mkijiuliza je mwaka unaishia huu lipi ambalo ulipanga kufanya limefanikiwa na kwa kiasi gani? ili mwaka unaoanza 2011 uanze na kila ulichokiacha,tufanye hivyo ili tufanikishe ujenzi wa Taifa letu pendwa Tanzania.
Share:

MAFUNDI WA DSTV NA DISH NYENGINE ZA BURE!!

 Je umewahi kukutana na usumbufu wa Mafundi wenye uwezo mdogo ama usumbfu wowote!!??
Je unahitaji kufunga DSTV mpya kwa bei halali bila kuongeza cha juu!!??
Je unahitaji kufunga Dish yenye channel za bure na ukaondokana na usumbufu wa kila siku kuita ita fundi!!?
 
 Fund dish akifunga Dish ya channel za bure
 
 Umeionaje hapa
 
Kwa Mafundi wa Dish Antenna aina zote na bei nafuu hapa ndipo mahala pake!!
Uzoefu usiokipimo na utapata ushauri bureee!!
Ufunge popote pale iwe Hotelini,Ofisini,Nyumbani na popote upendapo ndani ya Tanzania!!
Kuwa miongoni mwa walionufaika na huduma bora!!
0659161111
Share:

Dec 20, 2010

Zijue channel za nyumbani zinazopatikana kwenye Dish..!!








Hizi ndizo channel za Tanzania zinazopatikana kwenye Satellite Dish,ambayo inaanzia ft6 na kuendelea kwa kutumia C band lnb 1.
Unaweza ukajiuliza inakuwaje mtu anafunga dish kwa channel hizo tu,ila ambacho kitakuongezea ni channel za nje zikiwemo habari,movie na mengineyo...!!
Idadi ya channel inakuwa nyingi ama chache kutokana na idadi ya lnb na ukubwa wa dish pia lakini dish inayoanzia ft6 unaweza ukaona channel zaidi ya 60 zikiwepo na hizo hapo juu za channel Tanzania.
Share:

Dec 19, 2010

Dish hii haina uwezo....!!

Dish ndogo ( ku satellite dish ) haina uwezo wa kukamata channel zilizopo cband kama kwa mfano channel za Tanzania,pia haina uwezo wa kuondoa chenga zilizopo kwenye Antenna uliyofunga kwa ajili ya local kwani haina muingiliano wowote na channel zilizopo kwenye transmetter zaidi ya yote inatumia lnb ndogo tu.
Kwa kuongezea ukifunga Dish huwezi kumuona jirani yako akiwa anafanya mambo yake,maana wapo wanaoamini na kutoa soga za kwamba ukifunga dish ndo kila kitu hata mwizi wako unamuona jamani jamani si hivyo hayo mambo ni ya CCTV camera,nadhani nimesomeka......!!

Share:

Watu wanavyotafuta pesa......!!!

Ili mkono uende kinywani na hata ukikosa kicheko basi likutoke tabasamu ni lazima pesa zikutembelee,hata zikiwa za msimu na kwa kulijua hilo ndo maana watu wanaamka asubuhi wanajituma sana ilihali ankala ipatikane na maisha yaweze kwenda as usually banaa....!!
Kipindi wewe unaumia kutafuta pesa mwengine anaumia jinsi gani atakavyokuchukulia kiulaini na kuondoka nazo,akikuacha kwenye majuto ya ningejua ningenunua hata nanii... ila inakuwa ushachelewa wenye kazi zao washachukua mahela yao...!!
Kiukweli nilichogundua tunapenda sana shortcut ya maisha ila tunasahau misemo ya wazungu yenye maana kubwa sana,NO PAIN NO HONEY au NO GANE WITHOUT PAIN sasa iweje tupende vizuri bila kutaabika...??
Maisha ni magumu sana tena na bila kujituma kamwe hauwezi kutoka na kupenda shorcut madhara yake ni makubwa sana,pesa bila kufanya kazi ni sawa na kulipwa kabla ya kazi maana kazi utakuja ifanya tu siku za usoni,tena inaweza ikawa ni ngumu kuliko malipo ambayo ulikwishapokea,kuwa makini especially vijana wenzangu..!!
 Hii ni picha tu ambayo najua itakuwa imewatamanisha wengi na kudhani nina zaidi ya hizo kwenye akiba yangu kumbe ni picha tu wanaharakati wenzangu....!!
Nimeandika hii kutokana na jamaa fulani ambao waliwahi kunipigia simu kitambo kidogo,wakidai kunifahamu sana na kudai kuna wazungu wamefikia hotel hapa dar na walitaka kufanya biashara hivyo hawana mwenyeji,jamaa mmojawapo katika mtandao huo ambaye alijifanya yupo mkoa na ndiye ananijua mimi kwa maelezo yake,akaomba mimi niwe mwenyeji na kuna madawa ya mazao ama kitu kama mifugo ambayo yanapatikana s.group hivyo niwe kama mtu wa kati then nitapata % fulani....!!
Kusema kweli alivyokuwa ameanza huyo jamaa ndipo alipokosea na nikagudua hanijui bali alipata contact zangu kutoka mtandaoni ama kwa mtu hivyo hata dili yenyewe ilikuwa ya uongo kama jinsi alivyoanza nami nikawapotezea.....!!
Baada ya muda jamaa yangu mmoja nae akanihadithia kama ambavyo mimi nilikumbana nayo ila yeye ikawa wamefika kwenye suala la kutakiwa kutoa pesa kidogo ili apate kingi....!!
Kama ni watanzania ama wageni tunaenda wapi....???
Umakini katika pesa iwe wa hali ya juu otherwise mtalia jamani.....!!
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita