Call / WhatsApp +255673378129

Jul 1, 2016

KUEPUKA DISH YAKO KUPATA KUTU

Niwe mkweli katika hili usipopata fundi makini uwezekano wa kuepuka hili ni mdogo sana vinginevyo muhusika uwe makini sana na Fundi wako ingawaje mara nyingi muhusika inakuwia vigumu kuona jinsi fundi wako alivyofunga Dish huko juu ya paa!!

Sababu zinazopelekea Dish kupata kutu kwa haraka:-

Sababu zisizoepukika:-

> Ikiwa Dish inafungwa ufukweni.

> Ikiwa Dish ni FAKE.

Sababu zinazoepukika:-

> Kutokuweka vinavyozuia maji kuingia.


Tuone madhara ya kutotumia vinavyozuia maji kuingia ndani na kukosa pa kutokea!
1
Hii ni Stendi ya kubeba Dish,hiki ni kikalio ( Chini ) ambapo kwa kutokufunika juu,imesababisha maji yameingia na kwakuwa hakuna sehemu maalumu ya kutokea maji yanapoingia,yenyewe yakatafuta njia kwa kutafuna kidogo kidogo mpaka kupata njia kama muonavyo!

2
Huu ni mkono wa kushika LNB,upo mfano wa V,mkono huu ni bomba maana yake kati lipo wazi,upande wa mbele inafungwa LNB ambapo inazima maji kuingia na upande wa nyuma kuna ya kukipachika ili kuzuia maji yasiingie kama ilivyoonyeshwa picha namba ( 5 ) kwakuwa yakiingia kinachotokea pale kwenye mkunjo ndipo maji yatajitengenezea njia kama muonavyo hapo juu!
3
Matokeo yake ile V inageuka vipande viwili baada ya kuliwa na kutu!
4
Ufungwaji Dish wa namna hii ndio unaopelekea madhara tuliyoyaona hapo juu kwenye picha ( 1 - 3 ) jinsi maji yalivyosababisha kutu,ambapo kama fundi angetumia vifaa vyote ipasavyo yasingetokea madhara hayo yaliyotokea!
5
Hivi ndivyo unavyopaswa kufunga Dish yako kwa kutumia Plastic cover ili kuzuia maji yasiingia kwenye bomba ya Stend na mkono wa kushika LNB!

Nadhani kwa uchache umeambulia kidogo kwa maelezo zaidi
+255789476655 
NB:Kupiga kuanzia saa 08:30 - 18:00 
Share:

Jun 30, 2016

KUFUNGA DISH NDOGO ( KU DISH INSTALLATION )

Kwakuwa karibu Ving'amuzi vyote Tanzania vinatumia Dish ndogo leo niwape kasomo haka alau mwenye kujaribu na ajaribu atakapopata wasaa!!
Fanya haya ili uweze kufunga Dish ndogo:-

1.Dish Antenna Assembly:
- Unganisha kifaa kimoja kimoja kama karatasi ya maelekezi inavyoonyesha ili kulikamilisha dish lako bila kuacha hata kimoja kwakuwa kila kimoja kina kazi na umuhimu pia.

2.Unganisha stendi yako ya kubeba dish.





3.Angalia sehemu nzuri ya kufunga Dish ili uanze kufunga stendi yako:
- Hakikisha sehemu unayoifunga mbele hakuna miti itakayozuia kupokea signal.
- Sehemu imara itakayoweza kukaa Dish bila kucheza.
- Unashauriwa kuifunga juu ya usawa wa nyuma/jengo ili isipate kuguswa guswa.

4. Funga stendi yako ya dish sehemu ulipoona panafaa.
5. Funga Dish lako kwenye stendi kwa kulielekezea Satellite uliyoikusudia ( Muelekeo wa king'amuzi husika )
6. Unganisha Coaxial cable ( Signal cable ) kwenye king'amuzi chako kwa nyuma sehemu iliyoandikwa LNB IN kisha unganisha kwenye either kwenye Dish sehemu ya LNB ama kama utakuwa na kitafuta signal (Signal  Finder ),kama utatumia Finder lazima uwe na Test cable ( Kipande cha cable ambacho utachomeka toka kwenye finder mpaka kwenye dish ( LNB ) - Nimetoa mfano wa Finder hii kwakuwa ni rahisi kupatikana na hata bei yake ni ya kawaida ila kuna finder nyengine hazihitaji Test cale.
7. Upo tayari kwa kuanza kutafuta signal. Jinsi ya kutafuta signal ntawaletea somo hilo katika post nyengine!
Tuangalie kwenye video hapo chini!



+255 789 476 655
Share:

Jun 16, 2016

UNAANGALIAJE MPIRA BILA KULIPIA/MALIPO NAFUU!


Wadau/Wateja wa ving'amuzi wakubwa ni wapenzi wa mpira hii ilikuwa hata kabla Tanzania haijaingia katika makubaliano ya kati ya zile nchi zilizoachana na mfumo wa Analogue tv na kuingia katika mfumo wa Digital tv..Hii inatokana na wapenzi wa mpira kutaka kupata mpira kwa njia yeyote ile,hivyo imekuwa kama ndo biashara ikiwa ni mdau wa ving'amuzi ili ufanye mauzo mazuri ni lazima ujue namna ya kupata kuonyesha mpira hii imepelekea kina sisi kuchangamkia fulsa kwanza kutafuta njia za kupatikana kwa channels zinazoonyesha mpira bure/kwa bei nafuu kwa udi na uvumba ili kuweza kuuza kwa wahitaji ukiachilia kampuni iliyo na idhini ya kuonyesha mpira Multichoice ( DStv ) ambayo hakuna mdau yeyote wa mpira ambaye halalamikii bei za DStv hususani Packeges za Sports,hii inapelekea kila kukicha kubuniwa njia za kuibia channels za DStv!
Post hii itakamilika hivi karibuni karibu....
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita