Call / WhatsApp +255673378129

Jul 22, 2015

HOTEL TV SYSTEM INSTALLATION

TV INSTALLATION
Mapendekezo ni ya mteja kwa maana mmiliki wa hotel/sehemu yeyote husika 
kwamba tv zikae ukutani ama mezani,kazi yetu ni kutoa ushauri kwa jinsi mazingira yalivyo,je muonekano mzuri ni upi tv kukaa mezani ama ukutani? ingawaje mara nyingi tv kukaa ukutani ndo huwa zinapendeza na salama pia.

CHANNELS INSTALLATION
Tunatoa nafasi kwa muhusika kusema channel anazotaka ambazo angependa kuziona zinapatikana,pia tunatoa ushauri kwa channel atakazo kama zimejitosheleza ama kuna umuhimu wa kupunguza ama kuongeza kutokana na uzoefu tulionao tunajua mapenzi ya wateja wengi wa hotel/office n.k. kwa channel zinazopendwa sana!
- Control room
Hapa tunahifadhi channel zote tunazohitaji,kisha tunazisambaza kwenye tv zote zilizopo kwa ubora mmoja nikiwa na maana quality ya picha ni moja kwa tv zote hata zikiwa 100.

- Remote Control
Kwa kila tv iliyopo kwa kila chumba itajitegemea kubadili channel kwa kupitia Remote ya tv husika bila kumbugudhi anayeangalia tv nyengine.

PROJECTOR INSTALLATION
Kama ilikuwa hujui Projector inatengenezwa kwa masaa maalum,nikiwa na maana ya kuwa mathalani projector imetengezwa  itumike kwa masaa matano ( 5 ) yakitimia masaa matano hakuna njia ya kurenew yale masaa kwa lugha nyepesi itakulazimu ununue projector nyengine.Tupo kwa ajili ya kutoa ushauri na kukufungia pia popote panapostahili.

REPAILING
Inapotokea unakutana na ujumbe mmojawapo kati ya hii ifuatayo jua ya kuwa fundi anahitajika,inaweza kuwa kiushauri ama kiufundi zaidi kwa fundi kufika eneo husika.Ila kwa ushauri wa awali angalia cable yako ipo sawa? angalia je connector yako imekaa sawa? kwa upande wa Receiver/Decoder/tv ama kutoka kwenye Dish ama chanzo chochote cha channel!
- Bad Signal
- Signal Weak
- No Signal
- No Channel
- No Program
- No Service
- Searching for Signal

BAADHI YA KAZI ZA HOTEL TULIZOFANYA:-
- Bahari Lodge
- JB Belmont
- Geraffe View Hotel
- Transit Motel

UZOEFU:-
Yapata miaka nane ( 8 ) Mustapha MaDish nimejikita ukanda huu,nafunga Dish Antenna aina zote kwa channel za bure na kulipia,nadeal na receiver/decoder aina zote,nina team kazi yenye vijana wenye uzoefu unaozidi miaka miwili kwenye taaluma ya ufundi.
Nimefundisha vijana wapatao 17 ambao kwa sasa wanaendesha maisha yao kupitia taaluma hii wengine wakiwa wameajiriwa Multichoice Tanzania ( DStv ) na wengine makampuni mengine.
Najua kiundani kuhusu ving'amuzi vyote vilivyopo Tanzania.


UNA SWALI..?
UNAHITAJI HUDUMA..?
MSAADA ZAIDI..!
PIGA SIMU +255 784378129

Share:

Jul 21, 2015

MBUYU TWITE | AZAM TV & DSTV


Baraka za mikono salama,kazi nzuri kwa wengine imefanya nifike kwa huyu jamaa tegemezi la timu ya young African Mbuyu Twite,tumefunga DSTV na AZAM TV pia!


+255789476655
Share:

Jul 18, 2015

UPO FACEBOOK !!!???



Je blog yetu imekusaidia kwa kiasi fulani,kwa kukupatia maelezo kwa wakati na kwa kina kuhusu ving'amuzi bila kuchagua ama je blog yetu imekusaidia kukuwezesha kupata huduma ya kununua na kufungiwa king'amuzi kwa wakati? Ama imekusaidia kupata mafundi wa kukufungia king'amuzi chako kwa ubora stahiki!
Una maoni yeyote ili tu tuweze kufanya vizuri zaidi ama una la kutukosoa pale tulipoteleza!?
Tupo hapa kupokea yote bila kubagua lolote kwetu ni msaada wa kutufikisha tunapofikiri!
Swali langu je upo FACEBOOK !? kama ndivyo Bofaya Hapa kisha like page yetu ili uweze kuwa miongoni mwa wadau wetu watakaopata chochote kipya kuhusu king'amuzi kwa wakati ama pia waweza kutuandikia chochote na tukakifanyia kazi kwa wakati hata kama haitakuwa umepiga simu.

Share:

Jul 15, 2015

KING'AMUZI KITAKACHOONYESHA KOMBE LA KAGAME 2015

Ni kiu ya wapenzi wengi na maswali yakiwa yanazidi kila kukicha ya kuwa ni king'amuzi gani na kifurushi gani kitaonyesha CECAFA 2015 kombe la Kagame.
Wala nisikupotezee muda jibu ni DStv.
Kama utalipia kifurushi cha Compact Plus utaweza kuona hizi mechi kwa raha bila kukosa hata moja ikiwa live bila chenga!
Na hii ndio ratiba ya mechi:-

Date:18-Jul-15
APR vs Shandy
13:30
SS9 / Select 2

Date:18-Jul-15
Yanga vs Gor Mahia
15:55
SS9 / Select 2

Date:19-Jul-15
Adam City vs Malakia
13:30
SS9 / Select 2

Date:19-Jul-15
Azam FC vs KCCA
15:55
SS9 / Select 2

Date:20-Jul-15
Telecom vs Khartoum-N
13:30
SS9E / Select

Date:20-Jul-15
Gor Mahia vs KMKM
15:55
SS9E / Select

Date:21-Jul-15
Shandy vs LLB AFC
13:30
SS9E / Select

Date:21-Jul-15
Hegaan FC vs APR
15:55
SS9E / Select

Date:22-Jul-15
KCCA vs Adam City
13:30
SS9E / Select

Date:22-Jul-15
Telecom vs Yanga
15:55
SS9E / Select

Date:23-Jul-15
Hegaan FC vs Shandy
13:30
SS9E / Select

Date:23-Jul-15
APR vs LLB FC
15:55
SS9E / Select

Date:24-Jul-15
Khartoum-N vs Gor Mahia
13:30
SS9E / Select

Date:24-Jul-15
KMKM vs Yanga
15:55
SS9E / Select

Date:25-Jul-15
KCCA vs Malakia
13:30
SS9 / Select 2

Date:25-Jul-15
Adam City vs Azam
15:55
SS9E / Select 2

Date 26-Jul-15
Gor Mahia vs Telecom
13:30
SS9E / Select 2

Date 26-Jul-15
Yanga vs Khatoum-N
15:55
SS9E / Select 2

Date 28-Jul-15
Q/Final 1 (B1 vs A3)
13:30
SS9E / Select

Date 28-Jul-15
Q/Final 2 (A1 vs Best Qualifier)
15:55
SS9E / Select

29-Jul-15
Q/Final 3 B2 vs C2
13:30
SS9E / Select

29-Jul-15
Q/Final 4 C1 vs A2
15:55
SS9E / Select

31-Jul-15
S/Final 1 (w-qf3 vs w-qf4)
13:30
SS9E / Select

31-Jul-15
S/Final 2 (w-qf1 vs w-qf2)
15:55
SS9E / Select

02-Aug-15
3rd and 4th Play-off
13:30
SS9E / Select

02-Aug-15
Final:
15:55
SS9E / Select

Mechi zote zitaonyeshwa live!

MSAADA +255789476655
ZINGATIA:muda wa kupiga simu ni saa 08:00 asubuhi - saa 20:00 usiku.
Share:

Jul 1, 2015

DSTV IMESHUKA TSH 79,000= BILA UFUNDI!


Kwa wateja wapya hii inawahusu sana,muda ambao mamlaka ya mapato tanzania imepandisha bei ya kodi kwenye $,jambo lililopelekea pia kupanda kwa gharama za malipo ya mwezi ya vifushi vya ving'amuzi vyote.
Kwa kulizingatia hilo Multichoice Tanzania imeonelea ipunguze gharama za kununua king'amuzi,kwa tsh 79,000 tu unapata Vifaa vyote ikiwa kama Dish,Decoder,cable,n.k. bei hii inakuwa haina ufundi wala kifurushi.
Ili ufungiwe itakulazimu kulipia tsh 30,000,pesa hiyo licha ya kufungiwa pia itakulinda kwa muda wa miezi mitatu kama litatokea lolote la kiufundi,fundi atakuja kwako kuangalia tatizo bila malipo yeyote.
Baada ya hapo unachagua vifurushi kati ya vifuatavyo kisha unalipia ili uweze kupata channel zilizo bora kabisa!

1-DSTV BOMBA PACKAGE
Ina channel 65+ bora
Bei mpya ni Tsh 19,950
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

2-DSTV FAMILY PACKAGE
Ina channel 70+ bora
Bei mpya ni Tsh 42,900
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

3-DSTV COMPACT PACKAGE
Ina channel 85+ bora
Bei mpya ni Tsh 82,250
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

4-DSTV COMPACT PLUS PACKAGE
Ina channel 90+ bora
Bei mpya ni Tsh 122,500
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

5-DSTV PREMIUM PACKAGE
Ina channel 120+ bora
Bei mpya ni Tsh 184,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

KAMA UNA TATIZO LA KIUFUNDI AMA HUDUMA KWA WATEJA Bofya hapa

ZINGATIA:Muda wa kupiga simu ni saa 08:00 asubuhi - 20:00 usiku.

PIGA SIMU +255789476655 | mustaphamadish@gmail.com


Share:

Jun 26, 2015

AZAM TV BEI MPYA TSH 135,000/= BILA UFUNDI!


Ingawaje mikoani na sehemu nyingi tu bado wanauza bei wanazojua wao ila bei elekezi ni tsh 135,000 tu,hii inakuwa bila kifurushi wala ufundi!
Ili ufungiwe itakulazimu kulipia tsh 30,000 tu,ambao itakulinda kwa muda wa miezi mitatu na ikitokea ikasumbua fundi atakuja kumaliza tatizo bila gharama yeyote.
Bei ya zamani ya offer ilikuwa tsh 99,000/= ambapo sasa haipo tena.
Bei mpya ni Tsh 135000 utapata Dish,Decoder,Cable,n.k
baada ya kununua ili uweze kuona itakulazimu kuchagua na kulipia moja ya vifurushi vifuatavyo:-
1.AZAM PURE PACKAGE
Ina channel 25+ bora
Bei mpya tsh 12,000/=
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

2.AZAM PLUS PACKAGE
Ina channel 50+
Bei mpya tsh 20,000/=
Bofya Hapa kujua channel zilizopo katika kifurushi hiki!

3.AZAM PLAY PACKAGE
Ina channel 80+
Bei mpya tsh 25,000/=
Bofya Hapa kujua channel zilizopo katika kifurushi hiki!

4.AZAM SPORTS Add-On 
Ina channel 4 tu.
Bei tsh 15,000/=

5.INDIAN Add-On
Ina channel 15+
Bei tsh 6,000/=

6.INDIAN Bouquet
Ina channel 23+
Bei tsh 16,000/=


ZINGATIA:Muda wa kupiga simu ni kuanzia saa 08:00 asubuhi - 20:00 usiku.
MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA | CHOCHOTE KUHUSU AZAM TV | +255789476655
Share:

Jun 19, 2015

RAMADHANI KAREEM


Tumeanza mwezi,mwezi ambao kwetu sisi waislamu una maana kubwa sana kwa haraka haraka tu huu ndio mwezi ambao quraan tukufu ndio ilishushwa mwezi huu na kwa uchache zaidi ndio mwezi ambao mwenyezi mungu anatusamehe dhambi zetu tulizonazo na tutakazokuwa nazo,ni mwezi ambao sio ombi bali ni lazima kwa kila aliyejaaliwa kufunga maana yake ni kwamba kama huna tatizo lolote kiafya litakalokufanya ushindwe kufunga ni lazima kufunga..
Mwezi huu unatukumbusha kuacha yale yote ambayo mwenyezi mungu ametukataza kama kuzini,kusengenya,kuongopa,kuiba,nk pia tunakumbushwa kwa nguvu zote kufanya yale tunayostahili kufanya kwa imani zetu kama kuswali,kutoa sadaka na kwenda hija kwa walio na uwezo..
Tunafundishwa kufunga na kuswali,kufunga bila ya kuswali sawa na hakuna funga..
Kuna mengi ya kufanya ili funga zetu zikubalike ijapokuwa vijana wana misemo yao kuwa swaumu za mjini zina kazi ila ukitia nia unafunga bila wasi na kumuachia mungu ndiye mwenye kujua umefunga ukiwa sahihi ama lakini kwa kuzingatia misingi yote ya funga.
Ugumu wa vijana wengi katika mwezi huu ni kutamani,sio kula laa kwakuwa katika maisha ya kawaida ya watanzania wengi ni swaumu,ila linawashinda la kuatamani kufanya ngono.
Kuona ndoa nyiingi inapofikia kipindi cha kuelekea mwezi mtukufu ni jibu tosha la nini ambacho namaanisha,sasa kwa ninyi msiooa ama kuolewa swaumu kwenu zikoje!!???
Zaidi ya yote funga njema wapendwa mkumbuke kuswali na kutoa swadaka!

Share:

Jun 18, 2015

LOADING...


Nilichogundua karibu ving'amuzi vyote vina mapungufu na hii inatokana na kujisahau,wafanyakazi kufanyakazi bila juhudi binafsi wanafanya ile bora liende mwisho wa mwezi tukinge,pia makampuni yenyewe husika hayajajipanga katika baadhi ya mambo ili kukabiliana na ushindani uliopo.
Kwa kulitambua hilo tunakuja kuwa mfano kwa makampuni yote ya ving'amuzi ili kuleta changamoto kwa makampuni yaliyolala kuweza kuamka na kutoa huduma stahiki kwa wateja wao..
Tunakuja...
Kaa tayari kutupokea..
Share:

Jun 16, 2015

BEI MPYA YA MALIPO YA MWEZI AZAM TV


Burudani kwa wote..
Kwa mujibu wa Azam tv bei za vifurushi zimepanda kutokana na ungezeko la kodi,
hivyo kile kifurushi cha tsh 10,000/= kimekuwa tsh 12,000/=
kifurushi cha 15,000/= kimekuwa tsh 20,000/=
na kifurushi cha 20,000/= kimekuwa tsh 30,000/=
Pia siku za usoni kinakuja kifurushi kipya ambacho kitakuwa na channels za india tu,
hivyo ili uzione channel za india itakulazimu ulipie kifurushi hicho kipya lakini kwa kipindi hiki ni bure mpaka hapo ambapo itatangazwa.
Kujua channel zilizopo Bofya Hapa
Mambo yote ya kiufundi Azam tv piga : +255789476655

Share:

Jun 10, 2015

VIFURUSHI VYA TING | TING PACKAGES


Hivi ndivyo vifurushi vilivyopo na bei zake kwenye king'amuzi cha Ting kwenye Antenna na kwenye Dish!
1.REGULAR PACKAGE
Inachannel 12+ safi
Malipo ni Tsh 11,000/=
Kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
Package hii ni kwenye Antenna tu!
2.CLASSIC PACKAGE
Ina channel 30+ safi
Malipo ni Tsh 22,000/=
Kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
Package hii ni kwenye Antennatu!
1A.REGULAR PACKAGE
Ina channel 25+ safi!
Malipo ni Tsh 16,000/=
Kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
Package hii ni kwenye Dish tu!
2A.CLASSIC PACKAGE
Ina channel 50+ safi!
Malipo ni Tsh 24,000/=
Kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
Package hii ni kwenye Dish tu!
Kwa maelezo Zaidi piga +255789476655

Share:

Jun 9, 2015

KUNUNUA KING'AMUZI CHA ZUKU TV TANZANIA

Remote ya Zuku
Ili kutoa fulsa ya kila mtu aweze kununua kinga'amuzi cha Zuku Tv imeonelea kushusha bei,ambapo sasa ili kununua zuku itakulazimu kulipia Tsh 88,000 tu,badala ya Tsh 95,000/= ila hii inakuwa bila ufundi.
Ili ufungiwe itakulazimu kulipia Tsh 30,000 tu,pesa hii itakulinda ndani ya miezi mitatu kwa lolote likitokea fundi atahusika bila gharama yeyote ya ziada.
Baada ya hapo unachagua Kifurushi kati ya vifurushi vifuatavyo,ingawaje kwa mwezi wa kwanza unapata kifurushi bure!

1-ZUKU SMART PACK PACKAGE
Ina channel 36 safi.
Malipo ni Tsh 8,999
kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

2-ZUKU SMART PLUS PACKAGE
Ina channel 40 safi.
Malipo ni Tsh 13,000
 kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
3-ZUKU CLASSIC PACKAGE
Ina channel 69 safi.
Malipo ni Tsh 18,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

4-ZUKU PREMIUM PACKAGE
Ina channel 98 safi.
Malipo ni Tsh 25,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

5-ZUKU ASIA PACKAGE
Ina channel 26 safi.
Malipo ni Tsh 24,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!
ZINGATIA:Muda wakupiga simu ni saa 08:00 - saa 20:00 usiku.

Ili Kununua | Kupata Mafundi | Msaada 
Piga +255714973797
Share:

May 18, 2015

KWANINI TUMELAZIMIKA KUIGIA DIGITAL NA KUACHANA NA ANALOGUE?


Mabadiliko katika mfumo wa utangazaji kutoka mfumo wa analojia kwenda katika mfumo wa dijitali ni utaratibu ambao unaendelea ulimwenguni kote. Mabadiliko haya yanatokana na makubaliano ya nchi wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa lenye dhamana ya masuala ya mawasiliano yaani International Telecommucations Union yaliyofanyika mwaka 2005 huko Geneva, Uswisi. Makubaliano ya nchi wanachama ni kuzima kabisa matangazo katika mfumo wa analojia na kutumia mfumo wa utangazaji wa dijitali ifikapo tarehe 17 Juni 2015. 

Ili kuhakikisha mabadiliko haya yanafanyika kwa ufanisi, tija na pia kutoa muda wa kutosha wa kutekeleza mabadiliko haya, mwaka 2005 Serikali ilianza mchakato wa uhamaji kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda dijitali ambao ulihusisha wadau wote, wakiwemo wamiliki wa vyombo vya habari na vituo vya utangazaji wa televisheni, hatua kwa hatua, hadi kuridhia ratiba nzima ya uzimaji wa mitambo ya analojia. Kwa kifupi mchakato wa uhamaji ulipitia hatua zifuatazo:

Mwaka 2005:   Waraka wa kwanza wa mashauriano (consultative document) kuhusu umuhimu na faida za kuhama kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda dijitali ulitayarishwa na kusambazwa kwa wadau wote;

Mwaka 2006:   Waraka wa pili wa mashauriano na mapendekezo ya muundo wa leseni kwenye mfumo wa utangazaji wa teknolojia ya dijitali ulitayarishwa na kusambazwa kwa wadau wote;

Mwaka 2007:   Kamati ya kiufundi inayoshughulikia uhamaji kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda dijitali iliundwa;

Mwaka 2007:   Mkutano mkuu uliojumuisha vituo vyote vya utangazaji nchini ulifanyika Bagamoyo kupitisha maazimio ya mfumo wa leseni za utangazaji utakaotumika kwenye mfumo wa dijitali;

Mwaka 2010:   Kampuni tatu (3) zilipewa leseni za ujenzi wa miundombinu ya utangazaji ya dijitali. Kampuni tatu zilizopewa leseni za kusambaza matangazo ya dijitali ni Agape Associates Limited, Basic Transmission Limited, na Star Media (T) Limited. Kampuni hizo zilipewa leseni baada ya kuthibitisha kuwa zina uwezo wa kujenga miundombinu ya kurushia matangazo katika mfumo wa dijitali;

Mwaka 2010:   Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu Mabadiliko ya Utangazaji toka mfumo wa analojia kwenda dijitali iliundwa. Kamati hii hukutana kila baada ya miezi mitatu kutathmini maendeleo ya ubadilishaji wa mfumo wa utangazaji;

Mwaka 2011:   Kampeni ya Kitaifa ya kuelimisha umma kuhusu mabadiliko ya mfumo wa utangazaji ilizinduliwa rasmi na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa Tanzania rasmi nchi nzima mwisho wa kutumia mfumo wa Analogue ni tarehe 31/12/2014 saa 23;59.
Tukahamia mfumo wa Digital,ambao huu wa ving'amuzi tulionao ijapokuwa ilikuwa mwisho ni tarehe 17/06/2015,kuhama mapema ni namna ya kuangalia je kuna changamoto gani na vipi wahusika wanakabiliana nazo.

+255789476655
Share:

May 11, 2015

VING'AMUZI VINAVYOCHUANA | AZAM TV & DSTV | KIPI NI ZAIDI!?


Dstv ni wakongwe hii haina ubishi,ila ukongwe wa dstv haina maana kuwa hakuna king'amuzi ambacho kinaweza kuja na kufanya vizuri zaidi yake,hii inatokana na kwanza kujua mahitaji ya watazamaji kwa ujumla na kuwatimizia kile wanachokihitaji,unafuu wa bei ukizingatiwa.
Azam tv ni king'amuzi kipya kati ya vyote unavyoviona ila ndio king'amuzi kinachokimbizana na wakongwe,kwanini? kwasababu wameangalia watazamaji wanataka nini na kwa unafuu pia..Ingawaje Azam tv haijakidhi mahitaji wa wadau kwa 100% lakini alau wameweza kwa ukubwa.
Wadau wengi ni wapenzi wa mpira hivyo Azam tv wamefanikiwa kwa mpira wa Tanzania na Dstv bado anang'ang'ania ukongwe wake kwa mpira wa nje.
Ving'amuzi hivi vina mapungufu yake na kinachowakera wengi ni haya hapa:-

MAPUNGUFU YA DSTV
-Kubwa linalolalamikiwa na watanzania wengi ni bei kuwa juu,nikimaanisha malipo ya mwezi na hii inachangia na mtindo unaotumika wa kutumia $ badala ya Tsh.
Madhara ya kuwa bei juu kumefanya wadau watafute kila aina ya njia kuona wanapata uhondo wa dstv ila kwa njia isiyo rasmi,na hii inapelekea kupunguza walipaji halali wa malipo ya mwezi.
-Wana local channel,lakini malipo ya mwezi yanapokata hawaziachi zikawa bure.
Hayo ni mapungufu makubwa kwa Dstv.

MAPUNGUFU YA AZAM TV
-System wanayotumia kushindwa kutambua malipo ya mwezi wanayolipia wateja na kufunguka badala yake ukilipia kifurushi ukipendacho mpaka upige simu,hii imekuwa kero kwa wateja wengi wa azam tv,mteja anakaa mpaka wiki mbili na ikitokea hapigi simu unapita mwezi pasi kuona kile kifurushi alicholipia.
-Mawakala na wauzaji wengine wasio mawakala kuuza bei tofauti na bei sahihi.Hii sio tu mikoani ijapokuwa mikoani lawama hizi ni kubwa lakini hata hapa Dar es salaam wapo wanaouza bei juu tofauti na matangazo yalivyo.
-Picha kupotea kipindi cha mvua,king'amuzi ambacho kinaongoza kwa kupotea signal wakati wa mvua ndogo tu,hii ni kero nyengine kubwa kwa wateja wa Azam tv,kitaalamu hii inatokana na signal kuwa chini hivyo ni jukumu la Azam tv kuongeza signal badala ya 60 zifike alau 80 lakini kinachotakiwa mfikishe 100.
Hayo ni mapungufu makubwa kwa Azam tv.
TOFAUTI KUBWA KATI YA DSTV & AZAM TV
Dstv ana huduma zaidi ya moja kama:-
Extra view-Inakuwezesha kuona channel mbili tofauti kwa tv mbili tofauti kwa a/c moja.
Explora-Inakupa fulsa ya kurecodi saa 150 na mengineyo.
Umiliki na utofauti wa channel.
Dstv inaonyesha mpira wa nje na Azam tv mpira wa ndani.

MUSTAPHA MADISH | +255789476655 | mustaphamadish@gmail.com
Share:

May 1, 2015

STAR TV | AZAM TV | PAMOJA SASA

Awali ilikuwa ili kupata Star tv kwenye king'amuzi cha Azam ilikuwa ni fundi na ufundi wetu tu,kwani ilikuwa tunafunga satellite mbili kwa wakati mmoja ila baadae wenye mali yao hapo Satellite ya Amos 5 wakafanya ya kufanya.
Baada ya vuta nikuvute hatimae sasa Star tv imeungana na Azam tv,hivyo jambo hili limepelekea kila mmiliki wa king'amuzi cha Azam alipokee kwa furaha,huku wale ambao walikuwa wanasita kujiunga na Azam kwasababu hakuna Star tv huu ndo wakati wenu labda mseme lengine.

+255789476655 | HUDUMA ZA AZAM TV
Share:

Apr 27, 2015

MVUA NA VING'AMUZI VYETU


Kwa kawaida mvua inapokuwa inanyesha watu wengi nami nikiwa mmojawapo huwa mapenzi yapo kukaa sehemu tulivu kama panaruhusu unaangalia tv,iwe ni movie ama vyovyote vile ijapokuwa mimi mapenzi yangu kuangalia movie...
Ikiwa una king'amuzi chako na unataka kuangalia huku ukipisha mvua ifanye yake kisha uendelee na ratiba zako..King'amuzi nacho kinagoma kutoa picha..Mvua inaponyesha ving'amuzi vinavyotumia dish ndogo huwa vinaelemewa ila inapokata mvua navyo vinaonyesha picha kama kawaida..Unadhani ni kwanini vinaelemewa? Fuatana nami..






Share:

Apr 14, 2015

VING'AMUZI VYA ANTENNA


EASY TV
King'amuzi cha kwanza cha antenna ambacho mpaka sasa kipo ila kiukweli kama wanasua sua na kujikuta kila kukicha wanapoteza wateja badala ya kuongeza wateja.
Sababu ya king'amuzi hiki kupoteza wateja kila kukicha ni kutokana kukosa kuwapa uhakika wateja wao na wale wateja wapya,ambapo hata huduma zitolewazo kama zina usiri matokeo yake kimekuwa king'amuzi ambacho hakijulikani na watanzania wengi,pia kingine kinachowakimbiza wateja ni namna channel zinavyopungua kila kukicha ijapokuwa kuna ambazo zinaongezeka!
Pamoja na hayo yote malipo ya mwezi ni  tsh 10,000/= toka walipoanza mpaka sasa.


STARTIMES
Katika zile mbio za kuingia katika mfumo wa digital,ndipo kikazaliwa king'amuzi hiki ambapo kuna ushirikiano kati ya tanzania na china,hivyo kwa lugha nyepesi hiki ndicho king'amuzi cha TBC na hiki ndicho king'amuzi pekee unachoweza kupata TBC2.
Ingawaje king'amuzi hiki kilianza katika mfumo wa transmeter kwa lugha nyepesi kutumia antenna lakini sasa wameingia kwenye mfumo wa satellite pia mfumo wa dish hivyo kuwa ni kati ya vile ving'amuzi vichache vinavyotumia antenna na dish pia ila kwa decoder tofauti.

TING
Hiki king'amuzi ni mali ya taasisi ya dini,sababu hiyo imepelekea kuwa na idadi ya channel nyingi za dini zikiwemo za ndani na nje ya nchi.
Ingawaje nacho kilianza na antenna lakini baadae kikaongeza kutumia mfumo wa dish,hivyo kuna decoder aina mbili za antenna na za dish pia.

DIGITEK
Kulikuwa na  ile kila kampuni inayomiliki vituo vya tv kutaka kumiliki ving'amuzi vyao,na hii ilipelekea watanzania kuongea saana kwamba tutanunua ving'amuzi vingapi ila kuna baadhi ya makampuni wakaachana na habari hiyo ila makampuni mengine yakatimiza azma yao na katika kuthibitisha hili kikazaliwa king'amuzi hiki,
Ambacho walifanya hawakuwa na malipo ya mwezi,ilikuwa ukinunua wewe ni kutumia tu ambapo mpaka sasa.
King'amuzi hiki kikapotea,vilikuwa vimeisha huku fununu zikiwa wanaleta ving'amuzi vya kutumia satellite kama vilivyo ving'amuzi vyengine,kweli hatimae wakatoa decoder zenye uwezo wa kusoma antenna na dish.

CONTINENTAL
Katika kule kila kampuni kumiliki king'amuzi chake,star tv wameingia kwenye orodha hiyo kwa kumiliki king'amuzi hiki.Ambapo kumezaa star tv zaidi ya moja kama star bunge,star music na nyenginezo ilihali kuleta tofauti na ving'amuzi vyengine na kuongeza umuhimu kwa watazamaji.
Antenna ilihusika sana huku wakiwa hawana malipo ya mwezi kama digitek,ilifikia hatua wakahitaji kubadili ule mfumo waliokuwa wanautumia katika kurusha matangazo yao hivyo iliwalazimu kupotea hewani huku wateja wao wasijue siku watakayorejea.
Sasa wapo hewani,wapo hewani huku wakiwa wameingia katika ule mfumo uliotazamiwa na wengi ambapo hivi sasa wanatumia Antenna na Dish pia.

VING'AMUZI VYOTE HIVI VINAINGILIANA ANTENNA
Nimejaribu kutumia picha ya antenna moja kwa ving'amuzi vyote kwa kuwa unaweza ukatumia antenna hiyo kwa ving'amuzi vyote bila shida!
Kuna baadhi ya maeneo unaweza ukatumia antenna ya ndani na ukapata picha vizuri tu ila kuna maeneo ni lazima uweke antenna ya nje na bomba lako liwe refu pia.



KUNUNUA KING'AMUZI | MAFUNDI | USHAURI | +255789476655

Share:

Apr 9, 2015

BEI MPYA ZA MALIPO YA MWEZI DSTV

Ikiwa wadau wapo katika kulala na kuomba angalau gharama za malipo ya mwezi zipungua,hali imekuwa tofauti kutokana na gharama za uendeshaji ambapo imepelekea kupanda kwa bei za malipo ya mwezi kwa vifushi vyote vya Dstv kama ifuatavyo:-

BOMBA PACKAGE 
Awali ilkuwa tsh 18,500
Ikabadilika na kuwa tsh 23,500
Ikabadilika tena na kuwa tsh 19,975
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 19,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

FAMILY PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 40,000
Ikabadilika na kuwa  ths 51,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 42,900
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 39,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

COMPACT PACKAGE
 Awali ilkuwa tsh 66,000
Ikabadilika na kuwa  ths 84,500
Ikabadilika tena na kuwa tsh 82,250
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 69,000
kitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

COMPACT PLUS PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 113,000
Ikabadilika na kuwa  ths 147,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 122,500
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 109,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa

PREMIUM PACKAGE
Awali ilkuwa tsh 199,000
Ikabadilika na kuwa  ths 219,000
Ikabadilika tena na kuwa tsh 184,000
Ambapo sasa hii 2017 ni  Tsh 169,000
ukitaka kujua idadi na channel zilizopo Bofya Hapa


HUDUMA ZA DSTV | MSAADA KIUFUNDI | +255789476655

Share:

Mar 27, 2015

VIFURUSHI VYA AZAM TV | AZAM TV PACKAGES


Awali hakukuwa na mfumo huu wa vifurushi ila kutokana na uendeshaji na kutafuta maboresho imepelekea kuanza mfumo huu wa vifurushi,katika kumbukumbu za wengi ndicho king'amuzi kilichokuwa quality,channels nyingi ila malipo ya mwezi ni madogo!
Hivi ndivyo vifurushi vya azam tv,idadi ya channel na bei:-

1.AZAM LITE PACKAGE
Ina channel 40+ bora
Malipo ni Tsh 10,000/= kwa mwezi
Malipo ni Tsh 3,000/= kwa wiki
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

2.AZAM PURE PACKAGE
Ina channel 60+ bora
Malipo ni Tsh 18,000/=
Malipo ni Tsh 7,000/= kwa wiki
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

3.AZAM PLUS PACKAGE
Ina channel 90+
Malipo ni Tsh 23,000/=
Bofya Hapa kujua channel zilizopo katika kifurushi hiki!

4.AZAM PLAY PACKAGE
Ina channel 105+
Malipo ni Tsh 28,000/=

MSAADA - KIUFUNDI | KUNUNUA | CHOCHOTE KUHUSU AZAM TV | 
+255 789 476 655
Share:

Mar 20, 2015

BEI ZA VING'AMUZI NJE YA DAR ES SALAAM

Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu kuhusu bei za ving'amuzi katika mikoa yote ukiacha dar es salaam ijapokuwa baadhi ya wauzaji wa dar es salaam hili linawahusu!
Hapa nazungumzia ving'amuzi vyote vilivyopo tanzania,kampuni husika wanatoa bei elekezi ambapo bei hiyo inapaswa kuuzwa kwa mikoa yote tanzania bila kuongeza hata senti 5.
Unaweza ukaona ni jambo ambalo haliwezekani ila mimi najua ya kuwa inawezekana kama muuzaji ni wakala aliyeidhinishwa na kampuni hhusika.
Mfano wakala anaponunua azam tv kwa jumla anapata punguzo maalum na kuna utaratibu wa kurudishiwa pesa ya usafiri kwa kuzingatia mkoa gani anatoka,pia ving'amuzi vyengine wanautaratibu wao unaofafana na huo ili tu kufanikisha mawakala wote katika mikoa yote waweze kuuza bei elekezi na si vinginevyo!
Kinachotokea kutokujulikana kwa mawakala walioidhinishwa kwa baadhi ya mikoa kumesababisha wafanyabiashara kujiamulia kununua tu ving'amuzi na kuweka kwenye maduka yao na kujiuzia bei wanazotaka wao huku wakiwa hawajui vema kuhusu hivyo ving'amuzi,hii imepelekea malalamiko kuwa mengi kwa mteja kuchelewa kufunguliwa ili aweze kuona ama chochote kikitokea cha kiufundi aliyemuuzia anashindwa kumpa msaada unaostahiki kwa wakati.
Kwa maoni ushauri:+255789476655
Share:

Mar 1, 2015

BEI MPYA YA AZAM TV TSH 135,000/=


Hii ni kwa wateja wapya ambao wanataka kujiunga na azam tv,bei ya vifaa ni tsh 135,000/= hii namaanisha bila ufundi wala kifurushi!
Ili kufurahia huduma za azam tv inakupasa kufata utaratibu huu:-
VIFAA tsh 135,000/=
Inajumuisha Dish ikiwa na LNB,,Decoder ikiwa na smart card,cable mt20.
VIFURUSHI-
Azam pure tsh 12,000/= ch 25+
Azam plus tsh 20,000/= ch 50+
Azam play tsh 25,000/= zaidi ya ch 80
UFUNDI-
Ili ufungiwe inakupasa kulipa tsh 30,000/=
Hapa ndipo pana mvutano kidogo hapa,wateja wengi wanaona tsh 30,000/= ni nyingi na matokeo yake wengiwao wanaikwepa hii kwa kutafuta mafundi wao na kuwalipa chini ya 30,000 ama wanajikuta wanataka kufunga wenyewe matokeo yake wanaishia njiani kisha wanarudi tena kwetu!
Vipo vitu vya kujaribu lakini kitu kama ukijui tuachie tunaokijua,hii ina maanisha mgawanyiko wa kazi,madhara ya kuleta ufundi kufunga dish ikiwa hujui unaweza ukaua LNB ama ukaua Decoder.
1.Faida za kulipa tsh 30,000/= tukufungie sisi-
2.Ikiharibika ndani ya miezi mitatu repair bure.
Chochote kikitokea tunakusaidia kwa 100% kwa wakati.

Ukitaka kujua channels zilizopo kwenye kila kifurushi Bofya Hapa 

HUDUMA ZA AZAM TV | MSAADA KIUFUNDI | +255789476655
Share:

BEI MPYA YA DSTV TSH 99,000/= BILA UFUNDI


Baada ya ile offer ya tsh 99,000/=
Hii inajumuisha vifaa bila ufundi!
Kisha unachagua kifurushi ukipendacho kati ya hivi:-

KWA MAELEZO ZAIDI +255789476655

TUMEBOBEA KUFUNGA KWENYE:
HOTEL | APARTMENT | OFFICE
Share:

Feb 3, 2015

KIFURUSHI CHA AZAM PURE | AZAM PURE PACKAGE | TSH 18,000


Zijue channel zilizopo kwenye kifurushi cha azam pure:-
Kuna zaidi ya channel 60
  • Kwa wiki Tsh 7,000/=
  • Kwa mwezi Tsh 18,000/= 


Universal TV
BBS TV
Clouds TV Rwanda
Salam TV
Magic One
Channel 44
ASTV (Africa Swahili TV)
Boing
Africa News
Spark TV
TV - E
Salt TV
Baby First TV
Zodiak TV
Times TV
KASS TV
Jeem TV
MBC Plus Power
RAI Italia
Malawi National TV
KBC
Capital TV
Star TV
Azam Two
Azam One
KTN
K24
Bukedde TV 2
Rwanda TV
TV West
WBS
NBS TV
Urban TV
UBC
Citizen TV
EATV
ZBC 2
African Movie Channel
MBC 3
Liverpool TV
Manchester United TV
Real Madrid TV
Al Jazeera English
Fix & Foxi
Colors
MBC Bollywood
MTV India
ITV
Clouds TV
ZBC
Chanel 10
TBC1
Sinema Zetu
JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI Bofya Hapa


KWA HUDUMA | USHAURI | CHOCHOTE KUHUSU AZAM TV | +255 789 476 655
Share:

Jan 9, 2015

KIFURUSHI CHA AZAM PLAY | AZAM PLAY PACKAGE | TSH 28,000


Zijue channel zilizopo kwenye kifurushi cha azam play:-
Kuna zaidi ya channel105


  • Sony Max UK
  • Sony Channel UK
  • Universal TV
  • BBS TV
  • Clouds Plus
  • Royal TV Rwanda
  • BET
  • MSNBC
  • National Geographic Wild
  • Baby TV
  • Fox News
  • Clouds TV Rwanda
  • Salam TV
  • Magic One
  • Channel 44
  • ASTV (Africa Swahili TV)
  • Boing
  • Africa News
  • Spark TV
  • TV - E
  • Salt TV
  • AMC Series
  • Romanza Africa
  • Baby First TV
  • Zodiak TV
  • Times TV
  • Travelxp
  • KASS TV
  • Fox Sports 2
  • Bloomberg
  • ABS TV
  • wanasah
  • Jeem TV
  • MBC Plus Power
  • MBC 1
  • Rishtey Asia
  • RAI Italia
  • MBC Max
  • Malawi National TV
  • KBC
  • Capital TV
  • Star TV
  • NINA TV
  • Star Bharat
  • AsiaNet Middle East
  • Azam Two
  • Azam Sports HD
  • Azam One
  • KTN
  • K24
  • Bukedde TV 2
  • Rwanda TV
  • TV West
  • WBS
  • KTN News
  • NBS TV
  • Urban TV
  • UBC
  • Citizen TV
  • EATV
  • ZBC 2
  • BOX Africa
  • MTV Base
  • African Movie Channel
  • Fox Life
  • FOX Entertainment
  • MBC Action
  • MBC 2
  • ETV Africa
  • MBC 3
  • Landscape
  • MCS International
  • Liverpool TV
  • Manchester United TV
  • Real Madrid TV
  • National Geographic
  • Discovery Investigation
  • Fine Living
  • VIASAT Nature/ History
  • Al Jazeera English
  • Times Now
  • France 24 English 
  • NHK World
  • Fix & Foxi
  • MBC 4
  • MBC Drama 
  • Al Jazeera News Arabic
  • Isai Aruvi
  • Puthiya Thalamurai 
  • Mazhavil Manorama
  • ETV Telugu
  • Studio One
  • ABN Andhra Jyothi
  • Colors
  • Zoom
  • Sony SAB
  • UTV Movies
  • MBC Bollywood
  • Star Gold International
  • MTV India
  • Discovery Science
  • Star Plus
  • Kombat Sport 
  • Sony Max 
  • Nickelodeon 
  • BBC World News 
  • FOX Sports 
  • ITV 
  • Clouds TV 
  • ZBC 
  • Chanel 10
  • TBC1
  • Sinema Zetu
JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI Bofya Hapa

KWA HUDUMA | USHAURI | CHOCHOTE KUHUSU AZAM TV | +255789476655
Share:

Jan 4, 2015

KIFURUSHI CHA AZAM PLUS | AZAM PLUS PACKAGE | TSH 23,000


Zijue channel zilizopo kwenye kifurushi cha azam plus:-
Kuna zaidi ya channel 54


Universal TV
BBS TV
Royal TV Rwanda
BET
National Geographic Wild
Baby TV
Clouds TV Rwanda
Salam TV
Magic One
Channel 44
ASTV (Africa Swahili TV)
Boing
Africa News
Spark TV
TV - E
Salt TV
AMC Series
Romanza Africa
Baby First TV
Zodiak TV
Times TV
Travelxp
KASS TV
Fox Sports 2
Bloomberg
ABS TV
wanasah
Jeem TV
MBC Plus Power
MBC 1
RAI Italia
MBC Max
Malawi National TV
KBC
Capital TV
Star TV
NINA TV
Azam Two
Azam Sports HD
Azam One
KTN
K24
Bukedde TV 2
Rwanda TV
TV West
WBS
NBS TV
Urban TV
UBC
Citizen TV
EATV
ZBC 2
BOX Africa
MTV Base
African Movie Channel
MBC Action
MBC 2
ETV Africa
MBC 3
Landscape
MCS International
Liverpool TV
Manchester United TV
Real Madrid TV
National Geographic
Discovery Investigation
Fine Living
Al Jazeera English
Times Now
France 24 English
NHK World
Fix & Foxi
MBC 4
MBC Drama
Al Jazeera News Arabic
Colors
Zoom
Star Gold International
Zing
MTV India
Discovery Science
Star Plus
Kombat Sport
Sony Max
Nickelodeon
BBC World News
FOX Sports
ITV
Clouds TV
ZBC
JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI Bofya Hapa

KWA HUDUMA | USHAURI | CHOCHOTE KUHUSU AZAM TV | +255789476655
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita