Call / WhatsApp +255673378129

Jun 18, 2015

LOADING...


Nilichogundua karibu ving'amuzi vyote vina mapungufu na hii inatokana na kujisahau,wafanyakazi kufanyakazi bila juhudi binafsi wanafanya ile bora liende mwisho wa mwezi tukinge,pia makampuni yenyewe husika hayajajipanga katika baadhi ya mambo ili kukabiliana na ushindani uliopo.
Kwa kulitambua hilo tunakuja kuwa mfano kwa makampuni yote ya ving'amuzi ili kuleta changamoto kwa makampuni yaliyolala kuweza kuamka na kutoa huduma stahiki kwa wateja wao..
Tunakuja...
Kaa tayari kutupokea..
Share:

Jun 16, 2015

BEI MPYA YA MALIPO YA MWEZI AZAM TV


Burudani kwa wote..
Kwa mujibu wa Azam tv bei za vifurushi zimepanda kutokana na ungezeko la kodi,
hivyo kile kifurushi cha tsh 10,000/= kimekuwa tsh 12,000/=
kifurushi cha 15,000/= kimekuwa tsh 20,000/=
na kifurushi cha 20,000/= kimekuwa tsh 30,000/=
Pia siku za usoni kinakuja kifurushi kipya ambacho kitakuwa na channels za india tu,
hivyo ili uzione channel za india itakulazimu ulipie kifurushi hicho kipya lakini kwa kipindi hiki ni bure mpaka hapo ambapo itatangazwa.
Kujua channel zilizopo Bofya Hapa
Mambo yote ya kiufundi Azam tv piga : +255789476655

Share:

Jun 10, 2015

VIFURUSHI VYA TING | TING PACKAGES


Hivi ndivyo vifurushi vilivyopo na bei zake kwenye king'amuzi cha Ting kwenye Antenna na kwenye Dish!
1.REGULAR PACKAGE
Inachannel 12+ safi
Malipo ni Tsh 11,000/=
Kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
Package hii ni kwenye Antenna tu!
2.CLASSIC PACKAGE
Ina channel 30+ safi
Malipo ni Tsh 22,000/=
Kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
Package hii ni kwenye Antennatu!
1A.REGULAR PACKAGE
Ina channel 25+ safi!
Malipo ni Tsh 16,000/=
Kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
Package hii ni kwenye Dish tu!
2A.CLASSIC PACKAGE
Ina channel 50+ safi!
Malipo ni Tsh 24,000/=
Kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
Package hii ni kwenye Dish tu!
Kwa maelezo Zaidi piga +255789476655

Share:

Jun 9, 2015

KUNUNUA KING'AMUZI CHA ZUKU TV TANZANIA

Remote ya Zuku
Ili kutoa fulsa ya kila mtu aweze kununua kinga'amuzi cha Zuku Tv imeonelea kushusha bei,ambapo sasa ili kununua zuku itakulazimu kulipia Tsh 88,000 tu,badala ya Tsh 95,000/= ila hii inakuwa bila ufundi.
Ili ufungiwe itakulazimu kulipia Tsh 30,000 tu,pesa hii itakulinda ndani ya miezi mitatu kwa lolote likitokea fundi atahusika bila gharama yeyote ya ziada.
Baada ya hapo unachagua Kifurushi kati ya vifurushi vifuatavyo,ingawaje kwa mwezi wa kwanza unapata kifurushi bure!

1-ZUKU SMART PACK PACKAGE
Ina channel 36 safi.
Malipo ni Tsh 8,999
kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

2-ZUKU SMART PLUS PACKAGE
Ina channel 40 safi.
Malipo ni Tsh 13,000
 kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
3-ZUKU CLASSIC PACKAGE
Ina channel 69 safi.
Malipo ni Tsh 18,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

4-ZUKU PREMIUM PACKAGE
Ina channel 98 safi.
Malipo ni Tsh 25,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

5-ZUKU ASIA PACKAGE
Ina channel 26 safi.
Malipo ni Tsh 24,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
ZINGATIA:Muda wakupiga simu ni saa 08:00 - saa 20:00 usiku.

Ili Kununua | Kupata Mafundi | Msaada 
Piga +255714973797
Share:

May 18, 2015

KWANINI TUMELAZIMIKA KUIGIA DIGITAL NA KUACHANA NA ANALOGUE?


Mabadiliko katika mfumo wa utangazaji kutoka mfumo wa analojia kwenda katika mfumo wa dijitali ni utaratibu ambao unaendelea ulimwenguni kote. Mabadiliko haya yanatokana na makubaliano ya nchi wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa lenye dhamana ya masuala ya mawasiliano yaani International Telecommucations Union yaliyofanyika mwaka 2005 huko Geneva, Uswisi. Makubaliano ya nchi wanachama ni kuzima kabisa matangazo katika mfumo wa analojia na kutumia mfumo wa utangazaji wa dijitali ifikapo tarehe 17 Juni 2015. 

Ili kuhakikisha mabadiliko haya yanafanyika kwa ufanisi, tija na pia kutoa muda wa kutosha wa kutekeleza mabadiliko haya, mwaka 2005 Serikali ilianza mchakato wa uhamaji kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda dijitali ambao ulihusisha wadau wote, wakiwemo wamiliki wa vyombo vya habari na vituo vya utangazaji wa televisheni, hatua kwa hatua, hadi kuridhia ratiba nzima ya uzimaji wa mitambo ya analojia. Kwa kifupi mchakato wa uhamaji ulipitia hatua zifuatazo:

Mwaka 2005:   Waraka wa kwanza wa mashauriano (consultative document) kuhusu umuhimu na faida za kuhama kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda dijitali ulitayarishwa na kusambazwa kwa wadau wote;

Mwaka 2006:   Waraka wa pili wa mashauriano na mapendekezo ya muundo wa leseni kwenye mfumo wa utangazaji wa teknolojia ya dijitali ulitayarishwa na kusambazwa kwa wadau wote;

Mwaka 2007:   Kamati ya kiufundi inayoshughulikia uhamaji kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda dijitali iliundwa;

Mwaka 2007:   Mkutano mkuu uliojumuisha vituo vyote vya utangazaji nchini ulifanyika Bagamoyo kupitisha maazimio ya mfumo wa leseni za utangazaji utakaotumika kwenye mfumo wa dijitali;

Mwaka 2010:   Kampuni tatu (3) zilipewa leseni za ujenzi wa miundombinu ya utangazaji ya dijitali. Kampuni tatu zilizopewa leseni za kusambaza matangazo ya dijitali ni Agape Associates Limited, Basic Transmission Limited, na Star Media (T) Limited. Kampuni hizo zilipewa leseni baada ya kuthibitisha kuwa zina uwezo wa kujenga miundombinu ya kurushia matangazo katika mfumo wa dijitali;

Mwaka 2010:   Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu Mabadiliko ya Utangazaji toka mfumo wa analojia kwenda dijitali iliundwa. Kamati hii hukutana kila baada ya miezi mitatu kutathmini maendeleo ya ubadilishaji wa mfumo wa utangazaji;

Mwaka 2011:   Kampeni ya Kitaifa ya kuelimisha umma kuhusu mabadiliko ya mfumo wa utangazaji ilizinduliwa rasmi na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa Tanzania rasmi nchi nzima mwisho wa kutumia mfumo wa Analogue ni tarehe 31/12/2014 saa 23;59.
Tukahamia mfumo wa Digital,ambao huu wa ving'amuzi tulionao ijapokuwa ilikuwa mwisho ni tarehe 17/06/2015,kuhama mapema ni namna ya kuangalia je kuna changamoto gani na vipi wahusika wanakabiliana nazo.

+255789476655
Share:

May 11, 2015

VING'AMUZI VINAVYOCHUANA | AZAM TV & DSTV | KIPI NI ZAIDI!?


Dstv ni wakongwe hii haina ubishi,ila ukongwe wa dstv haina maana kuwa hakuna king'amuzi ambacho kinaweza kuja na kufanya vizuri zaidi yake,hii inatokana na kwanza kujua mahitaji ya watazamaji kwa ujumla na kuwatimizia kile wanachokihitaji,unafuu wa bei ukizingatiwa.
Azam tv ni king'amuzi kipya kati ya vyote unavyoviona ila ndio king'amuzi kinachokimbizana na wakongwe,kwanini? kwasababu wameangalia watazamaji wanataka nini na kwa unafuu pia..Ingawaje Azam tv haijakidhi mahitaji wa wadau kwa 100% lakini alau wameweza kwa ukubwa.
Wadau wengi ni wapenzi wa mpira hivyo Azam tv wamefanikiwa kwa mpira wa Tanzania na Dstv bado anang'ang'ania ukongwe wake kwa mpira wa nje.
Ving'amuzi hivi vina mapungufu yake na kinachowakera wengi ni haya hapa:-

MAPUNGUFU YA DSTV
-Kubwa linalolalamikiwa na watanzania wengi ni bei kuwa juu,nikimaanisha malipo ya mwezi na hii inachangia na mtindo unaotumika wa kutumia $ badala ya Tsh.
Madhara ya kuwa bei juu kumefanya wadau watafute kila aina ya njia kuona wanapata uhondo wa dstv ila kwa njia isiyo rasmi,na hii inapelekea kupunguza walipaji halali wa malipo ya mwezi.
-Wana local channel,lakini malipo ya mwezi yanapokata hawaziachi zikawa bure.
Hayo ni mapungufu makubwa kwa Dstv.

MAPUNGUFU YA AZAM TV
-System wanayotumia kushindwa kutambua malipo ya mwezi wanayolipia wateja na kufunguka badala yake ukilipia kifurushi ukipendacho mpaka upige simu,hii imekuwa kero kwa wateja wengi wa azam tv,mteja anakaa mpaka wiki mbili na ikitokea hapigi simu unapita mwezi pasi kuona kile kifurushi alicholipia.
-Mawakala na wauzaji wengine wasio mawakala kuuza bei tofauti na bei sahihi.Hii sio tu mikoani ijapokuwa mikoani lawama hizi ni kubwa lakini hata hapa Dar es salaam wapo wanaouza bei juu tofauti na matangazo yalivyo.
-Picha kupotea kipindi cha mvua,king'amuzi ambacho kinaongoza kwa kupotea signal wakati wa mvua ndogo tu,hii ni kero nyengine kubwa kwa wateja wa Azam tv,kitaalamu hii inatokana na signal kuwa chini hivyo ni jukumu la Azam tv kuongeza signal badala ya 60 zifike alau 80 lakini kinachotakiwa mfikishe 100.
Hayo ni mapungufu makubwa kwa Azam tv.
TOFAUTI KUBWA KATI YA DSTV & AZAM TV
Dstv ana huduma zaidi ya moja kama:-
Extra view-Inakuwezesha kuona channel mbili tofauti kwa tv mbili tofauti kwa a/c moja.
Explora-Inakupa fulsa ya kurecodi saa 150 na mengineyo.
Umiliki na utofauti wa channel.
Dstv inaonyesha mpira wa nje na Azam tv mpira wa ndani.

MUSTAPHA MADISH | +255789476655 | mustaphamadish@gmail.com
Share:

May 1, 2015

STAR TV | AZAM TV | PAMOJA SASA

Awali ilikuwa ili kupata Star tv kwenye king'amuzi cha Azam ilikuwa ni fundi na ufundi wetu tu,kwani ilikuwa tunafunga satellite mbili kwa wakati mmoja ila baadae wenye mali yao hapo Satellite ya Amos 5 wakafanya ya kufanya.
Baada ya vuta nikuvute hatimae sasa Star tv imeungana na Azam tv,hivyo jambo hili limepelekea kila mmiliki wa king'amuzi cha Azam alipokee kwa furaha,huku wale ambao walikuwa wanasita kujiunga na Azam kwasababu hakuna Star tv huu ndo wakati wenu labda mseme lengine.

+255789476655 | HUDUMA ZA AZAM TV
Share:

Apr 27, 2015

MVUA NA VING'AMUZI VYETU


Kwa kawaida mvua inapokuwa inanyesha watu wengi nami nikiwa mmojawapo huwa mapenzi yapo kukaa sehemu tulivu kama panaruhusu unaangalia tv,iwe ni movie ama vyovyote vile ijapokuwa mimi mapenzi yangu kuangalia movie...
Ikiwa una king'amuzi chako na unataka kuangalia huku ukipisha mvua ifanye yake kisha uendelee na ratiba zako..King'amuzi nacho kinagoma kutoa picha..Mvua inaponyesha ving'amuzi vinavyotumia dish ndogo huwa vinaelemewa ila inapokata mvua navyo vinaonyesha picha kama kawaida..Unadhani ni kwanini vinaelemewa? Fuatana nami..






Share:

Apr 14, 2015

VING'AMUZI VYA ANTENNA


EASY TV
King'amuzi cha kwanza cha antenna ambacho mpaka sasa kipo ila kiukweli kama wanasua sua na kujikuta kila kukicha wanapoteza wateja badala ya kuongeza wateja.
Sababu ya king'amuzi hiki kupoteza wateja kila kukicha ni kutokana kukosa kuwapa uhakika wateja wao na wale wateja wapya,ambapo hata huduma zitolewazo kama zina usiri matokeo yake kimekuwa king'amuzi ambacho hakijulikani na watanzania wengi,pia kingine kinachowakimbiza wateja ni namna channel zinavyopungua kila kukicha ijapokuwa kuna ambazo zinaongezeka!
Pamoja na hayo yote malipo ya mwezi ni  tsh 10,000/= toka walipoanza mpaka sasa.


STARTIMES
Katika zile mbio za kuingia katika mfumo wa digital,ndipo kikazaliwa king'amuzi hiki ambapo kuna ushirikiano kati ya tanzania na china,hivyo kwa lugha nyepesi hiki ndicho king'amuzi cha TBC na hiki ndicho king'amuzi pekee unachoweza kupata TBC2.
Ingawaje king'amuzi hiki kilianza katika mfumo wa transmeter kwa lugha nyepesi kutumia antenna lakini sasa wameingia kwenye mfumo wa satellite pia mfumo wa dish hivyo kuwa ni kati ya vile ving'amuzi vichache vinavyotumia antenna na dish pia ila kwa decoder tofauti.

TING
Hiki king'amuzi ni mali ya taasisi ya dini,sababu hiyo imepelekea kuwa na idadi ya channel nyingi za dini zikiwemo za ndani na nje ya nchi.
Ingawaje nacho kilianza na antenna lakini baadae kikaongeza kutumia mfumo wa dish,hivyo kuna decoder aina mbili za antenna na za dish pia.

DIGITEK
Kulikuwa na  ile kila kampuni inayomiliki vituo vya tv kutaka kumiliki ving'amuzi vyao,na hii ilipelekea watanzania kuongea saana kwamba tutanunua ving'amuzi vingapi ila kuna baadhi ya makampuni wakaachana na habari hiyo ila makampuni mengine yakatimiza azma yao na katika kuthibitisha hili kikazaliwa king'amuzi hiki,
Ambacho walifanya hawakuwa na malipo ya mwezi,ilikuwa ukinunua wewe ni kutumia tu ambapo mpaka sasa.
King'amuzi hiki kikapotea,vilikuwa vimeisha huku fununu zikiwa wanaleta ving'amuzi vya kutumia satellite kama vilivyo ving'amuzi vyengine,kweli hatimae wakatoa decoder zenye uwezo wa kusoma antenna na dish.

CONTINENTAL
Katika kule kila kampuni kumiliki king'amuzi chake,star tv wameingia kwenye orodha hiyo kwa kumiliki king'amuzi hiki.Ambapo kumezaa star tv zaidi ya moja kama star bunge,star music na nyenginezo ilihali kuleta tofauti na ving'amuzi vyengine na kuongeza umuhimu kwa watazamaji.
Antenna ilihusika sana huku wakiwa hawana malipo ya mwezi kama digitek,ilifikia hatua wakahitaji kubadili ule mfumo waliokuwa wanautumia katika kurusha matangazo yao hivyo iliwalazimu kupotea hewani huku wateja wao wasijue siku watakayorejea.
Sasa wapo hewani,wapo hewani huku wakiwa wameingia katika ule mfumo uliotazamiwa na wengi ambapo hivi sasa wanatumia Antenna na Dish pia.

VING'AMUZI VYOTE HIVI VINAINGILIANA ANTENNA
Nimejaribu kutumia picha ya antenna moja kwa ving'amuzi vyote kwa kuwa unaweza ukatumia antenna hiyo kwa ving'amuzi vyote bila shida!
Kuna baadhi ya maeneo unaweza ukatumia antenna ya ndani na ukapata picha vizuri tu ila kuna maeneo ni lazima uweke antenna ya nje na bomba lako liwe refu pia.



KUNUNUA KING'AMUZI | MAFUNDI | USHAURI | +255789476655

Share:

Apr 9, 2015

BEI MPYA ZA MALIPO YA MWEZI DSTV

Ikiwa wadau wapo katika kulala na kuomba angalau gharama za malipo ya mwezi zipungua,hali imekuwa tofauti kutokana na gharama za uendeshaji ambapo imepelekea kupanda kwa bei za malipo ya mwezi kwa vifushi vyote vya Dstv kama ifuatavyo:-

BOMBA PACKAGE 
Awali ilkuwa tsh 18,500
Ikabadilika na kuwa tsh 23,500
Ikabadilika tena na kuwa tsh 19,975
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 19,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

FAMILY PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 40,000
Ikabadilika na kuwa  ths 51,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 42,900
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 39,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

COMPACT PACKAGE
 Awali ilkuwa tsh 66,000
Ikabadilika na kuwa  ths 84,500
Ikabadilika tena na kuwa tsh 82,250
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 69,000
kitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

COMPACT PLUS PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 113,000
Ikabadilika na kuwa  ths 147,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 122,500
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 109,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

PREMIUM PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 199,000
Ikabadilika na kuwa  ths 219,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 184,000
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 169,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa


HUDUMA ZA DSTV | MSAADA KIUFUNDI | +255789476655

Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita