Call / WhatsApp +255673378129

Jun 6, 2012

KARIBUNI WAPENDWA!!

Tarehe 10.06.2012 jumapili,40 ya baba yangu marehemu ESMAILY O.HANYA hivyo kama utapata chance karibu sana,inafanyika nyumbani kwake Magomeni Mapipa,Idrisa street no.27,karibu na delux bar/chipolopolo bar/kwezi dispensary,itakuwa saa 7 mchana!!
Nawakaribisha wote ndugu jamaa na marafiki wa ukweli!
Share:

May 19, 2012

NITANUNUA VING'AMUZI VINGAPI!!??

Tarehe 31.12.2012 saa 23:59 itakuwa mwisho wa Local channel kupitia c band na Antenna pia na ili upate Local itakulazimu ununue king'amuzi ama ving'amuzi kutokana na channel za Tanzania utakazo!!
Mawazo yangu binafsi kulikuwa na mapungufu mengi sana kwenye mchakato huu na mwisho wa siku inaonyesha dhahili wakuu walikurupuka hawakufikiri kwa kina kabla ya kuweka mwisho mwaka huu!!
Tuangalie hali za watanzania wengi wao ni duni then tuangalie bei za ving'amuzi na channels zinazopatikana kwa kila king'amuzi,kuna kampuni moja tu ambayo binafsi naipa pongezi za kutosha EASY TV unapata Local channels karibu zote na bei yao ni 9000 tu kwa mwezi lakini zooote tupa kule!!
Nawaangalia wale wa vijijini ina maana hawastahili tunachokipata!!?? maana ilikuwa mtu anajipinda anafunga Dish ya Local anasahau,haina malipo ya mwezi wala nini zaidi ni kurekebisha tu litakaposumbua!!
Au ndo wazo la mtu mmoja tu alienda nje ya nchi akaona watu wapo UP TO DATE then akaja Tanzania kuwashawishi viongozi wakalipitisha,je mnajua hao ambao wanakwenda na wakati walianzia wapi!!??
Wananchi wengi watakosa haki yao ya msingi ya kupata habari kwa kukosa pesa ya kulipia ili aone/asikie hiyo taarifa ya habari.
IJAPOKUWA HATA NKISEMA WALIOLIPITISHA LIMEPITA,HAKUNA JINSI ILA UJUMBE SI MBAYA UKAWAFIKIA NA MKAONA MLIVYOVURUNDA HAPA!!
Ina meengi sana ila wacha niishie hapa nisije nikanyimwa hata hizo tenda maofisini mwao maana ndo hao hao wateja zangu!
Share:

May 5, 2012

TULIKUPENDA ILA MUNGU AMEKUPENDA ZAIDI

Nipo hapa kuwataarifu habari ya msiba wa baba yetu mpendwa MR ESMAILY OMARY HANYA wa magomeni mapipa mtaa Idrisa no.27.
Napenda kunukuu maneno ya mwenyewe MUSTAPHA ESMAILY O.HANYA kwa wadau wake wa blog hii "Muda mwingi sikuwa hewani kwasababu nilikuwa namuuguza baba yangu ambaye kwa bahati mbaya jana ametutoka na mazishi yanakuwa leo saa kumi jioni magomeni mapipa mtaa uweje no.47."
Kwa niaba ya Mustapha Esmaily Hanya.
Naitwa N.Salmin
Share:

Apr 10, 2012

RIPOTI KAMILI YA MADAKTARI!!

NI BAADA YA JOPO LA MADAKTARI MUHIMBILI KUMFANYIA UCHUNGUZI MPENDWA WETU S.KANUMBA.
 

MSANII nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba amefariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo linalojulikana kitalaamu kama Brain Concussion, taarifa za kitabibu zimeeleza.
Taarifa hizo za ndani, zilizopatikana jana baada ya jopo la madaktari bingwa watano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu huyo, zimeeleza kuwa tatizo hilo linaweza kumfanya mtu apoteze maisha mara moja au baada ya siku kadhaa. Mmoja wa madaktari hao ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini alisema waligundua tatizo hilo baada ya kumfanyia uchunguzi huo kwa zaidi ya saa mbili.

“Tulianza kuufanyia uchunguzi mwili wa marehemu kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 6:45 mchana na tukagundua kuwa marehemu alifariki kutokana na mtikisiko wa ubongo kwa kitaalamu, Brain Concussion,” alisema daktari huyo. Alisema Kanumba alipata mtikisiko wa ubongo ambao husababisha kufeli kwa mfumo wa upumuaji (cardio-respiratory failure) “Kilichomuua hasa ni mtikisiko wa ubongo, ambao endapo unatokea katika sehemu ya nyuma ya ubongo (cerebrum), huua kwa haraka” alisema daktari huyo na kuongeza kuwa mtikisiko wa ubongo  wa nyuma, husababisha matatizo ya mfumo wa upumuaji na hilo limeonekana katika mwili wake.

“Baada ya ubongo wake kutikiswa kwa nguvu, mfumo wa upumuaji ulifeli na ndiyo maana tumekuta kucha za Kanumba zikiwa na rangi ya bluu, huku mapafu yake yakiwa yamevilia damu na kubadilika kuwa kama maini, hizo ndizo dalili za kufeli kwa mfumo wa upumuaji.”

“Mtu aliyepata mtikisiko wa ubongo huweza kutokwa na mapovu mdomoni na hukoroma kabla ya kukata roho na ndivyo ilivyokuwa kwa Kanumba kabla hajafariki.”

Daktari mwingine aliyeshiriki katika uchunguzi huo ambaye pia aliomba jina lake lisitajwe alisema ubongo wa mwigizaji huyo ulikuwa umevimba na kushuka karibu na uti wa mgongo na hivyo kuathiri mfumo wa upumuaji.

Alisema sehemu ya maini na majimaji ya machoni ya marehemu, vimepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali ili kubaini endapo kuna sumu au kitu kingine katika mwili huo.

Baba mzazi azungumza Baba mzazi wa mwigizaji huyo, Charles Musekwa Kanumba alisema kwamba alipata taarifa za kifo cha mwanawe Jumamosi saa 10:00 alfajiri baada ya kupigiwa simu na dada wa marehemu, Sara Kanumba.  “Sara aliniuliza: ‘Una taarifa yoyote kuhusu mwanao Kanumba?’ Nikamjibu kuwa sina taarifa yoyote, ndipo aliponieleza habari za kifo hicho. Aliniambia Kanumba hatupo naye tena amefariki kwa kuanguka, amekorofishana na mpenzi wake.”  alisema taarifa hizo zilimsababisha aishiwe nguvu kwa kuwa kilikuwa kifo cha ghafla… “Basi kuanzia hapo, nilianza kupigiwa simu za kupewa pole, ndipo nilipoamini kumbe mwanangu amefariki.”

 Akizungumzia kuchelewa kufika msibani, alisema kumetokana na tatizo la mawasiliano. Awali, alikuwa amepanga mtoto wake Kanumba akazikiwe Mwanza kwa babu yake ndiyo maana hakufika mapema msibani.   “Nilikuwa nimepanga apitishwe hapa kwangu Shinyanga aagwe, halafu tumpeleke Mwanza kwa babu yake kumzika huko lakini alipokuja mama yake alinishauri kuwa huko kutakuwa na nafasi ndogo kwa sababu watu ni wengi pia alikuwa na marafiki wengi, wengine wa kutoka nje ya nchi kwa hiyo alinishawishi na tukakubaliana kumzika Dar es Salaam,” alisema.

Pia alikanusha uvumi kuwa hajafika msibani kwa kuwa walikuwa na ugomvi na marehemu akisema walishamaliza tofauti zao. Alisema anatarajia kufika leo usiku tayari kushiriki mazishi hayo.

Wabunge  kilio Jana, baadhi ya wabunge waliofika nyumbani kwa marehemu Kanumba waliangua vilio wakati walipotoa salamu zao za rambirambi.

Mbunge wa Viti Maalumu, Martha Mlata hakuzungumza na badala yake aliimba kipande cha wimbo uliozungumzia kifo na maneno ya wimbo huo yalionekana kuwagusa wafiwa na kusababisha vilio kuanza upya huku baadhi wakipoteza fahamu.

Mbunge mwingine, Neema Mwinyimgaya aliongeza majonzi masibani hapo alipounganisha msiba huo na wa mama yake… “Mama yangu amefariki miezi mitatu iliyopita, huko uliko mama, nakuomba umpokee kijana mwenzetu,” alisema mbunge huyo na kushindwa kuendelea.

Wabunge wengine waliohudhuria msiba huo ni Ismail Aden Rage (Tabora Mjini), Aboud Juma (Kibaha Vijijini), Mussa Azan Zungu (Ilala), Abbas Mtemvu (Temeke), Peter Serukamba (Kigoma Mjini) na Ritha Kabati (Viti Maalumu).

 Kova na mchango wa Kanumba Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema anakumbuka mchango wa Kanumba katika kuzuia uhalifu jijini.

“Tulishirikiana naye pamoja na wasanii wengine kuandaa bonanza maalumu ambalo lilidhamiria kukabiliana na uhalifu hapa jijini na kwa kweli mchakato ule ulifanikiwa kwani uhalifu ulipungua kwa kiasi kikubwa” alisema Kova.

“Kifo chake kimekuwa cha ghafla mno na nafikiri kujiweka tayari (kiimani) ni jambo ambalo kila mmoja anatakiwa kuwa makini nalo katika maisha yake,” alisema Kova.

Ratiba ya mazishi

2:30 - Msafara kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia Barabara ya Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi hadi Viwanja vya Leaders Club.

3:30 - Misa ya kumuombea na salamu mbalimbali.

6:00 – Kuaga

9:00 - Kuelekea Makaburi ya Kinondoni kupitia Barabara ya Tunisia


Share:

Apr 7, 2012

TOKA MOYONI IMENIUMA SANA!!

Sometimes unaweza ukakufuru na kutamani afe mtu fulani na aliyekufa akabaki,kutokana na mapenzi yako kwake ila aliyeumba ndiye kila kitu anaamua amchukue nani na muda gani,ukiangalia sana wale wazuri mara nyingi wanakuwa na uhai mdogo ila wale pasua wanaishi miaka miiingi ila siri anaijua Allah!

 Kiukweli nimeumizwa sana na kifo cha Kanumba,sababu ya mapenzi yangu kwake ila sina la kusema zaidi ya kumuombea alale mahala pema peponi!!
 Amefanya mengi mazuri na kusaidia wengi,mimi kwa Tanzania nilikuwa na wasanii wangu wawili tu wa kiume wasanii hasa JB na marehemu KANUMBA na ilikuwa nawaangalia wao maana huwa hawaharibu na sanaa kwao ipo kwenye damu yaani kama kipaji kipaji hasa!!
 Hakuna ama akitokea hawezi kuwa kama yeye!!
 Pumzika kwa amani mpendwa!!

 Alikweza kuwainua watoto wengi na huyu mmojawapo!!
Atazikwa jumanne katika makaburi ya kinondoni!!
Share:

Mar 26, 2012

WADAU SAMAHANI...

Kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu na umuhimu wa hii kitu kwenu tumeshindwa kuimaliza kurekebisha hii blog on time hivyo chochote ambacho mtakiona kipo tofauti na hii blog ni katika jitihada za kuboresha na soon itakuwa vizuri zaidi katika muonekano mpya na bora zaidi.
Unaweza kushiriki nasi kwa chochote ambacho unadhani tunaweza kufanya pamoja kupitia hii blog na mengineyo pia kama unahitaji huduma  yeyote katika kipindi hiki waweza wasiliana na muhusika kama si wahusika kwa njia zifuatazo: Kwa no.+255 659161111
Kwa email:mustaphamadish@gmail.com
Popote ulipo tupo nawe.
Ahsante n Karibu sana.
Share:

Mar 21, 2012

PATA KILICHO BORA!!

Wengi wanashida ya kupata Installer wenye uwezo na huduma bora!!
Hii ndo solution yenu!!
Kama wewe ni mmiliki wa Hotel ama unataka kujenga Hotel ama zile nyumba za wenyeji na hujui wapi utapata mafundi wenye uzoefu na kutoa ushauri kabla ya kufungiwa Channel unazotaka na kwa wakati!!
Huku bei ikiwa nafuu ambayo utaimudu kulipa huku huduma ikiwa ni ya kiwango cha kimataifa!!
Tunatoa huduma kisasa na kwa wakati tukizingatia ubora na matakwa ya mteja!!
Kwa maelezo zaidi unaweza wasiliana nasi kwa:
+255 732 575 718/716 899 155
mminstallers@ymail.com
Share:

Mar 17, 2012

FUFUA DISH LAKO LEO!!!

Aliyebahatika kufufua Dish lake!!
Nimegudua kuna Dish nyingi katika nyumba nyingi ambazo hazifanyi kazi zimekaa tu kama uchafu ama urembo!!
yanini kukaa na kitu kisicho na manufaa!!??

Share:

Jan 10, 2012

LOCAL CHANNELS ZATULIA KWENYE FUTI 6!!


Baada ya kusumbua muda mrefu hatimae Channels za Tanzania zote zilizopo kwenye Satellite zatulia!
Tatizo ilikuwa kama zinatulia za V za H zitasumbua na Zikitulia za H za V zitasumbua,tatizo hili huwa linatokea mara kwa mara na wala sitaki kuamimni kama ndio limeshakuwa limefika kikomo kwa ushauri tu ikiwa unataka Local channels kupitia Dish ukinunua la futi 8 itakuwa unapata uhakika wa kile ukitakacho kwasababu hata zikiwa zinasumbua kwenye futi 8 unaendelea kula raha!!
Hata channels ambazo awali zilipotea nazo zimerejea kama Mozambique n.k kwa LNB c band hiyo hiyo ya Local channels.
Pia unaweza ukapata za kenya kama KBC n.k. kwa kutumia KU lbn!!
Share:

Jan 3, 2012

FREE CHANNELS





Kwenye Dish ndogo kuna channels nyingi za bure,inategemea na wewe unahitaji channels za vipi!!
Lakini kwenye Dish ndogo hupati channels hata moja ya Tanzania.
Kwa maelezo zaidi usisite kuuliza!!
Share:

Oct 18, 2011

Dish thamani yake itabaki pale pale!!

Popote ulipo na popote utakapo unafunga.


Uzuri wa Satellite Dish Antenna ni popote ulipo ama utakapoamua kuweka makazi ukilifunga utakacho kuona utaona ikiwa clear bila chenga,Dish inakaa popote na Signal inaingia lakini lisikingwe ili kupata Satellite husika hii inamaana Dish huwezi kufunga chumbani!!
Kwa kuongeze ukifunga Dish huwezi muona mwanao wakati anaenda shule maana kuna maswali mengi tunakumbana nayo,huko mitaani watu wanadanganyana ya kuwa ukifunga Dish kama nyumba ya pili choo chao vile vya uswazi unaweza ukamuona!!

Jamani jamani sio kweli hiyo ni kazi ya CCTV Camera!!!
Share:

Aug 31, 2011

Savvanah Bar & Restaurant

In Quality centre Dar es salaam....!!!
Mpaka sasa najivunia kuwa na watu ambao wanaheshimu uwepo wangu,wanathamini mchango wangu na mengineyo mazuri kama hayo,hii imepelekea leo kupewa shavu palee kwenye jengo jipya kabisa la Quality centre lililop pugu road,hapa ndani pana kitu kipya pia kinaitwa Nivvanah bar & restaurant...!!
Hapa tenda ilikuwa ya wenzangu ambao walikuwa wanafunzi wangu na wao ndo waliosababisha mimi kuhitajika hapo kwenda kutoa ambacho nilistahili kukitoa na mwisho wa yoote ikawa kama ambavyo utapata fursa kutembelea na kujionea..!!
Kuna channels za Local na DSTV zaidi ya yote kumepambwa na flat screen ni hayo tu kwa leooo...!!!
Share:

Aug 8, 2011

DSTV offer imeisha..!!

Ilikuwa kama utani na kuacha watu wakajiuliza hee DSTV kunani tena ama ndo wameishiwa,ama wameteteleka kwa sababu ya STAR TIMES...!!!??
Baada ya kutoa bonge la offer kwa 89000/= uliweza kupata full installations..!!
Watu wakajisahau na wengine wakiamini wataendelea kushuka ndipo wao watakapofunga ila mambo yakawa ndivyo sivyo,offer imeisha na wengine wakiitamani hata ile bei ya 89000/= ambayo muda wake umeshaisha..!!
Jamani labda kama itakuwa mmepoteza umakini ni kwamba Multichoice ni kampuni kubwa na ipo serious na kazi zaidi ya yote wanajua wakifanyacho na hata burudani zao za ukweli na ndio maana hata wateja zao ni watu makini na ambao wapo up to date..!!

Share:

Aug 4, 2011

CHANNELS ZA TANZANIA KWENYE DISH..!!




 Swali ambalo nakumbana nalo kila kukicha ya kuwa channel gani na ngapi za Tanzania zinapatikana kwenye S.Dish na kwanini nyengine hazipatikani? huku wengine wakidhani channels zote za Tanzania zinapatikana kwenye S.Dish..!!
Zaidi ya yote kuna ambao mpaka leo hii wanaamini ya kuwa ukifunga S.Dish Antenna hata zile channel ambazo zinatumia Antenna zitakuwa hazina chenga kwa sababu karibu na Antenna hiyo kuna Dish...!!
Channels za Tanzania ambazo zinapatikana kwenye Dish ni zile tu zinazotumia Satellite kurusha matangazo yao mfano:-ITV,CAPITAL,EATV,AGAPE,CHANNEL 10,STAR TV na TBC1.
Pia hakuna ufundi wa kufanya nyengine zionekane kwenye Dish mpaka wahusika watakapoamua kujiunga na Satellite.
Uzuri wa kutumia Dish ni kwamba hata nje ya nchi channel husika inaonekana kwa kutumia dish lakini kama utatumia Transmetter kurusha matangazo itakuwa ni Tanzania tu tena wala si nchi nzima sehemu chache tu za nchi..!!
Hivyo kuna ulazima wa channel zote za Tanzania kujiunga na Satellite kurusha matangazo yao,hii ni kwa faida yao katika kujitangaza zaidi maana itakuwa inaonwa na watu wengi zaidi..!!
C2C,DTV,CTN,TV TUMAINI,CLOUDS.
Hizi hazipo kwenye Satellite hivyo hazipatikani kwenye Dish.
Share:

Jul 14, 2011

MAPIPA COMMISSION AGENCY

Pesa si mbaya ila matumizi ndio ambayo mabaya na hii ndio 1 kati ya matumizi mazuri ya pesa,japo yale mabaya hata wakati unafanya unaamini ni mazuri kwako..!!
Nilikuwa sehemu 1 wanapaita Magomeni Mapipa kuna yard mpya ya kuuza magari imefunguliwa inaitwa MAPIPA COMMISION AGENCY jamaa hawa wanauza gari aina zote mzigo unatoka moja kwa moja toka Japan na bei zao pia ni za kawaida sana..!!
Hapa bana nikawafungia dish mbili za KU (ndogo) lengo ni kuona DSTV na Channels za bure za MBC na lengo likatimia na mambo yakawa kama ambavyo pesa ilitumika kutaka mazuri ndivyo walivyoyapata..!!
Zamani banaa ndo ilikuwa mtaani ama nyumba ikifungwa dish wao wanaume lakini si sasa kwani bei ni za kawaida tu isipokuwa ilikuwa imani za watu tu,kama vipi tugongee nawe uzunguke dunia kama ambavyo wenzio wanavyozunguka wakiwa na TV zao majumbani..!
Share:

Jul 8, 2011

Somewhere in Tabata..!!

Haya ndio kati ya mambo yanayotufanya tuwe bize na heshima iwepo katika jamii na maisha yaweze kwenda mbele..!!
Hii ni sehemu moja wanapaita Tabata jijini Dar es salaam,kilichofanyika ni kuinstall DSTV katika vyumba vyote nyuma nzima pamoja na Local channels,zilizo kwenye Dish na zilizo kwenye Antenna kisha tukachukua vilivyo vyetu mwendo kijumba kinachofuata..!!
Share:

Jul 3, 2011

Tupo pamoja ila Email ni nyingi sana na zote nitazijibu..!!

C kwamba nimewapotezea wadau wangu laa hasha,ila kazi ni nyingi na utulivu unakuwa mdogo sana,yote ni ninyi mnaonifanya mimi niwe bize hivyo nathamini sana uwepo wenu hivyo wote mtapata kile mnachotaka ijapokuwa inaweza ikawa si kwa muda ule utakao ila ukiwa mvumilivu tatizo lako hapa ndipo kwenye solution.
Pamoja sana.
Mustapha MaDish.
Share:

Jun 20, 2011

TUSIUCHUKULIE POA UKIMWI..!!


 Kwa mtazamo wangu kutokana na research ndogo niliyoifanya inaonyesha kwa sasa swala la gonjwa la ukimwi si kama ilivyokuwa kama miaka ya nyuma na kadri siku zinavyozidi kwenda watu wanazidi kuchukulia poa na kuona kama  mtu kuugua mafua na maisha kuendelea kama kawa..!!
Nimetumia neno kuchukulia poa kwasababu katika watu ambao nawakusudia zaidi ni vijana ijapokuwa wote nataka twende sawa ila kwa vijana ni too much..!!
Leo hii NGONO imekuwa ndio inawatumikisha sana watu,utakuta watu wapo bize sana kwa ajili ya kufanya NGONO.wanatafuta pesa,wanaongopa,wanatumia muda mwingi sana na kufanya kila linalowezekana ili tu mwisho wa siku wafanikishe kufanya NGONO.
Siku hizi idadi ya walio wengi wanapenda sana ngono na upendo wa dhati unakuja baada ya kufanya ngono na hii inasababisha idadi ya wanaooa/kuolewa hupungua kila kukicha maana inakuwa ngumu kudumu kwa kutokupata kile ambacho either alikitegemea kabla ama alitaka tu kuona kiundani inakuwa aje..?
Mapenzi yanadumu miezi kadhaa tu then wanaachana ama mtu mmoja anakuwa na zaidi ya mpenzi mmoja na ndo pabaya sana hapa..
Unayemuamini ana wapenzi wawili nawe ukiwa wa tatu,hapo hapo nawe unakiacha unayemuamini unao wengine wa kuzugia pengine watatu,inaweza ikawa mpenzi wako unayemuamini hayuko poa kifedha hivyo kuna wa kukununulia vocha na matumizi mengine huku ukiwalipa kwa penzi lako lakini huna future nao,uliye na future nae ndiye huyo mwenye wapenzi wawili wewe ukiwa wa tatu na yaweza kuwa mmoja tu kati ya hao ndo unatumia kinga tena pia pengine siku za mwanzo mwanzo tu na mkishazoeana inakuwa mpango....!!
Hapa UKIMWI utatukosa ??
Kama ulikuwa hujui automatically kama utamsaliti mpenzi wako jua ya kuwa nawe atakusaliti ama anakusaliti...!!
Jamani,jamani UKIMWI upo tusijisahaulishe kama vipi tuwe na mmoja na yakishindikana hayo TUVAE..!!
Ni hayo tu kwa leo toka kwangu kuja kwenu.
Mustapha E. Hanya
Share:

Jun 17, 2011

CHANNEL ZINAZOPATIKANA EASY TV..!!

Ntawaletea idadi ya channel zote zinazopatikana kwenye ving'amuzi kutokana na maombi yenu ili muweze kuelewa na kufanya maamuzi yaliyo sahihi na leo hii naanza na EASY TV.
EASY TV ina jumla ya channels 32 ila zinazoonyesha ni 30 tu.
Movie 1
Movie 2
Movie3
Movie Arabic
Aljazeerah
CNN
BBC
CCTV4
UBC
Citizen
TBC 1
Star TV
Channel 10
Capital
EATV
TVZ
ITV
Clouds TV
EWTN/TV Tumaini
Mliman TV
Emmanuel TV
Peace TV
Channel V
Xing kong
Ph'x China
JSC document
JSC sport
MTV
Child
Ila kiukweli mfumo wa ving'amuzi wanaujua wenyewe maana channel wanazouza nyingi ni za FREE TO AIR hivyo satellite husika wakihama channel inapotea,hivyo mpaka baada muda ndipo wanairejesha na pengine isilejee tena..!!
Pia wanaweza kuongeza channel pale wanapoona channel ipo ipo tu na inafaa kutazamwa na watanzania wanaibandika..!!
Kwenye easy tv nimemalizia hapa next time ntahamia kwenye STAR TIMES na ntamalizia na TING ni hayo tu kwa leo n nawatakia week end njema wadau..!!

Share:

Jun 6, 2011

Transit Motel Airport

 Baada ya kusababisha Transit Motel ya ukonga kazi ikahamia Transi Motel ya air port na kazi ikawa ni moja tu kufanya TV zionyeshe kwa uzuri ili mteja aweze kidhi haja yake kwa kile anachotaka kukiona..!!

Nikaanza ingia chumba mpaka chumba na hiki ni chumba kimojawapo kati ya vyote vizuri vilivyopo..!!

 Mpaka hapa nikapita,wanapaita RECEPTION kwa niliowaacha ni mapokezi huwezi ingia mpaka upitia hapa


Hapo tayari kwa matumizi ya wageni kama si wenyeji ili maisha yaendelee huku ukiangalia TV ikiwa clear kabisa,ukipuliziwa na AC na pia ukitaka chakula ama kinywaji chochote unapiga tu simu unaletewa chumbani kama hautahitaji kutoka nje..!!
Nami nikachukua kila kilichochangu mwendo nikachapa..!!



Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita