Call / WhatsApp +255673378129

Jun 13, 2016

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI KWENYE KING'AMUZI CHAKO


Pata msaada wa haraka na updates za Visimbuzi instagram @mustaphamadish
Hili ni moja kati ya yale ambayo ni kero kwa watumiaji wa ving'amuzi kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha na kukosa sehemu ya kupata maelezo ya kina kama hapa!
Swali la kwanza unatumia king'amuzi gani!?
Ving'amuzi vyote vyenye vifurushi ukilipa kifurushi ambacho si kile ulicholipia mwezi uliopita kama pesa pungufu hakuna picha utakayoiona na ikiwa pesa ni nyingi utaendelea kuona kifurushi kilichoisha,hivyo ili uone kifurushi ambacho umekusudia kutokana na pesa uliyolipa unapaswa kubadili kifurushi kwa kufata mtindo niliouelekeza hapa!
Chagua king'amuzi chako hapo chini ili kupata maelezo ya kina:-
  • Azam tv Bofya Hapa kujua kuhusu jinsi ya kuhama kifurushi!
  • Dstv Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
  • Startimes  Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
  • zuku Bofya Hapa kujua jinsi ya kuhama kifurushi!
Kwa maelezo haya nadhani hakuna usumbufu utakaoupata tena
na  kwa maelezo zaidi no.yetu ni ile ile!
+255 789 476 655

Share:

Jun 10, 2016

SI LAZIMA KUTAFUTA FUNDI

Nilikwishasema na leo narejea tena inapotokea king'amuzi chako hakionyeshi la kufanya kwanza Bofya Hapa ukiona bado huelewi hebu fanya jitihada za kulifikia Dish lako ama Antenna yako!! Sasa kama hii Dish fundi atacharge pesa ya signal wakati ilikuwa ni kukata hayo matawi ya mpapai ama kuukata kabisa!
Ushauri wangu watumiaji wa Ving'amuzi mjiongeze mtuhitaji inapolazimika tu sio kwa kazi kama hizi ambazo wenyewe mnaweza kuzifanya,huwa sijisikii vema kufanya kazi ambayo situmii taaluma yangu mfano wa hii hapa!

Share:

May 15, 2016

JINSI YA KUUNGA COAXIAL CABLE ( SIGNAL CABLE )

Leo nimeonelea tuelekezane jambo hili ambalo limeshakuwa ni tatizo miongoni mwa watumiaji wengi wa ving'amuzi,lengo langu likiwa ni lile lile sote kwa pamoja tuhamie Digital huku tukiwa na ufahamu wa kutosha juu ya ulimwengu huu!
Sio jambo geni kuunga Cable ya Signal,ile Cable inayotoa Signal kutoka kwenye Dish ama Antenna kuleta kwenye king;amuzi chako na kila mtu huwa na sababu yake ya kuunga!
> Sababu zinazopelekea kuungwa kwa Coaxial Cable:-
  • Cable kuwa fupi
  • Cable kuchunika
  • Cable kukatika
Hakuna madhara katika kuunga Cable kikamilifu isipokuwa madhara yanaweza kutokea ikiwa itaungwa ndivyo sivyo,pia inashauriwa kuunga Cable si zaidi ya mara mbili!

A > Uungwaji wa kienyeji usiotakiwa ingawaje unatumiwa na wengi

 No.1

No.2

No.3

Uungwaji huu sio mzuri kiujumla kwakuwa licha ya kuwa na muonekano mbaya pia kuna uhai mdogo wa signal,mbaya zaidi inategemea umeweka wapi muungo huu,ikiwa utaweka kama ilivyo hii picha hapo chini ni dhahili umetengenezea mazingira ya kuingia maji na kupigwa jua hivyo maji yatatengeneza kutu na jua litabandua hiyo gundi hapo hivyo maisha ya Signal huishia hapo.Ingawaje hii wakati mwengine hufanywa na Wateja wenyewe lakini pia kuna mafundi hufanya hivi kusudi huku wakijua kitaaluma hii haipo ni moja kati ya kazi chafu zisizotakiwa.




B > Uungwaji mwengine wa kienyeji usiotakiwa ingawaje unaonekana una nafuu

 No.1

 No.2

 No.3

No.4

Uungwaji huu angalau kimuonekano hauleti picha mbaya na wakati mwengine ni ngumu kuonekana kama umeungwa,uungwaji huu unatofautiana kidogo na wa A huu unahitaji umakini kidogo kwakuwa ukijichanganya kidogo na kusababisha ukagusanisha nyaya hakuna mawasiliano yatakayo pita katika muunganiko huo.Uungaji wa A na B ni kawaida kupunguza signal ikiwa hujaunga vizuri.
NB: muungo A na muungo B unahitaji umakini ili nyaya zisigusane.

SIGNAL QUALITY
Unachopaswa kufanya ni hiki hapa toka kwangu:-

  • Kwanza ni lazima ununue vihusika vifuatavyo

  1. Joint
  2. F connector pic 2
Ambapo thamani yake vyote ni kuanzia 2000 mpaka 3000 ingawaje unaweza ukauziwa hata 10000 inategemea tu unanunua wapi?
  • Chuna Coaxial cable ya vizuri kwa mtindo huu kama inavyoonekana hapo chini
Hakikisha Center conductor haigusani na Outer conductor

Outer conductor unaupindia juu ya jacket kama unavyoona hii picha

Outer conductor inakuja kugusana na Connector utakayoifunga isipokuwa Center conductor haitakiwi igusane na connector
  • Jinsi JOINT inavyofungwa na kufanya kazi






NB:Uungwaji wote wa Cable hakikisha Center conductor haigusani na Outer conductor.

mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita