Call / WhatsApp +255673378129

Mar 24, 2016

NINI UFANYE KING'AMUZI CHAKO KIKIPOTEZA SIGNAL!!


Ukiona neno NO SIGNAL ama kwa kukurahisishia ukiona hupati picha kwenye King'amuzi chako na unapata ujumbe ambao hauhusiani na malipo ujue kuna tatizo la Signal lakini utathibitisha vipi kujua kama ni kweli tatizo ni Signal.
> Kila King'amuzi kina channel ya/za bure ( hapa simaanishi Local channel ) ambapo hata ikiwa malipo yako ya mwezi yamekata utaendelea kuangalia tu huwa hazikati,hivyo yakupasa uzijue Channels hizo ili unapoona umepata ujumbe huuelewi jaribu kuweka channels hizo uone zitaonyesha!? Ikiwa zitaonyesha maana yake tatizo sio signal,tatizo litakuwa ni malipo na ikiwa hazitaonyesha jibu lake tatizo ni Signal.Nimejaribu kuwajuza njia hii ya kienyeji kutokana na wengiwetu hizi lugha zilizokuja na ndege ni mtihani nami nimegundua hilo hivyo sitawaacha nitaenda nanyi sambamba!

Cha kufanya ukishajiridhisha kuwa tatizo ni Signal:-
  • Angalia Signal Cable ( waya inayotoka kwenye Dish/Antenna ) ipo sawa?
> Hakuna sehemu iliyochunika/kukatika
> Imechomekwa sawa kwenye King'amuzi chako sehemu ya lnb in/Antenna
> Imechomekwa sawa kwenye Dish/Antenna ya hicho king'amuzi
> Signal Cable ( Coaxial Cable ) Ina nyaya mbili ndani ambazo hazipaswi kugusana ( Siku nitawaeleza kazi za hizo nyaya )

Ikiwa umeona kupo sawa huna budi kuwasiliana na fundi wako ikiwa unamkumbuka ama unaweza kuwasiliana na kampuni husika ya king'amuzi ukikosa msaada piga namba hii +255789476655.

Tatizo linaweza likawa ni nini baada ya hatua za awali kuzifata?
> Yaweza kuwa Dish ama Antenna imepoteza muelekeo wake
> Yaweza kuwa kama king'amuzi cha Dish lnb kufa
> Yaweza kuwa AC ya signal kwenye king'amuzi imekufa
Zaidi ya yote ili kupata uhakika wa nini tatizo ni fundi atakapofika sehemu ya tukio!

IKIWA UMEFANYA MALIPO NA HUPATI PICHA Bofya Hapa

mustaphamadish@gmail.com
+255789476655
Share:

Mar 21, 2016

KIFURUSHI CHA AZAM SPORTS HD HAKIPO TENA!


Hili ni mojawapo kati ya maboresho ya kampuni ya Azam Media kupitia king'amuzi chake cha Azam tv..
Awali kulikuwa na vifurushi kama vitano hivi ambapo ni:-
  1. AZAM PURE PACKAGE tsh 12,000/=
  2. AZAM PLUS PACKAGE tsh 20,000/=
  3. AZAM PLAY PACKAGE tsh 25,000/=
  4. AZAM SPORTS HD PACKAGE tsh 15,000/=
  5. AZAM INDIAN PACKAGE tsh 16,000/=
 Kifurushi cha Azam Sports HD kwanza kikatolewa kujitegemea badala yake kikaongezwa kwenye kila kifurushi kati ya vifurushi vitatu na jambo zuri zaidi kikapunguzwa bei na kuwa tsh 3,000/= Hivyo kama Azam Pure Package badala ya kulipa tsh 12,000/= itakulazimu kulipia tsh 15,000/= ambapo utaona na kifurushi cha Azam Sports HD kwa lugha nyepesi kifurushi cha Azam Sports HD hakipo tena!
UKITAKA KUJUA BEI MPYA YA VIFURUSHI VYA AZAM Bofya Hapa

MAFUNDI +255 789 476 655
Share:

Mar 18, 2016

STARTIMES KIFURUSHI CHAKO KIKIISHA

 

KUNA AINA MBILI YA VING'AMUZI:-
DISH - kinacotumia Dish
ANTENNA - kinachotumia Antenna

Malipo ya mwezi yanapoisha wengi tunajua ya kuwa Local channel zinabaki ni kweli ila sio kwa ving'amuzi vyote!
Kuna namna mbili ya walivyofanya Startimes vipo ving'amuzi ambavyo malipo ya mwezi yakiisha zinabaki local channel na vipo ving'amuzi malipo ya mwezi yakikata local zinakata na kubaki TBC1 na ya matangazo!
Utajuaje kama kipi ni kipi!?
Wakati unataka kununua king'amuzi cha Startimes iwe ya Dish/Antenna muulize anayekuuzia kuwa king'amuzi hicho ni cha aina gani cha kukata local channel ama kubaki!? Usikimbilie unafuu wa bei kwa maana unapopewa bei mbili bei ya chini ndio ambayo malipo yakikata channel hazibaki!
Ukitaka kujua vifurushi vya Startimes Bofya Hapa
Share:

Mar 17, 2016

AZAM TV KIFURUSHI CHAKO KIKIISHA



Nimeonelea niweke hapa ili wateja wote wa Azam tv na wale wanaotaka kujiunga kulifahamu hili..
Awali ilikuwa usipolipia malipo ya mwezi zinabaki Lacal channel kwa muda wa wiki tatu siku 21..
Lakini sasa utaratibu umebadilika,ambapo kama malipo yako ya mwezi yatakata zitabaki channel mbili tu TBC1 na XTRA tofauti na ilivyokuwa awali..
Hii imepokelewa tofauti na mategemeo ya wateja wengi ambao walidhani kadri siku zinavyozidi kwenda nipo unafuu utakuja kupatikana kama Local channel zote kuwa bure hata usipolipia muda wote!
KWAKO IMEKAAJE HII..!!??
Unajua kama kifurushi cha AZAM SPORT HD hakipo!!??
Unataka kujua bei mpya ya vifurushi na maboresho yaliyofanyika!!?? Bofya Hapa

+255 789 476 655
Share:

Mar 10, 2016

CUSTOMER CARE ZA VING'AMUZI TANZANIA


Katika vitu wanavyofail karibia makampuni yote ya ving'amuzi Tanzania ni CUSTOMER CARE ingawaje baadhi ya makampuni wameboresha lakini si kwa kukidhi mahitji ya wote..
Nilichogundua ni kwamba wateja wengi hawapendi kupokelewa na mashine,muda ambao mteja anasikiliza sauti iliyorekodiwa salio lake linaendelea kuliwa matokeo yake mteja anaweza akatumia zaidi ya 5000 na bado hapati nafasi ya kuongea na mhudumu na mara nyingi simu za makampuni za ving'amuzi huwa ni za mezani ( Landline ).
Kampuni moja tu ya king'amuzi Tanzania ambayo simu zake kama utatumia mtandao unaofanana na hizo namba inakuwa bura huliwi shilingi yako,hili ni zuri na makampuni mengine kama wangetumia utaratibu huu ingekuwa ahueni ijapokuwa tatizo la simu ni moja kati ya matatizo makuu!
Ukiachilia utafutaji wa mtoa huduma kuwa wa tabu pia unapompata huyo mtoa huduma anakuhudumia kana kwamba yeye ndiye aliyekupigia bila kujali kwamba wewe ndiye uliyepiga na huna salio la kutosha na ikitokea simu yako ikakatika pasipo kumaliza tatizo lako hata hawasumbuki kukupigia wakiamini lazima utaweka vocha na kuwapigia tu...
Kuna hili nalo mteja anayekuhudumia unamwambia tatizo lako,inaonyesha uelewa wake mdogo shortcut anaona ni kukwambia ubebe king'amuzi chako na kukipeleka katika ofisi zao,ambapo tatizo hilo linaweza likaelekezeka kwenye simu na tatizo likaisha..
Mbaya kupita zote ni hili la namba za Customer Care kutokuwa hewani muda wa kazi tena inaweza ikawa zaidi ya wiki moja hili ni tatizo!
Kwa leo ni hayo tu!

MUSTAPHA HANYA
mustaphamadish@gmail.com
+255 789 476 655
Share:

Mar 9, 2016

KIFURUSHI CHA ZUKU SMART PACK | TSH 8,999


 Habari njema kwa wateja wa zuku na wale wanaotaka kujiunga na zuku tv ni hii hapa:-
Kwa tsh 8,999
Unapata kuona channel za tv 30
Radio 18
+ Local channel

Punde nitawawekea channel zilizopo....!!

Ukitaka kujua vifurushi vingine vya zuku tv BOFYA HAPA
Share:

Feb 25, 2016

OFFER YA DSTV UKINUNUA UNAPATA...


Je unahitaji kujiunga na DStv hii itakuwa inakufaa zaidi kwa maana hapatakuwa na kisingizio tena ipo hivii:-
Kama unahitaji kujiunga kwa maana kununua ni tsh 79,000/= bila ufundi ila ndani yake kuna kifurushi cha Compact sijui nimeeleweka hapa!!??
Na kwa wale wateja wa zamani ukinunua kifurushi cha Compact kwa tsh 84,500 utapata kuona mpira live nazungumzia EPL,LALIGA na EURO 2016!
kutaka kujua vifurushi vingine vya DStv usiwe mvivu  Bofya Hapa
Share:

Feb 17, 2016

VIFURUSHI VYA CONTINENTAL DECODER


Yawezekana mpaka sasa kwenye king'amuzi chako cha Continental channel zipo ila huoni picha kila ukibadili unakutana na kialama cha $ maana yake mpaka ulipie ehee tunalipiaje:-
Mteja wa continental. Kulipia kumeanza tarehe 15 February 2016, baada ya kutokuwa na malipo kwa muda wote toka kiwe hewani. Lipia king'amuzi chako cha continental kuendelea kupata channels za continental ambapo channel za nyumbani zote ni bure hata usipolipia.
Vifurushi, Siku 7 @3,999/= , Siku 15 @6,999/= , Siku 31 @11,999/= .
 Continental Decoder The quality to talk about
 Kwa Maelezo zaidi +255789476655
Share:

Feb 10, 2016

BEI MPYA YA VIFURUSHI VYA ZUKU

Kuanzia tarehe 01/03/2016 malipo ya vifurushi vya zuku itapanda kutokana na sababu za kimaboresho kwa mujibu wa Zuku!
Tsh 10,000/= kifurushi kipya Bofya Hapa
Ambapo kifurushi cha Classic kitakuwa tsh 18,000/= badala ya tsh 15,000/= iliyopo sasa!
Kupata kujua channel zilizopo kwenye kifurushi cha Classic Bofya hapa
Alkadharika kifurushi cha Premium kitakuwa tsh 25,000/= badala ya tsh 22,500/= iliyopo sasa!
Kupata kujua channel zilizopo kwenye kifurushi cha Premium Bofya Hapa
Share:

Feb 9, 2016

UNATAKA KUNUNUA AZAM TV!!??


Yapata wiki ya pili sasa kwa wale wauzaji king'amuzi cha Azam tv kimekuwa adimu kutokana na mzigo kutokuwepo makao makuu ya Azam,ingawaje taarifa zilizotoka ilikuwa jumatatu ya tarehe 8/2/2016 mzigo ungekuwa umeshafika na kuanza kuuzwa kwa mawakala na wateja pia ila hali imekuwa tofauti kutokana na sababu zilizo nje ya kampuni ingawaje jitihada za haraka zinaendelea kufanyika!

Hali hii imepelekea kwa wale mawakala/wafanya biashara tu wanaouza kwa kusua sua kipindi ambacho king'amuzi kina kuwa adimu wao bado wanavyo na matokeo yake wanauza bei juu tofauti na bei stahiki,hii ni kwa Dar na nje ya Dar pia!

Ninachoweza kuwasihi wateja wote wanaohotaji kujiunga na Azam tv waendelee kuwa na subira,mpaka jumatatu ya tarehe 15/2/2016 king'amuzi cha azam kitakuwa kinapatikana kwenye zile sehemu zinu zote,ingawaje juhudi zinazofanyika zikifanikiwa hata kabla ya jumatatu kitaanza kuuzwa! Wale waliopiga simu kama ambavyo wameahidiwa baada ya kuacha mawasiliano yao kwamba watafahamishwa pindi tu uuzwaji utakapoanza nasi tutafanya hivyo bila shaka na wale ambao bado wapo njia panda piga no.+255 789 476 655 kisha acha mawasiliano yako kisha utafahamishwa pindi tu uuzwaji utakapoanza! Kwa wale wa Dar es salaam unaweza kuletewa mpaka ulipo na kufungiwa kisha unalipia!
Kujua vifurushi vya Azam tv Bofya Hapa
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita