Call / WhatsApp +255673378129

May 15, 2016

JINSI YA KUUNGA COAXIAL CABLE ( SIGNAL CABLE )

Leo nimeonelea tuelekezane jambo hili ambalo limeshakuwa ni tatizo miongoni mwa watumiaji wengi wa ving'amuzi,lengo langu likiwa ni lile lile sote kwa pamoja tuhamie Digital huku tukiwa na ufahamu wa kutosha juu ya ulimwengu huu!
Sio jambo geni kuunga Cable ya Signal,ile Cable inayotoa Signal kutoka kwenye Dish ama Antenna kuleta kwenye king;amuzi chako na kila mtu huwa na sababu yake ya kuunga!
> Sababu zinazopelekea kuungwa kwa Coaxial Cable:-
  • Cable kuwa fupi
  • Cable kuchunika
  • Cable kukatika
Hakuna madhara katika kuunga Cable kikamilifu isipokuwa madhara yanaweza kutokea ikiwa itaungwa ndivyo sivyo,pia inashauriwa kuunga Cable si zaidi ya mara mbili!

A > Uungwaji wa kienyeji usiotakiwa ingawaje unatumiwa na wengi

 No.1

No.2

No.3

Uungwaji huu sio mzuri kiujumla kwakuwa licha ya kuwa na muonekano mbaya pia kuna uhai mdogo wa signal,mbaya zaidi inategemea umeweka wapi muungo huu,ikiwa utaweka kama ilivyo hii picha hapo chini ni dhahili umetengenezea mazingira ya kuingia maji na kupigwa jua hivyo maji yatatengeneza kutu na jua litabandua hiyo gundi hapo hivyo maisha ya Signal huishia hapo.Ingawaje hii wakati mwengine hufanywa na Wateja wenyewe lakini pia kuna mafundi hufanya hivi kusudi huku wakijua kitaaluma hii haipo ni moja kati ya kazi chafu zisizotakiwa.




B > Uungwaji mwengine wa kienyeji usiotakiwa ingawaje unaonekana una nafuu

 No.1

 No.2

 No.3

No.4

Uungwaji huu angalau kimuonekano hauleti picha mbaya na wakati mwengine ni ngumu kuonekana kama umeungwa,uungwaji huu unatofautiana kidogo na wa A huu unahitaji umakini kidogo kwakuwa ukijichanganya kidogo na kusababisha ukagusanisha nyaya hakuna mawasiliano yatakayo pita katika muunganiko huo.Uungaji wa A na B ni kawaida kupunguza signal ikiwa hujaunga vizuri.
NB: muungo A na muungo B unahitaji umakini ili nyaya zisigusane.

SIGNAL QUALITY
Unachopaswa kufanya ni hiki hapa toka kwangu:-

  • Kwanza ni lazima ununue vihusika vifuatavyo

  1. Joint
  2. F connector pic 2
Ambapo thamani yake vyote ni kuanzia 2000 mpaka 3000 ingawaje unaweza ukauziwa hata 10000 inategemea tu unanunua wapi?
  • Chuna Coaxial cable ya vizuri kwa mtindo huu kama inavyoonekana hapo chini
Hakikisha Center conductor haigusani na Outer conductor

Outer conductor unaupindia juu ya jacket kama unavyoona hii picha

Outer conductor inakuja kugusana na Connector utakayoifunga isipokuwa Center conductor haitakiwi igusane na connector
  • Jinsi JOINT inavyofungwa na kufanya kazi






NB:Uungwaji wote wa Cable hakikisha Center conductor haigusani na Outer conductor.

mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

Apr 15, 2016

AV CABLE NI NINI!?


A inasimama badala ya Audio - Sauti
V inasimama badala ya Video - Picha
Zinakuwa nyaya tatu zenye rangi tatu tofauti:-


Nyekundu - Sauti Kulia
Nyeupe - Sauti Kushoto
Nyano - Picha


Hivyo tafsiri nyepesi ni kwamba AV CABLE ni waya unaosafirisha Sauti na Picha kutoka kwenye kifaa chochote kinachoweza kutoa picha na sauti na kuingiza kwenye TV, kifaa hicho kinaweza kuwa DVD, King'amuzi, game n.k.
Mfumo wa picha unaoonekana kwa kutumia AV cable hujulikana kama SD - Standard Definition 
 

Cable hii hutumika kwenye TV yenye AV Port yaani ile sehemu ya kuchomekea AV ambapo napo unachomeka kwa kufata rangi kama uvyoona hapo chini!


Zipo tv ambazo hazina AV port ama hicho kifaa ambacho unataka kutumia AV cable hakina AV Port ufanye nini ili uweze kuendelea kutumia AV cable ama Cable nyengine?
Unapaswa uangalie TV/DVD/King'amuzi kina Port gani badala ya AV Port?
Ufanye nini ikiwa TV yako ina AV port moja ama mbili nawe una vifaa zaidi ya viwili unataka kutumia pasipo kuchomoa chomoa AV cable?
Unapaswa kutumia kifaa kinachoitwa AV SELECTOR
mustaphamadish@gmail.com
+255789476655
Share:

Apr 12, 2016

KOPO HALISAIDII CHOCHOTE KWENYE DISH


Leo nimeonelea niongelee hili jambo kwakuwa ukiachilia kuliona sehemu mbali mbali pia nimekuwa nikulizwa kama kuna umuhimu wa wenye ving'amuzi vya madish kuweka makopo?
 Jambo la awali la kuzingatia king'amuzi kiwe cha Dish ama Antenna kina namna ya ufungaji wake kwa kutumia vifaa vyote vilivyomo kwenye set ya king'amuzi hicho,ikitokea kimojawapo umekiacha ndipo unajikuta nafasi ya kile ulichokiacha inachukuliwa na KOPO!
Kutumia KOPO kunatokana na sababu hizi:-
  • Tuanze kiufundi
- Fundi hupaswi kuacha kutumia kitu chochote kati ya ulivyovikuta kwenye set ya Dish kwakuwa vyote vina kazi yake na ni muhimu sana.

Hapa unamshawishi mteja atafute kopo lilipo ili aweze kufunika akiamini atasaidia angalau kuepusha gharama za kuita ita fundi.

Ukifunga hivi ni kipi ambacho kitamshawishi mteja aongezee ufundi wake wa kuweka kopo?
Fikra za watanzania wengi wanaamini wakifunika na kopo husaidia:-
  • Huzuia kunguru kufanya uharibifu
  • Husaidia picha kutokupotea wakati wa mvua
Niseme tu ukweli KOPO halisaidii chochoteikiwa fundi amefanyakazi safi.
Kupotea kwa Picha kwa dish ndogo kipindi cha mvua ni kawaida kutokana na uwezo mdogo ili kuepuka hili inakulazimu kutumia Dish kubwa ama lnb maalum na kuhusu kunguru fundi akifanyakazi yake vema kunguru hata abembee vipi hawezi kufanya uharibifu!
mustaphamadish@gmail.com
Share:

UMELIPIA NA BADO HUPATI PICHA!?


Hili ni janga kubwa karibia kwa wateja wote wa ving'amuzi vya kulipia,unafanya malipo lakini hupati picha kwa wakti ama hupati picha kabisa!
Njia za kufanya ili usipate usumbufu wakati wa kufanya malipo ya mwezi:-
> Kabla ya kufanya malipo hakikisha unajua bei ya kifurushi unachotaka kulipia
> King'amuzi chako umekiwasha kabla hujafanya malipo
> Ikiwa unalipia kifurushi ambacho ni tofauti na cha awali huna budi kupiga simu ama kufata njia zilizoelekezwa ili kubadili kifurushi
> King'amuzi chako kina Signal ya kutosha

Nini ufanye ikiwa umeshalipia na hukufata njia hizo:-
> Washa king'amuzi chako
> Hakikisha kina Signal kwa kuangalia channel ambayo ipo bure ( mf:ya matangazo )
> Piga simu kwenye kampuni husika ya king'amuzi unachotumia ili ufunguliwe ama upewe maelekezo zaidi na ikitokea umekosa msaada namba hii ni msaada kwako +255789476655
mustaphamadish@gmail.com
Share:

Mar 24, 2016

NINI UFANYE KING'AMUZI CHAKO KIKIPOTEZA SIGNAL!!


Ukiona neno NO SIGNAL ama kwa kukurahisishia ukiona hupati picha kwenye King'amuzi chako na unapata ujumbe ambao hauhusiani na malipo ujue kuna tatizo la Signal lakini utathibitisha vipi kujua kama ni kweli tatizo ni Signal.
> Kila King'amuzi kina channel ya/za bure ( hapa simaanishi Local channel ) ambapo hata ikiwa malipo yako ya mwezi yamekata utaendelea kuangalia tu huwa hazikati,hivyo yakupasa uzijue Channels hizo ili unapoona umepata ujumbe huuelewi jaribu kuweka channels hizo uone zitaonyesha!? Ikiwa zitaonyesha maana yake tatizo sio signal,tatizo litakuwa ni malipo na ikiwa hazitaonyesha jibu lake tatizo ni Signal.Nimejaribu kuwajuza njia hii ya kienyeji kutokana na wengiwetu hizi lugha zilizokuja na ndege ni mtihani nami nimegundua hilo hivyo sitawaacha nitaenda nanyi sambamba!

Cha kufanya ukishajiridhisha kuwa tatizo ni Signal:-
  • Angalia Signal Cable ( waya inayotoka kwenye Dish/Antenna ) ipo sawa?
> Hakuna sehemu iliyochunika/kukatika
> Imechomekwa sawa kwenye King'amuzi chako sehemu ya lnb in/Antenna
> Imechomekwa sawa kwenye Dish/Antenna ya hicho king'amuzi
> Signal Cable ( Coaxial Cable ) Ina nyaya mbili ndani ambazo hazipaswi kugusana ( Siku nitawaeleza kazi za hizo nyaya )

Ikiwa umeona kupo sawa huna budi kuwasiliana na fundi wako ikiwa unamkumbuka ama unaweza kuwasiliana na kampuni husika ya king'amuzi ukikosa msaada piga namba hii +255789476655.

Tatizo linaweza likawa ni nini baada ya hatua za awali kuzifata?
> Yaweza kuwa Dish ama Antenna imepoteza muelekeo wake
> Yaweza kuwa kama king'amuzi cha Dish lnb kufa
> Yaweza kuwa AC ya signal kwenye king'amuzi imekufa
Zaidi ya yote ili kupata uhakika wa nini tatizo ni fundi atakapofika sehemu ya tukio!

IKIWA UMEFANYA MALIPO NA HUPATI PICHA Bofya Hapa

mustaphamadish@gmail.com
+255789476655
Share:

Mar 21, 2016

KIFURUSHI CHA AZAM SPORTS HD HAKIPO TENA!


Hili ni mojawapo kati ya maboresho ya kampuni ya Azam Media kupitia king'amuzi chake cha Azam tv..
Awali kulikuwa na vifurushi kama vitano hivi ambapo ni:-
  1. AZAM PURE PACKAGE tsh 12,000/=
  2. AZAM PLUS PACKAGE tsh 20,000/=
  3. AZAM PLAY PACKAGE tsh 25,000/=
  4. AZAM SPORTS HD PACKAGE tsh 15,000/=
  5. AZAM INDIAN PACKAGE tsh 16,000/=
 Kifurushi cha Azam Sports HD kwanza kikatolewa kujitegemea badala yake kikaongezwa kwenye kila kifurushi kati ya vifurushi vitatu na jambo zuri zaidi kikapunguzwa bei na kuwa tsh 3,000/= Hivyo kama Azam Pure Package badala ya kulipa tsh 12,000/= itakulazimu kulipia tsh 15,000/= ambapo utaona na kifurushi cha Azam Sports HD kwa lugha nyepesi kifurushi cha Azam Sports HD hakipo tena!
UKITAKA KUJUA BEI MPYA YA VIFURUSHI VYA AZAM Bofya Hapa

MAFUNDI +255 789 476 655
Share:

Mar 18, 2016

STARTIMES KIFURUSHI CHAKO KIKIISHA

 

KUNA AINA MBILI YA VING'AMUZI:-
DISH - kinacotumia Dish
ANTENNA - kinachotumia Antenna

Malipo ya mwezi yanapoisha wengi tunajua ya kuwa Local channel zinabaki ni kweli ila sio kwa ving'amuzi vyote!
Kuna namna mbili ya walivyofanya Startimes vipo ving'amuzi ambavyo malipo ya mwezi yakiisha zinabaki local channel na vipo ving'amuzi malipo ya mwezi yakikata local zinakata na kubaki TBC1 na ya matangazo!
Utajuaje kama kipi ni kipi!?
Wakati unataka kununua king'amuzi cha Startimes iwe ya Dish/Antenna muulize anayekuuzia kuwa king'amuzi hicho ni cha aina gani cha kukata local channel ama kubaki!? Usikimbilie unafuu wa bei kwa maana unapopewa bei mbili bei ya chini ndio ambayo malipo yakikata channel hazibaki!
Ukitaka kujua vifurushi vya Startimes Bofya Hapa
Share:

Mar 17, 2016

AZAM TV KIFURUSHI CHAKO KIKIISHA



Nimeonelea niweke hapa ili wateja wote wa Azam tv na wale wanaotaka kujiunga kulifahamu hili..
Awali ilikuwa usipolipia malipo ya mwezi zinabaki Lacal channel kwa muda wa wiki tatu siku 21..
Lakini sasa utaratibu umebadilika,ambapo kama malipo yako ya mwezi yatakata zitabaki channel mbili tu TBC1 na XTRA tofauti na ilivyokuwa awali..
Hii imepokelewa tofauti na mategemeo ya wateja wengi ambao walidhani kadri siku zinavyozidi kwenda nipo unafuu utakuja kupatikana kama Local channel zote kuwa bure hata usipolipia muda wote!
KWAKO IMEKAAJE HII..!!??
Unajua kama kifurushi cha AZAM SPORT HD hakipo!!??
Unataka kujua bei mpya ya vifurushi na maboresho yaliyofanyika!!?? Bofya Hapa

+255 789 476 655
Share:

Mar 10, 2016

CUSTOMER CARE ZA VING'AMUZI TANZANIA


Katika vitu wanavyofail karibia makampuni yote ya ving'amuzi Tanzania ni CUSTOMER CARE ingawaje baadhi ya makampuni wameboresha lakini si kwa kukidhi mahitji ya wote..
Nilichogundua ni kwamba wateja wengi hawapendi kupokelewa na mashine,muda ambao mteja anasikiliza sauti iliyorekodiwa salio lake linaendelea kuliwa matokeo yake mteja anaweza akatumia zaidi ya 5000 na bado hapati nafasi ya kuongea na mhudumu na mara nyingi simu za makampuni za ving'amuzi huwa ni za mezani ( Landline ).
Kampuni moja tu ya king'amuzi Tanzania ambayo simu zake kama utatumia mtandao unaofanana na hizo namba inakuwa bura huliwi shilingi yako,hili ni zuri na makampuni mengine kama wangetumia utaratibu huu ingekuwa ahueni ijapokuwa tatizo la simu ni moja kati ya matatizo makuu!
Ukiachilia utafutaji wa mtoa huduma kuwa wa tabu pia unapompata huyo mtoa huduma anakuhudumia kana kwamba yeye ndiye aliyekupigia bila kujali kwamba wewe ndiye uliyepiga na huna salio la kutosha na ikitokea simu yako ikakatika pasipo kumaliza tatizo lako hata hawasumbuki kukupigia wakiamini lazima utaweka vocha na kuwapigia tu...
Kuna hili nalo mteja anayekuhudumia unamwambia tatizo lako,inaonyesha uelewa wake mdogo shortcut anaona ni kukwambia ubebe king'amuzi chako na kukipeleka katika ofisi zao,ambapo tatizo hilo linaweza likaelekezeka kwenye simu na tatizo likaisha..
Mbaya kupita zote ni hili la namba za Customer Care kutokuwa hewani muda wa kazi tena inaweza ikawa zaidi ya wiki moja hili ni tatizo!
Kwa leo ni hayo tu!

MUSTAPHA HANYA
mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

Mar 9, 2016

KIFURUSHI CHA ZUKU SMART PACK | TSH 8,999


 Habari njema kwa wateja wa zuku na wale wanaotaka kujiunga na zuku tv ni hii hapa:-
Kwa tsh 8,999
Unapata kuona channel za tv 30
Radio 18
+ Local channel

Punde nitawawekea channel zilizopo....!!

Ukitaka kujua vifurushi vingine vya zuku tv BOFYA HAPA
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita