Call / WhatsApp +255673378129

Dec 6, 2015

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI DSTV


Wateja wengi wa DStv wanakumbwa na kadhia hii,kutokujua utaratibu kwa kutaka kuhama kutoka kifurushi kimoja kwenda kingine hivyo kwa post hii utaelewa vema jinsi ya kuhama kifurushi!
Kwanza vijue vifurushi vya Dstv kwa Kubofya Hapa
Ikitokea umelipia kifurushi cha DStv Bomba  Tsh 23,500 na mwezi umeshaisha unataka kulipia kifurushi cha DStv Compact  Tsh 84,500 unaweza kufanya hivyo kwa kufata utaratibi huu:-

1 - Washa Decoder yako,kisha weka channel namba 200.
2 - Lipia Tsh 84,500 
3 - Piga nambari 0768988800 ( Atakayepokea mwambie kuwa unahitaji kubadili kifurushi toka DStv Bomba kwenda DStv Compact nae atafanya hivyo na itapokea ndani ya dk 5 tu )

Unaweza kubadili kifurushi kwa kufata utaratibu huu kwa kifurushi chochote kile na unaweza kufanya zoezi hili hata kabla kifurushi chako hakijaisha!

+255789476655
Share:

Dec 5, 2015

EMANUEL TV | TB JOSHUA

 Ni mkristo gani ambaye ni muangaliaji wa tv na haijui Emmanuel tv? ama hamjui TB Joshua?
Pastol wa kanisa la mataifa yote..
Emmanuel tv ni tv ambayo ina wapenzi karibu dunia nzima,ni tv kubwa sana ya dini ambayo makao makuu yake ni Lagos Nigeria,imeanzishwa 8/3/2006 mmiliki akiwa ni Emmanuel Global Network,Lugha inayotumika ni English,Inarusha matangazo Africa,North/Central America na Europe!
Binafsi na team yangu tumeshafunga sana madish ili wadau waangalie hii tv inapatikana bure kama utafunga kwa kupitia Dish ndogo/kubwa na receiver ya kawaida tu unapata zaidi ya channel 65 zote zikiwa free ikiwemo hii Emmanuel tv! Ila hata katika baadhi ya ving'amuzi Emmanuel tv inapatikana ila huko ni lazima malipo ya mwezi yahusike vinginevyo huwezi kuiona!

Kwa maelezo zaidi jinsi ya kuipata channel hii na nyengine za Dini!
+255 789 476 655





Share:

Dec 3, 2015

FUNDI DISH HUJISIKII VIBAYA | KWA UCHAFU HUU!?

 Lawama zimekuwa ni nyingi kuhusu Ving'amuzi kusumbua,ambapo Ving'amuzi vinavyolalamikiwa wala havina usumbufu huo,katika kuchunguza nimegundua ya kuwa mafundi husababisha Ving'amuzi vionekane vinasumbua hata kama havina sifa hiyo ijapokuwa kweli kuna Baadhi ya Ving'amuzi vinasumbua ukiachilia uwezo wa fundi..
Baadhi ya Dish nilizowahi kukutana nazo na nikabahatisha kupiga picha ni hizi hapa chini:-

 Dish ya ZUKU tv
Badala ya fundi kutoboa na Drill yeye alichofanya ni kutafuta mawe na mbao na kufanya alichofanya kama ambavyo macho yenu yanaona hapo,matokeo yake kila baada ya muda mfupi picha itakuwa inakata kata ama hata kupotea na matokeo yake fundi hakauki kwako mwisho wa siku king'amuzi hiki kinasumbua!
 Hizi ni Dish za Azam tv
Nilikutana nazo pale Ubungo National Housing,hii ya mbele ndio mpya kwa muonekano na ya kule mwisho ya siku za nyuma kidogo,kilichofanyika hapa ni kile kile uzembe wa fundi wa kutokutoboa na Drill!

Alichofanya fundi ni kutafuta misumari ya zege na kugonga mpaka nadhani alijibonda midole kwa maana zege hili sio la kitoto..

 Baada ya kukata misumari kadhaa maana ulishindwa kuingia wote akaonelea atafute vitu vya kuweka ili kuweza kukaza kwakuwa msumari hauwezi kuingia wote,juu ya kichwa cha msumari kumewekwa bolt kwa ili pia kuweka mkaze ambao haijasaidia chochote..

 .....!!

 Kwakuwa kazi yote aliyoifanya haijasaidia kitu fundi huyu akaonelea atafute na kamjiti ili kuizuia Dish hii isishuke na kupoteza signal..

 Fundi wetu huyu akamalizia kwenye kuchomeka cable kwenye lnb,ukiachilia uchafu alioufanya hapo pia kuna kitu hajakifunga hapo ambacho kazi yake ni kufunika kabisa hayo maungio ya hiyo cable,je unayajua madhara ya ufundi huu..!!??

 Kazi ya fundi hiyoo...!!!

 Yametafutwa mawe yalipo yakapangwa kwa uchungu ili kuhakikisha signal zinapatikana na hazipotei..
Ah jamani kweli hii hata hujisikii vibaya bwana fundi..!!??

 Ile ya zege ikagongwa hapa kwa mbwembwe balaa..

 Hivi mteja wako unayemfungia ameona kazi hii?

Hii ni maeneo ya Kimara ila hii cha ajabu ni kwamba ilipofungwa mteja anaona kila kitu jinsi ilivyo sasa ambacho nimeshindwa kuelewa ameridhika na uchafu huu ama vepe!
 Hii ni Dish ya DStv

 Macho yako yameona nini hapo...!?

 Ni wazi kuwa ukuta huo haufai kubeba hii dish ila alichofanya bwana fundi akatumia ufundi wake kuonyesha yakuwa hata kama ukuta haufai yeye anauwezo wa kufanya ukafaa..

 Fundi na ufundi wao..!

 Hapa uhakika wa signal hakuna kabisa...

 Hii nadhani inatokea kwa mafundi dish wa Tanzania tu!


Hapa utalaumu King'amuzi unachotumia ama fundi aliyekufungia?
Nnachoweza kukusihi angalia sana kazi anayokufanyia fundi wako zinafanana na hizi?
JE UNAHITAJI FUNDI KWENYE KAZI SAFI TOFAUTI NA UCHAFU HUU KWA AJILI YA KING'AMUZI CHOCHOTE UNACHOKIJUA WEWE?
PIGA +255 789 4766 55



Share:

Dec 1, 2015

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI AZAM TV


Wateja wengi wa Azam tv wanakumbwa na kadhia hii,kutokujua utaratibu kwa kutaka kuhama kutoka kifurushi kimoja kwenda kingine hivyo kwa post hii utaelewa vema jinsi ya kuhama kifurushi!
Kwanza vijue Vifurushi vya Azam tv kwa kubofya Hapa
Ikitokea umelipia kifurushi cha Azam Pure Tsh 15,000 na mwezi umeshaisha unataka kulipia kifurushi cha Azam Plus Tsh 23,000 unaweza kufanya hivyo kwa kufata utaratibi huu:-
Lipia kwanza Tsh 23,000 kisha chukua simu yako bonyeza *150*50*5# kisha piga utapata ujumbe huu
Karibu Azam tv
Chagua
  1. Kiswahili <
  2. English
( Tunachagua kiswahili,una bofya OK )
  1. Angalia salio
  2. Badili kifurushi <
  3. Sajili Huduma Mpya
  4. Endeleza Kifurushi Cha Nyongeza
( Unachagua Badili kifurush,una bofya OK )

Ujumbe utakaoupata nia:-
  • Tafadhali ingiza namba ya Smartcard
( Weka namba za Smartcard yako,kisha una bofya OK )

Ujumbe utakaoupata ni:-
  1. Pure 15,000
  2. Plus 23,000 <
  3. Play 28,000
  4. Kihindi Pekee 16,000
( Unachagua namba 2,una bofya OK )

Ujumbe utakaoupata ni:-
  1. Badili sasa hivi <
  2. Badili baada ya kifurushi kuisha
( Unachagua namba 1,una bofya OK )

Ujumbe utakaoupata ni:-

Asante. Ombi lako linashughulikiwa. Utapata ujumbe muda si mrefu.AZAM TV

Kisha utapokea ujumbe mfupi kwenye simu yako unaotoa maelezo kama ombi lako limefanikiwa ama laa!!
Hii ni jinsi ya kuhama toka kifurushi cha Azam Pure kwenda kifushi cha Azam Plus.Utaratibu wa kuhama kifurushi ni huu kwa vifurushi vyote na ikitokea umelipia Tsh 23,000 na haujahama kifurushi itafunguka kifurushi kile kile cha Tsh 15,000 na kubaki kwenye a/c yako Tsha 5,000.Unaweza ukabadili kifurushi ndani ya masaa 72 kwa lugha nyepesi siku tatu na ikitokea imezidi hapo huna budi kupiga simu ili wakusaidie zaidi!
Zoezi hili uhakikishe king'amuzi chako umekiwasha kisha ndipo unafanya zoezi hili na inachukua dk 5 mpaka 20 kubadilika kifurushi na ukitaka kujua zoezi lako limefanikiwa baada ya muda Angalio Salio kwa kutumia utaratibu wa hapo juu!
Kwa uchache huu nadhani nimekusaidia kitu!

+255 789 476 655
Share:

Nov 26, 2015

RATIBA YA AZAM TV

Ilikupata ratiba ya king'amuzi chako cha Azam tv:-
Chukua remote yako,bonyeza 1- menu..

2- Digital TV
 

3- Programme Guide 

4- Chagua channel unayotaka kupata ratiba yake ya wiki nzima kama inavyoonekana hapo juu! 
 
5- Ikiwa maelezo hayajaeleweka kwamsaada Zaidi piga +255789476655
Share:

Nov 25, 2015

KUZIMIKA KWA VING'AMUZI BILA TAARIFA KWA WATEJA!

Idadi ya simu ninazopokea kwa takribani wiki tatu mpaka leo hii ni wateja wa baadhi ya ving'amuzi ambavyo vimekata matangazo yao bila taarifa yeyote kwa wateja wao na kitu kibaya zaidi ushirikiano unakuwa sio mzuri kwa mujibu wa wateja wanaonipigia mimi!


Ving'amuzi vilivyokata ni ZUKU tv.
Ijapokuwa ikarejea hewani ila hakukuwa na taarifa yeyote ama kuwataka radhi wateja wao.
TING nao wakapotea hewani mpaka leo hii na mchezo ni ule ule hakukuwa na taarifa wala kuomba radhi kwa kwa nguvu ile wanayotumia kuuza ving'amuzi!

CONTINENTAL pia hawapo hewani!
Ubaya ambao unatokea hapa taarifa na kuwataka radhi wateja hakuna kwa nguvu ile wanayotumia kuuza king'amuzi na kwa bahati mbaya Continental wana nafasi nzuri ya kufikisha ujumbe kwa umma kupitia Startv ama RFA lakini matangazo yanayoendelea ni yale ya kuuza ving'amuzi!
ANGALIZO TOKA KWA MUSTAPHA MADISH:
Tatizo lililopo kwa Continental na Ting ni satellite waliyopo ya Amos 5:-
Jukumu la makampuni waliyopo Satellite hii walitakiwa watoe taarifa kwa wakati kwa wateja wao ili waendelee kuwa na imani nao kwa maana ipo wazi kifundi tunajua Satellite ya Amos 5 haipo tena imepotea hivyo ili Ting na Continental ni lazima wahame Satellite je watahamia Satellite gani hilo wanalijua wahusika.
Yapo matatizo ambayo huwezi kuyazuia kwakuwa najua vema mfumo mzima ulivyo,yapo ya kuepukika na yapo ambayo hayaepukiki,ila kinachopaswa kufanyika ni kutoa taarifa kwa wakati kwa wateja wenu na kwa umma kwa ujumla huku mkiendelea kutatua tatizo kwa wakati,kukaa kimya kwenu ni kupoteza imani kwa wateja wenu,inaonekana mnatoa huduma mbovu na hii inapelekea kufanya maamuzi ya kuamua kununua king'amuzi kingine!
+255789476655
Share:

Nov 19, 2015

UNATAKA KUJUA NINI KUHUSU DIGITAL TV ?



Yapo mengi ambayo siwezi kuyamaliza kwa siku moja na pia siwezi kuyamaliza ikiwa sijajua ambacho wewe ungependa kujua kuhusu ulimwengu huu wa Digital tv na hata ukihitaji kujua yale ya Analogue tv nipo tayari kukujuza kwa kina kabisa!
Ni nini ambacho ungependa kukijua yawezekana kuhusu king'amuzi chochote kati ya vilivyopo Tanzania ama vinavyotumika Tanzania ingawaje ninauzwa nje ya nchi.Hata kama swali halihusiani na ving'amuzi ila tu linahusiana na ulimwengu huu wa Digital tv nnachoweza kusema karibu alau tuwekane sawa.

NIULIZE:
  • Chochote ambacho ungependa kujua ikiwa kutokea kule tulikotoka Analogue tv ama hapa tulipo Digital tv.
  • Jambo lolote la kiufundi ambalo linakutatiza katika ving'amuzi vyote vilivyopo.

Ili na wengine wanufaike na majibu ya maswali yatakayoulizwa naomba muulize kwenye sehemu ya ku comment nami nitajibia hapo ili maswali yasijirudie!
Share:

Nov 16, 2015

DSTV HUDUMA KWA WATEJA NA KUPATA MAFUNDI WA DSTV


Je unatumia DStv? ama unahitaji kujiunga na DSTV? 
Karibu kwa kufata utaratibu huu:-

IKIWA UNATUMIA DSTV:
  • Umelipia na bado hupati channel?
  • Picha inakatakata ama haionyeshi kabisa
  • Unataka kuhama toka nyumba moja kwenda nyengine
  • Unahitaji kuongeza Decoder nyengine ama kubadili
  • Unahitaji ufafanuzi zaidi kuhusu bei mpya za vifurushi
  • Unahitaji kujua chochote kuhusu huduma za DStv
  • Unahitaji Fundi 
  • Msaada wowote wa kiufundi
Dish ya DStv ikiwa kwenye setting!

Fundi akifanya ufundi wake!

Piga simu namba +255658046655 Kwa msaada zaidi! 

UNAHITAJI KUJIUNGA NA DSTV
  • Kujua Bidhaa zote za DStv
  • Kujua bei halisi/Offer ya kununua king'amuzi
  • Kujua bei halisi ya vifurushi Bofya Hapa
  • Kujua bei ya Ufundi
  • Kujua namna ya kuweza kuunganishwa
  • Kupata huduma ya kuletewa ulipo na kulipia baada ya kuletewa
  • Ikiwa umenunua na hujafungiwa ili upate fundi popote ulipo Tanzania
  • Yote yanayohusu DStv

Piga simu namba +255658046655 Kwa msaada zaidi!


Share:

Nov 1, 2015

VIFURUSHI NA CHANEL ZA STARTIMES



Ni moja kati ya makampuni ambayo yanamiliki ving'amuzi aina mbili tofauti kimasafa,nikiwa na maana ya kuwa kuna aina mbili ya Decoder za startimes:
  • StarTimes ya Antenna
  • StarTime ya Dish
Kwa kukurahisishia startimes wakati wanaanza hapa nchini walianza na mfumo wa kutumia Antenna tu,mfumo huu ukawa na lawama nyingi sana katika swala zima la kukatakata kwa picha wakaja kuboresha kwa kuleta na mfumo wa Dish ingawaje hata ule mfumo wa Antenna nao kwa sasa upo vizuri umeboreshwa!

Hivi ndivyo vifurushi vya StarTime:-

KWA KING'AMUZI CHA DISH

1- KIFURUSHI CHA NYOTA
Ina channels 30+ bora!
Bei yake ni Tsh 11,000 Kwa mwezi
Tsh 4,000 Kwa wiki
Tsh 1,100 Kwa siku
Bofya hapa kujua channels zilizopo kwenye kifurushi hiki!

2- KIFURUSHI CHA SMART
Ina channels 60+ bora!
Bei yake ni Tsh 21,000 Kwa mwezi
Tsh 8,000 Kwa wiki
Tsh 2,100 Kwa siku
Bofya hapa kujua channels zilizopo kwenye kifurushi hiki!

3-STARTIMES SPORT PLUS ( Cha ziada )
Ina channels 4+ bora!
Bei yake ni Tsh 14,000
Bofya hapa kujua channels zilizopo kwenye kifurushi hiki!

4- KIFURUSHI CHA SUPER
Ina channels 100+ bora!
Bei yake ni Tsh 36,000 Kwa mwezi
Tsh 12,000 Kwa wiki
Tsh 3,600 Kwa siku
Bofya hapa kujua channels zilizopo kwenye kifurushi hiki!

5- STARTIMES CHINESE PACKAGE
Inajumuisha kifurushi cha Smart
Ina channels 84+ bora!
Bei ni Tsh 43000
Bofya hapa kujua channels zilizopo katika kifurushi hiki!

6-STARTIMES INDIAN PACKAGE 
Sasa inapatikana kama kifurushi cha ziada
Ina channels 8+ bora!
Bei ni Tsh 18000
Bofya hapa kujua channels zilizopo kwenye kifurushi hiki!

KWA KING'AMUZI CHA ANTENNA

1-  KIFURUSHI CHA NYOTA
Ina channels 30+ bora!
Bei yake ni Tsh 9,000 Kwa mwezi
Tsh 3,000 Kwa wiki
Tsh 900 Kwa wiki
Bofya hapa kujua channels zilizopo kwenye kifurushi hiki!

2-  KIFURUSHI CHA MAMBO
Ina channels 60+ bora!
Bei yake ni Tsh 14,000 Kwa mwezi
Tsh 6,000 Kwa wiki
Tsh 1,500 Kwa siku
Bofya hapa kujua channels zilizopo kwenye kifurushi hiki!

3-  KIFURUSHI CHA UHURU
Ina channels 80+ bora!
Bei yake ni Tsh 20,000 Kwa mwezi
Tsh 7,000 Kwa wiki
Tsh 2,500 Kwa siku
Bofya hapa kujua channels zilizopo kwenye kifurushi hiki!




Kwa Maelezo zaidi
Instagram @mustaphamadish
Call / Whatsapp / Text 
+255 658 046 655
Share:

KING'AMUZI GANI BORA TANZANIA!?


Swali ambalo kila kukicha nakutana nalo kutoka kwenu..
Kwa kuanzia nikwambie ving'amuzi vilivyopo Tanzania ili niweze kukwambia kilicho bora..
Azam tv
 Continental
Coconut Digital tv
DStv
Digitek
Easy tv
Startimes
Ting
Zuku tv
Kwa kuanzia nikwambie ving'amuzi vyote vina ubora wake na mapungufu yake,itakapotokea umemiliki king'amuzi kimojawapo kati ya hivyo lazima utatoa sifa na mapungufu pia ila tatizo linakuja pale mapungufu yanapozidi sifa jibu linakuwa hakifai ila kama itatokea sifa zikazidi mapungufu jibu linakuja ndicho king'amuzi bora.
Ili ujue ni king'amuzi gani bora inapaswa kutambua wewe muhitaji vifuatavyo:-
  • Unataka kuangalia nini? ( Unapendelea channel gani )
  • Unataka kuangalia picha katika ubora upi?
  • Uwezo wako kifedha wa kununua king'amuzi na kufanya malipo ya mwezi?
  •  
Ukishajielewa wewe mwenyewe ndipo unapaswa kufanya hili la pili:-
  • Tafuta chaguo lako lilipo ( Unachotaka kuangalia kipo king'amuzi gani )
  • Ubora wa kampuni husika na Product ( Huduma zitolewazo ni katika misingi inayotakiwa )
  • Uliza kwa mtu ama watu wanaojua ( wanaotumia/waliowahi kutumia ) king'amuzi unachohisi kinakufaa ili kujiridhisha kabla ya kununua.N.B:usiulize kwenye kampuni husika kabla hujauliza kwa wanaotumia kwakuwa kama kampuni inayouza hicho king'amuzi hakitakupa jibu sahihi ila watakupa jibu la kibiashara ili ununue.
  • Uliza hapa +255789476655 tunajua ving'amuzi vyote kiundani zaidi,jibu utakalopata hapa lifanyie kazi.
  •  
King'amuzi gani unachopaswa kununua baada ya kuzingatia hayo:-
  • Ambacho kina Products nzuri na imara.
  • Ambacho kinajali wateja  
  • Ambacho matangazo yake hayakatikati kira mara pasipokuwa na taarifa.
  • Ambacho kina channel nzuri na picha safi.
  •  
Kila king'amuzi kinajitahidi kufanya kila wawezalo ili wawe wabora,wingi wa ving'amuzi umesaidia hili hivyo kila leo uboreshaji unafanyika kama unaona king'amuzi unachotumia hawana dalili ya kuboresha huduma zao unangoja nini kuhama!?
Kuna king'amuzi kilikuwa na wateja wengi sana lakini sasa ama kila kukicha idadi ya wateja inapungua,unadhani ni kutokana na nini? huduma mbovu na kutotaka kubadilika,hili makampuni mengine mjifunze laa sivyo kila kukicha watabadilishwa Ma sales Manager
+255 789 476 655 
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita