Call / WhatsApp +255673378129

Dec 14, 2017

UTAJUAJE KAMA TV YAKO INA KING'AMUZI NDANI?


Swali la wengi kwasasa ni hili kutokana na ukweli kwamba uondoshwaji wa local channels kwa baadhi ya Visimbuzi imekuwa kama janga hivi.. Sasa niwape namna ya kujua jinsi gani ya kupata local channels kupitia tv ikiwa ina kisimbuzi ndani, inaweza ukatumia Antenna ama Dish inategemea na uwezo wa tv:-
Utajuaje kama tv yako ina kisimbuzi ndani?
  • Ingia kwenye INPUTs inategemea na brand, zipo ambazo zinatumia SOURCE, INPUT n.k unabonyeza na itakuletea orodha ya input zote mfano:-
AV
HDMI1
VGA
USB
ATV
DTV
Ukiona ina DTV ujue ina kisimbuzi.
  • Njia nyengine unachukua remote yako unabonyesha kwenye SETTING unaenda kwenye SEARCH hii nayo inategemea na tv, tv nyengine hutumia tune n.k hapa unaweza ukaweka AUTO SEARCH itakuletea Analogue tv na Digital tv ikikuletea hizo chaguo ujue tv yako ina kisimbuzi ila kama itakuletea Analogue tv pekee ujue haina kisimuzi..
 Ikiwa tv yako ina DTV maana yake inapokea matangazo ya Digital hivyo unapaswa kutafuta Antenna na kuchomeka muelekea wa Startimes/Ting ama Continental na kufanya search kama kila kitu kikiwa sawa channels zitaingia..
Kuna DVB T1/ T2 hii ni kwa ajili ya antenna.
Kuna DVB S1/ S2 hii kwa ajili ya dish.

Insta @mustaphamadish
Whatsapp+255784378129

Share:

1 Unasemaje..??:

Anonymous said...

Mbona huku kwetu hamjapita nasi tuna maswali yetu tunataka mkurugenzi atujibu.. kwanini hamtoi offer mwisho wa mwaka kwa wateja kama ilivyo ving'amuzi vyengine

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita