Call / WhatsApp +255673378129

Nov 27, 2017

ZIJUE OFFER ZA VING'AMUZI 2017 KUELEKEA 2018

Tunaelekea katika kumaliza mwaka 2017 na tunategemea kuingia mwaka 2018, yapo mengi ambayo kupitia blog hii umefaidika kwa hali yeyote ile kama ndivyo tunashukuru kwakuwa ndio lengo letu, lakini pia nadhani yapo yaliyokukera kupitia blog hii kama ndivyo tunasikitika na kukuomba radhi pia maana sio lengo letu na ukizingatia hata kama itatokea unafanya jambo zuri vipi sio wote watakaopendezwa nalo kwa kuzingatia wapo ambao lengo lao ni kuharibu tu ama kutengeneza njia ya kufanya vibaya.. Zaidi ya yote shukrani kwa wale wote walio pamoja nasi kwa mwaka mzima na hata hapo miaka ya nyuma maana bila ninyi wala mimi na team yangu tusingefika hapa na isingezaliwa MADISH TECHNOLOGY.
Leo nawaletea orodha ya ving'amuzi vyenye offer katika msimu huu wa kumaliza mwaka 2017:-
 Bofya king'amuzi ambacho unataka kujua offer yake na utapata maelezo ya kina kuhusu offer hizo!
+255789476655 
Whatsapp+255784378129
Insta @mustaphamadish 
Share:

Nov 23, 2017

DISH 3 | DECODER & RECEIVER 18 | CHANNELS 18 | KWA KILA TV


Hotel - Tv system installation:- 
Hii ni hotel ina flow zipatazo tano ina zaidi ya room 50, ina ukumbi wa mikutano,sherehe, ina restaurant, ina bar na kuna sehemu ya Disco pia. Hapa tulichofanya ni kufunga tv ambazo ni zaidi ya 60 tv ambazo kila moja inapokea channels 18 na kila tv inajitegemea,nikiwa na maana mtumiaji anaweza akabadili channel bila kumuingilia mwengine ( tv nyengine ).




Mfumo uliotumika
  Baadhi ya Vifaa vilivyotumika:-
  • Dish ya FTA
  • Receiver kwa channel za Free
  • Dish ya DStv
  • Decoder za DStv
  • Dish ya Azam tv
  • Decoder za Azam tv
  • Signal Ampl.
  • Splitters
  • Multiswitch
  • Cable 
  • Connectors


Dish zimefungwa tatu, mbili zikiwa ni za kulipia na moja ikiwa ni ya channel za bure,Signal inayotoka kwenye Dish inaingia moja kwa moja kwenye chumba maalum, ambapo tunaita control room, sehemu ambayo decoder na receiver zote 18 zinafungwa hapo na sehemu kubwa ya mfumo mzima unafungwa hapo, kisha zinatoka cable ambazo zinakuwa zimebeba channel 18 na zote zinaishia kwenye tv ambazo zipo vyumbani na kwengineko kwenye jengo la hotel.

Hii ni Control Room sehemu ambayo ile connection muhimu yote tumeimaliza hapa

Kwa maelezo zaidi +255789476655
Whatsapp+255784378129
Face Book


Share:

Nov 11, 2017

TUNATENGENEZA UTOFAUTI NA WENGINE

Mwaka unaishia yapo yaliyoenda sawa na yapo ambayo yamezidi kwenda kombo, hapa nazungumzia ulimwengu mzima wa Digital tv, ulimwengu ambao umekuja na fursa kwa namba kubwa kwetu sisi vijana lakini pia kuna changamoto ambhata ambazo zinawakabili wote wanaohusika na mulimwengu huu wa Digital tv... zipo zilizopata utatuzi na zipo ambazo zinaonekana zinaenda kutatuliwa na hapo hapo zipo ambazo hata dalili kama zitakuja kutatuliwa hakuna... Mimi na team yangu kila kukicha tunajitahidi kuwa tofauti na wengine, yaweza kuwa walitutangulia ama wametukuta.. tumelifanya hili kwa uchache ingawaje pongezi tunazozipata inaonyesha walionufaika ni wengi sana kupitia uwanja huu..
Panapo majaaliwa mwakani tutafanya makubwa zaidi na kuwafikia hata ambao hawana uwezo wa kufika humu sisi tutawafikia.!!


 #MustaphaMaDish na zao lake #FundiMakini
Hivi kweli Fundi unafanyaje kazi chafu kama hii!!?? kuna baadhi ya mafundi wengine wamepata ajira kabisa makampuni makubwa yenye kuendesha huduma hizi za Digital tv lakini wanafanya kazi chafu na wanafikia hatua ya kupiga picha na kuzipost kwenye mitandao... mimi ama sisi huwa tunawaita kina #FundiKalipua mbioni kuja na Signal Quality tv
 








Aliyefunga hapa ni #FundiKalipua sio #FundiMakini Toka #MaDishTechnology
Whatsapp +255784378129
Share:

WAKATI MWENGINE TUNAZUNGUMZIA KAZI KWA SURA NYENGINE

 Eneo ni Hotel ya Sea Cliff ndani ya mgahawa wa Karambezi, robo 3 ya wateja wa mgahawa huu ni ngozi nyeupe na lugha itumikayo kwa wengi wa wateja wa hapa ni kiingereza na hivyo hata mazingira huwa kama sio Tanzania hivi...
Kwa mwezi wa 10 imekuwa ni sehemu ambayo nimetembelea zaidi ya mara 12 kwa nyakati tofauti ingawaje ilikuwa tunakula na kunywa lakini kikubwa ilikuwa ni kwa mazungumzo maalumu ya kikazi zaidi isipokuwa kwa sura nyengine na siku ya 12 mtu wa mwisho kufanya nae mazungumzo alikuwa ni Gabo na Deo.
Naweza kusema kila jambo ama hatua upigayo shukuru Mungu kwakuwa yeye ndiye anayekuwezesha!
Alhamdullah!



mustaphamadish@gmail.com

Share:

Nov 5, 2017

OFFER YA STARTIMES 2017 KUELEKEA 2018


MFALME WA BURUDANI ZA FAMILIA
Offer hii inakupa unafuu kama ifatavyo:-
  • Kwa Tsh 78,000 StarTimes ya Dish - Unapata vifaa pamoja na kifurushi cha mwezi mmoja.
  • Kwa Tsh 34,000 Decoder ya Antenna.
  • Ufundi Tsh 30,000 Startimes ya Dish.
  • Ufundi Tsh 20,000 Startimes ya Antenna.
  • Vifurushi vya Startimes Bofya Hapa
King'amuzi cha Startimes kinafanya vizuri sana kwa Offer mara kwa mara hutoa offer na zawadi kem kem hii ni katika kufanya wateja na wanaotaka king'amuzi hiki kupata ahueni!
Kwa Maelezo zaidi +255789476655 
Whatsapp+255784378129
Share:

Nov 1, 2017

OFFER YA ZUKU TV


Katika kumbukumbu yangu ilikuwa ili umiliki king'amuzi cha Zuku tv ni lazima ilikuwa uwe na Tsh150,000/= Bei ikashuka ikawa Tsh 105,000/=! Ikashuka tena kwa Tsh 95,000/=
Kwa sasa OFFER iliyopo ni tsh 88,000/= unapata Dish,Decoder,Kufungiwa na miezi mitatu bure!
Bei hii inakuwa ni bila ya ufundi, ufundi ni Tsh 20,000/=
Whatsapp+255784378129
mustaphamadish@gmail.com
NB:Usikubali kulipa zaidi!

Share:

Oct 31, 2017

TUMEFUNGA TV 15 | DISH 1 | MUHIMBILI HOSPITAL

Ilikuwa ni kazi ya siku moja ama 2 ila kutokana na mazingira yalivyo imetuchukua wiki 2 ama 3.. hii ni sehemu ambayo haitakiwi kelele na inapotokea idadi ya wagonjwa ni kubwa hakuna nafasi ya kina sie kufanya tulichokifanya hivyo ikawa tunachagua siku maalumu katika wiki ili kulitimiza hili tulilolifanya..
Huu ni mfumo ambao umetumia Dish 1 Decoder 1 lakini picha imeenda kwenye tv 15 na zote zikiwa saaaafi huku tukiacha wagonjwa wakipata alau taarifa ya habari...!


Tupigie +255789476655
Whatsapp+255784378129
Share:

Oct 30, 2017

STARTIMES UNALIPIA KIFURUSHI HAKIFIKI MWEZI!?

Jinsi inavyokuwa:- Kuna aina tofauti ya vifurushi kwa king'amuzi cha Antenna na Dish pia
Watumiaji wengi wa king'amuzi cha StarTimes hulipia pengine 9,000 ama 6,000 na kutegemea kifurushi alicholipia kiishi kwa muda wa mwezi mmoja,matokeo yake kinaenda wiki moja ama hata wakati mwengine hakifiki wiki malipo yanaisha na mtumiaji kutakiwa kulipia tena,hapa ndipo wateja wengi hutamani kukibeba king'amuzi na kukipiga chini!!!
Usichokijua ni kwamba:- Kifurushi ulichopo ni cha juu,yawezekana upo kwenye kifurushi cha Tsh 24,000 ama cha Tsh 36,000 hivyo inapotokea umelipia Tsh 9,000 ama Tsh 6,000 itahesabu siku hivyo haitafika mwezi channel zitakata!
Unachopaswa kufanya:- Ikiwa hujua upo kifurushi gani ni bora kufanya jambo moja la msingi upige simu kabla ama baada tu ya kulipia ili uhamishiwe katika kifurushi unachokitaka kikuwezeshe kufika mwezi mzima!
Kwa Maelezo zaidi!
+255789476655
Whatsapp +255784378129



Share:

Oct 29, 2017

KWENYE NYUMBA 1 | TUMIA DISH 1 KWA WAPANGAJI WOTE


Imezoeleka kufanyika kwenye Aparment kubwa,ambapo gharama na hata mfumo wake huwa expensive ila leo nikupe siri, mfumo huu unaweza kuwa rahisi na bora kwako hata wewe ambaye unamiliki nyumba ambayo sio apartment kuubwa, hata nyumba ya kawaida ambayo ina wapangaji ama mnaishi wenyewe tu familia na mngependa kutumia Dish moja ama Antenna moja kwa tv zote zilizopo kwenye nyumba yako na kila tv ikiwa na king'amuzi chake, kinachotumika kwa wote ni Dish ama Antenna isipokuwa king'amuzi kila mtu anakuwa na chake na analipia vile apendavyo! tumeifanya rahisi kwako ambapo kwa gharama ndogo itakuwezesha kumudu. Hii ni kwa wamiliki wa nyumba ambao mmekusudia ziwe za biashara kwa maana kupangisha,tumeona msuguano uliopo hivi sasa kwenye majumba mengi pale ambapo tumepata kazi ya kwenda kufunga madish,kuna upishani kati ya mwenye nyumba na mpangaji na mara nyengine hutokea upishani kati ya fundi na mteja wake ambaye ni mpangaji wa hiyo nyumba,upishani hutokea pale ambapo mmoja anapopendekeza dish ifungwe mahali fulani huku fundi akitaka ifungwe mahali fulani mwisho wa ubishani huu mara zote fundi huwa mshindi kwakuwa dish haifungwi tu kama inavyofungwa Antenna ya kawaida,dish inamuelekeo wake maalumu na ni lazima ufatwe.



Technology ambayo inatumika imewarahisishia wenye nyumba na pia,nikupe faida kiuchache:-wapangaji
Faida kubwa anayopata mwenye nyumba ni kuepuka uharibifu wa nyumba yake. Faida nyengine ni jengo ama nyumba kuwa safi ( Muonekano mzuri )
Faida anazopata mpangaji ni kupunguza gharama za kufunga na kurepair king'amuzi.

 Dish ambazo zina wateja wengi.

Antenna.

INAFANYAJE KAZI:-
  • Inafungwa Dish moja ama mbili zile zinazopendwa kutokana na eneo ulilopo ama utapata ushauri toka kwetu.
  • Unaweza ukafunga na Antenna 1 kama kutakuwa na ulazima huo.
  • Inaenda Cable kwa kila Point ya Tv kwa nyumba ama jengo lote husika.
  • Kila mpangaji/Mkazi wa hiyo nyumba/jengo atakachopaswa kuhamia nacho/kununua ni king'amuzi tu na kuchomeka pasipo kufunga tena Dish/Antenna.
  • Kila kwenye tv ( King'amuzi ) ataweza kufurahia matangazo pasipo kumuingilia mwengine.
  • Ikitokea kuna repair wahusika wote watahusishwa ama watahusika kwakuwa Dish/Antenna ni moja.

 INAWEZEKANAJE?
     Tupigie  +255789476655  
Whatsapp+255784378129
Email:mustaphamadish@gmail.com
Popote Tanzania ukituhitaji tunafika kwa kazi zifatazo:-
  • Kufunga mfumo wa TV kwenye Hotel
  • Kufunga mfumo wa TV kwenye Apartment
  • Kufunga mfumo wa TV kwenye Nyumba binafsi
  • Kufunga mfumo wa TV kwenye Office
  • Kufunga mfumo wa TV kweny Lodge/Bar n.k
  • Kufunga CCTV Cameras kwenye Hotel/Apartment/Office n.k
  • Kufunga Electric Fence kwenye Yard/Apartment/Office n.k
Share:

Oct 15, 2017

CABLE SNAKE BUNNINGS


Hiki ni kifaa maalum ambacho kinatumika katika kuvuta wire unaopita kwenye Conduit, hutumika pale inapotokea ugumu katika kupitisha cable ili uweze kufika kwenye point husika..
Cable Snake mara nyingi hutumika pale tunapofanya Installation kwenye Apartment, Hotel, n.k

Naseer - Zao la Mustapha MaDish akifanya yake na Cable Snake

Technical Director akizungumza na mjomba Cable Snake

Karibu kwa Ushauri, Huduma na Yote yanayohusu burudani ya TV.
Whatsapp+255784378129
+255789476655
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita