Call / WhatsApp +255673378129

Nov 3, 2014

USISUMBUKE | PIGA +255658046655 | TUNAKUFATA ULIPO

Nilichogundua ni kwamba nina wadau wengi sana ambao haipiti siku bila kutembelea haka kablog chetu na kupata mawili matatu kuhusu ukanda huu..
Wengi mnataka kujua habari za ving'amuzi na huduma kwa ujumla..
Ufumbuzi wa ving'amuzi vyote upo kwenye haka kablog,maana yake ukishindwa kuelewa simu inahusika,ukipiga tu jua shida yako imeisha!


KWA KUWAJALI WATU WANGU...
Nimeanzisha huduma ambayo haikupi usumbufu na ni rahisi kwako!
Natekeleza maana ya huduma mtandaoni,kama tujuavyo huu ni wakati wa Digital hivyo lazima twende kidigital zaidi...
Swali unapenda/unataka king'amuzi gani kati ya hivi:-
DStv/Azam tv/Digitek/Continental/Zuku tv/Star times.
Piga simu sema unataka kipi,tunakupa ushauri na kisha utaletewa mpaka ulipo
Tukifika unalipia na kufungiwa papo hapo!
Ila hii ni kwa wakazi wa Dar es salaam tu!
Piga sasa +255784378129
TUMEBOBEA KUFUNGA KWENYE:-
HOTEL/APARTMENT/MAOFISINI NA MAJUMBANI.
BAADHI YA WALIONUFAIKA NA HUDUMA ZA MUSTAPHA MADISH:-
TRANSIT MOTEL/JB BELMONT/GERRAFE VIEW HOTEL/IKULU-OFFICE YA WAZIRI MKUU/PSPF/BAHARI BEACH LODGE/N.K.
Share:

Nov 1, 2014

HDMI CABLE


Imenipelekea kuandika post hii kutokana na simu niliyoipokea hivi karibuni kutoka Dodoma,lakini kabla ya simu hiyo kuwaelewesha wadau wangu kuhusu HDMI CABLE ni kawaida tu ila kwenye hii blog yetu leo wacha nitoe kile kidogo nilichonacho kwa wadau wangu!
Unapozungumzi HD
lazima ushirikishe cable inayoitwa HDMI CABLE,kwasababu ili uone picha katika mfumo wa HD ( Ubora wa picha wa hali ya juu ) ni lazima utumie HDMI CABLE,cable ambayo inatoa picha kutoka kwenye inaweza kuwa DVD/Receiver/King'amuzi ama chochote chenye uwezo wa kutoa HD na kupeleka kwenye tv ambayo nayo ikiwa ina uwezo wa kupokea HD.



Hii cable inachomekwa kwenye tundu lililoandikwa HDMI.
Ili kujua kama tv/DVD ama king'amuzi chako ni HD unapaswa kuangalia kwa umakini je kuna tundu lililoandikwa HDMI,kama lipo hilo jua kifaa chako hicho ni HD.
Je unavijua ving'amuzi vilivyo kwenye mfumo wa HD hapa Tanzania..??

  Una swali  piga +255789476655
Share:

Oct 29, 2014

DSTV PACKAGES | VIFURUSHI VYA DSTV


Lengo la kuwa na vifurushi tofauti ni kutoa fulsa kwa kila mdau kuweza kununua na kufanya malipo ya mwezi kutokana na uwezo wake.
Hivi ndivyo vifurushi vya DStv,idadi ya channel na bei kwa ujumla:-

1-DSTV BOMBA PACKAGE
Ina channel 65+ bora
Bei mpya ni Tsh 19,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

2-DSTV FAMILY PACKAGE
Ina channel 70+ bora
Bei mpya ni Tsh 39,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

3-DSTV COMPACT PACKAGE
Ina channel 85+ bora
Bei mpya ni Tsh 69,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

4-DSTV COMPACT PLUS PACKAGE
Ina channel 90+ bora
Bei mpya ni Tsh 109,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

5-DSTV PREMIUM PACKAGE
Ina channel 120+ bora
Bei mpya ni Tsh 169,000
Bofya Hapa kujua channel zilizopo kwenye kifurushi hiki!

CHANNEL MAALUM | BEI ZAKE

DStv French Touch
Ina channel 7 bora
Malipo ni Tsh 15,600
kujua channel zilizopo!


DStv Indian
Ina channel 4 bora
Malipo ni Tsh 71,500
kujua channel zilizopo!


DStv French Plus
Ina channel 15 bora
Malipo ni Tsh 88,000
kujua channel zilizopo!


DStv Great Wall China
Ina channel 10 bora
Malipo ni Tsh 16,500
kujua channel zilizopo



JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI Bofya Hapa


  Mafundi wa DStv | Chochote kuhusu DStv | +255 789 476 655
Share:

Oct 27, 2014

VING'AMUZI VISIVYO NA MALIPO

Nilichogundua ni kwamba watanzania wengi wanapenda ving'amuzi rahisi,rahisi kwenye kununua na katika ulipaji wa kila mwezi na pindi linapotokea swala la kutokuwa na malipo ya mwezi inakuwa ndio unafuu zaidi,kwasababu wanzania wengi wenzangu na mie...
DIGITEK

Hiki hakina malipo ya mwezi kwa mujibu wa wao wenyewe,ukinunua kwa tsh 110,000/= 
Inakuwa umemaliza labda gharama yako itazidi ikiwa unahitaji na Antenna.
CONTINENTAL

Hiki nacho sio kama hakina ila kipo hivi,ukinunua unaangalia na kuanza kulipia baada ya miezi 12 yaani mwaka mmoja,ingawaje mpaka sasa malipo hayajaanza kufanyika.
Ya Antenna tsh 75000/=
Ya Dish tsh 105000/=

TULIPOTOKEA....
TING pia haikuwa na malipo ya mwezi ilikuwa ukinunua umenunua,lakini sasa malipo mwanzo mwisho...

MAONI | USHAURI | HUDUMA | +255789476655
Share:

Oct 26, 2014

UNATAKA AZAM TV? | TUNAKUFATA | UNALIPIA | UNAFUNGIWA PAPO HAPO!

Hapa tunazungumzia malipo ya mwezi ni Tsh 12500/=
Unapata jumla ya channel 60.
Ukitaka kuzijua bofya hapa
Huduma hii inaweza kukufata popote ulipo ndani ya dar es salaam na malipo ukafanyia nyumbani ama mahali ulipo kabla ya kufungiwa king'amuzi chako.
Hii itakurahisishia wewe kutokusumbuka!
Hii yote ni katika kuboresha huduma zetu na kukuweka karibu yetu.
Kazi hii ni moja kati ya waliolipia nyumbani!




Unataka tukufate ulipo,ama tatizo lolote kuhusu azam tv?
+255789476655 Mustapha.
Share:

Oct 16, 2014

NAWALETEA CONTINENTAL YA DISH


Hatimae marejeo yamekuwa mazuri,ambapo sasa macho ya watanzania na wadau wa ving'amuzi kwa ujumla yameelekezwa kwa Digitek kuona yakuwa nao watatoa dish baada ya Continental kutoa Dish!
Hii inamaanisha leo ukihitaji king'amuzi cha Continental nitakachokuuliza cha kwanza..
unataka Continental ya Antenna ama ya Dish..
kisha mengine yanafata..

Share:

UWEZO BINAFSI

Ijapokuwa imepita miezi ipatayo 10 ila hili ni moja kati ya niyakumbukayo na ya kujivunia pia na sababu napokea simu mpaka wakati mwengine naona imepitiliza ila kwakuwa ndo kazi yangu sinabudi kumaliza shida za wadau wangu...
Nakumbuka ni maeneo ya sinza pale kumekucha kwa mzee moja hivii wa kihindi nilifunga Azam tv,kama ilivyoada kulipua kwangu ni mwiko nikafanya yangu na kanuni zangu kisha nikakabidhi kazi kwa mteja wangu!
Mteja cha kwanza kuniambia "nimependa kazi yako,umechukua muda mfupi na kazi safi" kwa kulithibitisha hilo wakamtoka wekundu wekundu pale nje ya malipo ya king'amuzi,hii alitoa kama pongezi yake kwang,nami kwakuwa nimetumwa helaa aaah nikashukuru pale wekundu wangu mfukoni kisha nikachapa mwendo!
ilipita kama wiki mbili alipata tatizo la king'amuzi maana kulikuwa na fundi akaleta ufundi nyumbani kwake hivyo alitaka msaada wa fundi,ilimlazimu afike ofisini na kwa bahati mbaya sikuwepo..fundi aliyepo akachukua nafasi yake akaenda na mteja kuangalia tatizo...
Tatizo alilimaliza na mteja akaendelea pata burudani kama kawaida...
Ikapita kama siku kadhaa tu mbele akaja tena ofisini kwa kununua king'amuzi kingine ila kwasasa alitaka zuku lakini safari hii pia hakunikuta,alidai aondoke na vifaa vyake ila kufungiwa anataka afungiwe na Mustapha,nilijaribu kupigiwa simu nami nilisema ukweli ni kama baada ya siku nne ndipo nitakuwa na muda,kitu ambacho kila mmoja pale ofisini alishangaa kuona mteja anakubali kuningoja..
Haikuchukua siku nne bali yule mteja alingoja kama wiki na siku tatu ndipo nikapata muda wa kwenda kumfungia Zuku yake..
Na hapo ndipo nikapata malalamiko ya fundi aliyeenda kufanya repair baada ya kupita mimi..
Hakukuwa na maelewano mazuri,lugha ya biashara haikutumika hapa ila nilichofanya ni kumtaka radhi kisha nikampa burudani kama ilivyo ada!
Matokeo yake hataki fundi yeyote zaidi Mustapha.
Hapa tunazungumzia uwezo binafsi si kama najua saana,ijapokuwa najua vilivyo vingi ukanda wangu na hata aliyefanya hivyo ni mwanafunzi wangu kati ya wanafunzi wangu wengi tu ila alishindwa ama wanashindwa kufata ile misingi husika..
Mafanikio huja kwa kupenda unachofanya!
Ukipenda unachofanya,utakifanya kwa uwezo wako wote na hii lazima ufanikiwe..
Upo facebook Bofya hapa like page yangu kupata mapya ya ving'amuzi vyote Tanzania
Share:

Oct 13, 2014

HII SIO SAWA KABISA

...nilipoona Dish hii ya DStv wala sikushangaa sana na badala yake ndipo nikaamua kupiga picha ili alau kile ambacho nilichokuwa sijawahi hata kukumbusha tukumbushane kwa pande zote mbili..
Mafundi wenzangu na wateja wetu pia wote wa ving'amuzi kwa ujumla hasa vile vya kutumia Satellite Dish.
Nianze na mafundi wenzangu wataalam wa madish... 
Inawezekana ukawa na kazi nyingi na inakulazimu ukifika site -kwa mteja,huwa huitaji kutumia muda mwingi bila kuangalia kama kazi unayoifanya itakuwa nzuri ama laa,matokeo yake unalipua tu ili mteja aone tu kwa wakati huo nawe uchukue chako na kesho akuite tena...
Kitaaluma hii si sawa hata kidogo..
Yaani kama umemuibia mteja wako..
Madhara ya hii licha ya kuonekana fundi mbabaishaji pia hautaweza kupata wateja wengine kupitia wateja uliowafanyia uhuni huu!!

Hakuna tangazo zuri kama kupitia kwa mteja uliyemuhudumia vema,labda nikwambie kitu ijapokuwa hii blog inanipa wateja lakini si kama ufikiriavyo wateja wangu wengi wanatokana na wale niliowahudumia vizuri na hii ndio siri ya mafanikio yangu katika taaluma hii..

Ila nilichogundua wateja wengi hasa wanawake si wasichana si wamama wao shida yao kubwa ni kuona tv inaonyesha,ila swala umefunga wapi hilo utajua fundi.
Wateja wetu wapendwa..

Share:

Oct 12, 2014

KING'AMUZI CHA BEI RAHISI KULIKO VYOTE TANZANIA

Swali?
Je unahitaji urahisi wa kulipa malipo ya mwezi ama kununua..!?
Limekuwa kama tatizo hivi kwa nchi yetu toka lilipokuja swala la udigital kuingia na kulazimika kila aliye Tanzania ili uangalie tv ni lazima king'amuzi kihusike!
Issue inakuwa hapa kuhusu king'amuzi!!
Kipi ni bei rahisi na kizuri kinachomfaa mtanzania na hata asiye mtanzania kwa ujumla!
Kipi ni king'amuzi bei rahisi swali la jibu hilo unaweza ukawa nalo wewe ila mimi wajibu wangu ni kukuletea bei za ving'amuzi vyote kisha wewe ndio mchaguzi kutokana na kipato chako na upenzi wa channel kwa king'amuzi husika..
DSTV TSH 99,000/= BEI YA OFFER BILA UFUNDI.
BEI YA SASA DSTV Bofya hapa
Hii sio bei ya siku zote,bei hii ni maalum kwa offer tu na pindi offer itakapoisha bei kamili nitawaletea!
 Baada ya hapo unachagua kifurushi ili ulipie uweze kuona Bofya hapa
Angalizo:Malipo ya mwezi yanapanda ama kupungua kutokana na dollar.

ZUKU TV TSH 75000/= BILA UFUNDI
Ambapo ukinunua unapata na mwezi mmoja bure!
 Baada ya mwezi wa offer kuisha unachagua kifurushi ili uendelee kuona Bofya hapa

AZAM TV TSH 135000/=
BEI YA SASA AZAM TV 

Kwasasa bei ya Azam tv ni tsh 135000 bila kufungiwa wala kifurushi.
Kufungiwa ni tsh 30,000/=
Vifurushi ni:- Bofya hapa

STARTIMES TSH DISH
STARTIMES TSH  ANTENNA
Hivi karibuni kimeanza cha dish,lakini hii haina maana kuwa cha antenna hakifanyi kazi kipo kama kawaida.
Vifurushi vya startimes ni:- Bofya hapa

DIGITEK TSH
Hii haina malipo ya mwezi ukinunua inakuwa ndio umenunua!
Lakini kutoka hapa kwangu na mtazamo wangu nitakuja kuzungumza kuhusu ving'amuzi visivyokuwa na malipo ya mwezi.

CONTINENTAL TSH 145000/=
Hiki nacho hakina malipo ya mwezi ukinunua umenunua.
Kujua channel zilizopo Bofya hapa

EASY TV TSH
Hiki kwa mwezi ni tsh 10,000/=

TING TSH 125000 DISH
 Tsh 20000/= ch100

TING TSH 60000 ANTENNA 
Vifurushi tsh 8000/= ch18+
16000 ch40+

Post hii itaboreshwa......

+ 255 789 47 66 55
Share:

Oct 11, 2014

STARTIMES YA DISH

King'amuzi ambacho kilipoanza kilipokelewa vizuri sana,watanzania wengi walinunua ila baadae kidogo kulitokea tatizo,tatizo ambalo liliwaweka wakati mgumu sana hasa katika kupata wateja wapya na wale wa zamani kutafuta namna ya kuondokana na tatizo hilo..
Tatizo la signal ambalo lilipelekea picha kukata kata ama kupotea kabisa ila ambalo lililokuwa linatokea hata kama mteja hajafunga vizuri Antena yake ama mafundi ambao wateja wanawatafuta ili wafungiwe Antanna zao kufunga ndivyo sivyo lakini atakachomalizia kusema tatizo ni la star times wenyewe..
Tatizo ambalo walikabiliana nalo na kulimaliza kabisa na kama inatokea kwa sasa zungumza na fundi wako ila kama ni fundi wewe mwenyewe maana watanzania tunaongoza kwa kuingilia kazi za watu..unapaswa Antanna yako kuielekeza Makongo juu,tatizo likiendelea hebu angalia cable yako ipo sawa? hakuna sehemu iliyochubuka kama sio kukatika? 
Likizidi hapo kuna namna unaweza nicheck nikakusaidia!
Binafsi huwa nasema Digital ni Dish ila inapotumika Antenna naona bado Analogue!
Pongezi kwenu Star times Tanzania kwa kuboresha huduma zenu kwa kuleta startimes ya dish,hili ni jambo zuri sana kwenu na kwa wateja wenu kwa ujumla!
Kwa tsh 105000/= umepata star times ya dish
Ambayo inakuwa na kifurushi cha mwezi mmoja ndani
Kwa maelezo zaidi na kuunganishwa +255789476655
Share:

Oct 10, 2014

KIFURUSHI CHA ZUKU PREMIUM | ZUKU PREMIUM PACKAGE | TSH 25,000


Zijue channel zilizopo kwenye kifurushi cha zuku premium:-
Kuna jumla ya channel 98 TV
channel 55 radio
Zuku Zone
Guest Channel
Citizen
KTN
NTV
K24
Kiss (KE)
EBRU
QTV
Kass tv
UBC
3Stone tv
NBS Uganda
Channel 10
TBC1
Clouds tv
WBS
ITV
MBC tv
Njata tv
Wholesome tv
Zuku Entertainment
EATV
Zuku Max
Zuku Max+2
Zuku Action
Zuku Action+2
Zuku Swahili Movies
AMC Series
Zuku Sports
Zuku Sports HD
Zuku Life
BBC World News
Al jazeera (English)
i24 English
TVC News
DW-tv
France 24 (English)
CCTV News
Zuku Kids
Smile of a Child
AMC
Eurosport News
FOX Sports
FOX Sports 2
FOX Entertainment
AMC USA
Viasat Nature
Viasat History
Viasat Crime
Viasat Explorer
Discovery Science
Nat Geo Gold
CCTV-9 Documentary
CCTV-4 (Chinese)
iConcerts
One Music
Kerrang!
Sky News
TLC
Nickelodeon
E! Entertainment
FX
Shortstv
MSNBC
Baby tv
Duck tv
JamJam
FineLiving
Fashion One
Fashion tv
Ginx tv
Magic
Kiss
Smash Hits
Box
MTV Base
i24 French
Vox Africa
Dubai tv
Abu Dhabi tv
Hope tv
Emanuel tv
EWTN
God tv
Family tv
Inspiration tv
Ahlulbayt tv
Peace tv
Safeer tv
Hope Intarnational
Al-erth Alnabawi

KWA HUDUMA | USHAURI | MAFUNDI | PIGA +255789476655
Share:

Oct 9, 2014

SIKU KAMA YA LEO MIAKA YA NYUMA...!


Tarehe 10 mwezi wa 10 miaka kadhaa nyuma..
Mustapha Hanya nikazaliwa kwa kichache nilichonacho Mustapha MaDish ukitiita hivyo inatosha..
Ah siwezi sema najua kila kitu ila nashukuru kwa umri wangu nimejua mengi sana..
Hakuna wa kumshukuru zaidi ya Allah muweza wa yote!
Kama leo nakumbuka siku yangu hii ya kuzaliwa sitakuwa sahihi kama sitawahusisha wazazi wangu wawili..
Daima ntaomba na sitaacha kuomba dua kwa Alla ampunguzie adhabu ya kaburi baba yangu mpendwa,huyu kwangu ndiye anakuwa shujaa,ndiye aliyenimezesha na kunifanya niishi popote na nisimame na yeyote na mwisho wa siku sirudi nyuma wala sinyoshi mikono juu..
Mungu ailaze roho ya marehemu baba mpendwa ISMAILY OMARY HANYA.
Shukurani za dhati pia zimuendee mama kipenzi FATUMA BAKARY wote kwa pa1 kufanya jitihada wawezavyo mpaka mimi leo nakuwa Mustapha MaDish maana yake wanastahili pongezi sijatoka nje ya mstari unaopaswa kijana kuwa ijapokuwa nna rafiki zangu kadhaa nilisoma nao na wengine kuishi nao mtaani kuwa nje ya mstari kwa kujiingiza kwenye matumizi ya madawa ama kuwa watu wa matukio.
SHUKURANI KWENU WADAU..
Pia napenda kuwashukuru wadau wangu woote popote mlipo,nashukuru mpo sambamba na mimi kila kukicha napokea simu nyingi sana na zote zikionyesha ya kuwa mnanikubali na mnatembela haka ka blog chetu,nami nitajitahidi kadri niwezavyo maoni yenu kuyafanyia kazi!


Share:

Oct 8, 2014

KIFURUSHI CHA ZUKU ASIA | ZUKU ASIA PACKAGE | TSH 24,000


Jumla ya channel zote zilizopo kwenye kifurushi maalum cha asia:-
Kuna jumla ya channel 27.
Zoom
Star Plus
Life OK
Colors
SAB
B4U Movies
B4U Music
Star Gold
Star jalsh
Zee Punjabi
Zee Cinema
Zee News
Zee Khana Khazana
Zing
MTV India
ET Now
Times Now
ARY News
ARY Digital
ARY Qtv
ARY Zauq
ARY Musik
UTV Movies
Aastha
Aastha Bhajan
Surya tv
Sun tv
More info: +255789476655 | mustaphamadish@gmail.com

Share:

Oct 7, 2014

STAR TV KWENYE AZAM TV


Swali limekuwa nawezaje kupata star tv kwenye king'amuzi cha azam tv!!??
Na hii imetokana na baadhi ya wengine kupata star tv kwenye king'amuzi cha azam tv..
Je star tv wameungana na azam tv!!??
Jibu ninaloweza kuwapa ni kwamba star tv haijaungana na azam tv,badala yake kutokana na uwezo wa fundi unaweza ukapata star tv kwenye king'amuzi cha azam tv..
N.B:Kutokana na uwezo wa fundi!
Soon nitawaletea picha ni vipi inakaa..

Share:

Oct 5, 2014

TUNAWATAKIA EID MUBARAKA..!!

Leo ni sikukuu..ina maana kubwa sana kwa waislam..lakini hii haina maana kuwa inawahusu waislam tu..
Kwakulijua hili tunachukua nafasi hii kuwatakia sikukuu njema watanzania wote na dunia kwa ujumla..
Yeyote atakayepata bahati ya kupitia blog yetu hii salamu hizi zinamuhusu!
Mapumziko mema..!
Share:

KIFURUSHI CHA ZUKU CLASSIC | ZUKU CLASSIC PACKAGE | TSH 18,000


Zijue channel zilizopo kwenye kifurushi cha zuku classic:-
Kuna jumla ya channel 69 tv
Channel 55 radio
Zuku Zone
Guest Channel
Citizen
KTN
NTV
K24
Kiss (KE)
EBRU
QTV
Kass tv
UBC
3Stone tv
NBS Uganda
Channel 10
TBC1
Clouds tv
WBS
ITV
MBC tv
Njata tv
Wholesome tv
Zuku Entertainment
EATV
Zuku Max
Zuku Action
Zuku Swahili Movies
AMC Series
Zuku Sports
Zuku Life
BBC World News
Al jazeera (English)
i24 English
TVC News
DW-tv
France 24 (English)
CCTV News
Zuku Kids
Smile of a Child
AMC
Eurosport News
FOX Sports
FOX Entertainment
AMC USA
Shortstv
MSNBC
Baby tv
Duck tv
JamJam
FineLiving
Fashion One
Ginx tv
Magic
Kiss
Smash Hits
Box
MTV Base
i24 French
Vox Africa
Dubai tv
Abu Dhabi tv
Hope tv
Emanuel tv
EWTN
God tv
Family tv
Inspiration tv
Ahlulbayt tv
Peace tv
Safeer tv
Hope Intarnational
Al-erth Alnabawi

KWA HUDUMA | USHAURI | MAFUNDI | PIGA +255789476655
Share:

Oct 3, 2014

BEIN SPORTS KWA TANZANIA


Awali kulikuwa na Abudhab baadae swala la kabumbu likahamia kwa Aljazeera,ambapo sasa ni nafasi ya Bein Sports mfumo wa ulipaji ukiwa ni ule ule na Decoder zitumikazo ni zile zile tofauti yake ni card tu!
Tanzania ni nchi mojawapo kati ya nchi kadhaa walizokuwa wanaangalia kandanda kupitia Decoder hizi!
Nimepokea simu nyingi sana kulizwa kuhusu swala la upatikanaji wa Bein Sports kwa Tanzania na ni kwa nini haipatikani kwa sasa na ni kwanini walihama toka nilesat kwenda badr na mengineyo yanayohusiana na Bein Sports...
Kwanini watanzania wanahaha kuitafuta Signal ya Bein Sports..??
..kutokana na maoni ya wengi ni kwamba..
Inaonyesha mpira live..
Haina malipo ya mwezi,ina ya mwaka na ni nafuu sana..
Hizo ndio sababu kuu mbili za kwanini Bein Sports inahitajika kwa udi na uvumba!
Watanzania lawama zao zote wanawatupia DStv kuhusu kupotea kwa signal ya Bein Sports kwa Tanzania..
AMBACHO LABDA HUKIJUI AMA 7BU KILA MTU ANAVUTIA KWAKE...
Kibiashara hakuna ambaye angependa kuona anapata hasara...
Na kama kuna kanuni za kibiashara lazima zifuatwe ili kila kitu kiende kwenye mstari..
Bein Sports huku hapaswi kuwepo..
mwenyewe wa huku ni DStv...
Lawama ni nyingi kwamba DStv gharama sana malipo ya mwezi..
Sababu kukawa na packages kwakuwa imeonekana watu wanauwezo tofauti wa kipato..
Sio lazima ulipie Premium 142000*
IJAPOKUWA BAADHI YA MIKOA INAPATIKANA HAPA TANZANIA..
Lakini sio kitu chenye uhakika tena kwasababu haitakiwi kabisa huku kwetu..
KAMA WEWE NI MPENZI WA MPIRA..
Piga +255789476655 uunganishwe na DStv kwa tsh 99000/=
Pia unaweza ukalipia package mpya inayoitwa Bomba kwa tsh 17000/=
Yenye channels za Sports kama Super Sport Select 1 na 2 na nyenginezo zaidi ya 65!

Share:

Oct 1, 2014

DSTV BOMBA PACKAGE | CHANNELS 65+ | TSH 19,000

Zijue Channel zilizo kwenye kifurushi cha DStv Bomba




FTA

KBC
CITIZEN
TBC
STAR TV
CHANNEL 10
ITV
Clouds Tv
KTN News
K24
Bukedde Tv
WBS
NBS Tv
e Tv Africa
Dish



MICHEZO


SuperSport Blitz
SuperSport Select1
SuperSport 2Select


SINEMA

Movie Zone
Africa Magic Epic Movies
Africa Magic Hausa
Africa Magic Yoruba
Africa Magic Lgbo
Africa Magic East
Maisha Magic BONGO



BURUDANI

Telemundo
E!
CBS Reality
CBS Action
CBS Drama
AMC
Vox Africa
TVC E


HABARI NA MAELEZO

BBC World
Al Jazeera
CNBC Africa
Bloomberg Tv
CNC World
SABC News


 MAKALA

National Geo Wild
DiscoveryFamily
ED
Spice Tv


MAISHA

Fashion TV


DINI

One Gospel
TBN
Daystar
Islamic channel
EWTN
Inspration TV
Kingdom Africa
Dove Tv
Emanuel Tv
FAITH


MUZIKI

Hip Tv
Sound city

WATOTO

Nickelodeon
Disney Junior
JimJam
Mindset Learn

KIMATAIFA

Zee World
NDTV 24*7
RAI International
TV5 Monde Afrique
 CCTV 4
CCTV Documentary
CCTV French
CCTV Entertainment
China Movie Channel
Shanghai Dragon Tv
Hunan Tv
Jiantsu Channel
Phoenix News Ent
RTPI
TV Mundal

RADIO

Over 40 Channels

JINSI YA KUHAMA KIFURUSHI Bofya Hapa
KUPATA MAFUNDI WA DSTV Bofya Hapa
VIFURUSHI VYA DSTV Bofya Hapa  
KUJUA BEI NA KUNUNUA DSTV Bofya Hapa

Kwa Maelezo zaidi  Piga +255789476655

Share:

DSTV TANZANIA YATOA OFFER TSH 99000/=

 




Kwa wateja wapya hii ni habari njema kwako,ambapo sasa unaweza kuunganishwa kwa tsh 99000 tu!
Hii inaanza leo tarehe 1/10/2014 mpaka kuisha kwa strock ya offer!
Kukurahisishia unaweza ukalipia gharama ya usafiri kutokana na umbali uliopo kisha huma ikakufata ulipo!
Ili upate huduma hii piga +255789476655
mustaphamadish@gmail.com

Share:

KIFURUSHI CHA ZUKU POA | ZUKU POA PACKAGE | TSH 13,000


Zijue channel zilizopo kwenye kifurushi cha zuku poa:-
Kuna jumla ya channel 53
Zuku Zone
Guest Channel
Citizen
KTN
NTV
K24
Kiss (KE)
EBRU
QTV
Kass tv
UBC
3Stone tv
NBS Uganda
Channel 10
TBC1
Clouds tv
WBS
ITV
MBC tv
Njata tv
Wholesome tv
Zuku Entertainment
EATV
Zuku Max
Zuku Action
Zuku Swahili Movies
AMC Series
Zuku Sports
Zuku Life
BBC World News
Al jazeera (English)
i24 English
TVC News
DW-tv
France 24 (English)
CCTV News
Zuku Kids
Smile of a Child
i24 French
Vox Africa
Dubai tv
Abu Dhabi tv
Hope tv
Emanuel tv
EWTN
God tv
Family tv
Inspiration tv
Ahlulbayt tv
Peace tv
Safeer tv
Hope Intarnational
Al-erth Alnabawi

KWA HUDUMA | USHAURI | MAFUNDI | PIGA +255789476655
Share:

Sep 15, 2014

DECODER YA CONTINENTAL


Niwe mkweli kwakuwa mimi napenda kwanza muonekano mzuri wa picha hivyo inapozungumziwa HD iwe HD kweli na kama hata isiwe HD lakini muonekano wa picha uwe mzuri, king'amuzi hichi ni moja kati ya ving'amuzi vyenye muonekano wa picha mzuri sana kwa zile channel zote zinazomilikiwa na Continental.
Huu ni mwaka 2018 bei kwa sasa ni Tsh ... kwa Decoder ya Antenna na Tsh ....  kwa Decoder ya Dish ikiwa set imekamilika, hapa nikiwa na maana inakuwa na Dish, Decoder, Cable, LNB
Ufundi ni Tsh 30,000/= kwa king'amuzi cha Dish
Share:

Sep 9, 2014

HII NDIO NYUMBA YA VING'AMUZI

Mwaka 2014 ndio huu unaelekea ukingoni ambapo mwakani mwaka 2015 inatupasa nchi nzima tuwe tumeshahamia Digital huku tukiwa tumeondokana kabisa na Analogue!
Ijapokuwa kuigia Digital kulikuwa na misemo mingi,wapo waliunga mkono ambapo idadi kubwa walilalama huku kila mtu akiwa na sababu yake ila wengi wao wakilalamikia uchumi!
Ingawaje malalamiko yalikuwa meengi ila udigital tumeingia na faida zake zinaanza kuonekana.
Kuna kampuni nyingi za ving'amuzi na kwa ujumla zote zinafanya vizuri haina ubishi kuwa kila kampuni ina wapenzi wake kutokana na huduma na channel husika|
Hii Blog ipo toka hapa Tanzania kuna kampuni tatu tu za ving'amuzi DSTV,GTV na EASY TV ijapokuwa mmiliki mwenyewe ambaye ni Mustapha E.Hanya a.k.a Mustapha MaDish yupo toka enzi ya DSTV tu.
Ukomavu wangu kwenye ukanda huu umenifanya niwe msaada mkubwa kwa watanzania na wasio watanzania kwa kuwahudumia kwa mkono wangu ama kwa ushauri tu.
Nipo sahihi sana nikisema kuwa hii ndio nyumba ya ving'amuzi kwakuwa leta kesi ya king'amuzi chochote ikishindikana kwenye mikono yangu ni hakika umefail jumla.
Binafsi najisikia faraja sana kuona mimi nakuwa msaada kwa wengine,kuona wengine wanaendesha maisha yao kupitia mimi,kuona watu wanatamani kuwa kama mimi..
Sina ambacho naweza sema zaidi ya Ahsante Allah kwa kila hatua nipigayo..
Nafikiria kufanya bora zaidi..zaidi ya hili ambalo naliendeleza kwa lengo lile lile kuendesha maisha huku kuwafunua upeo wengine hasa vijana wenzangu..
kama nilikuwa mwanga kuwa mtanzania wa kwanza kufungua Blogsite inayohusu hii taaluma na ikawa ya kwanza kwa Africa mashariki na kati ni hakika nimechonga barabara wacha wengine wapite kiulaini lakini watakuwa wananishukuru si tu kwa kunifuata hata wakiwa peke yao ndani ya nafsi zao watanishukuru kama si kunizungumzia..
Ili ufikie mafanikio lazima ukumbane na changamoto na ndicho kinachotokea..
Nipo kwa ajili ya kuwahudumia watanzania na wasio watanzania,waishio Tanzania na nje ya Tanzania pia..
Niulize leo chochote kuhusu king'amuzi chochote Tanzania..
DSTV
AZAM TV
ZUKU TV
DIGITEK
TING
STARTIMES
CONTINENTAL
EASY TV
Kwa swali lolote liwe la kiufundi ama huduma kwa ujumla!
Kutaka kuunganishwa pia!
Unaweza wasiliana nami:
Kama upo facebook utafanya busara kama utalike page ya mustaphamadish
+255789476655/714973797
mustaphamadish@gmail.com

 
Share:

Aug 31, 2014

LINAPOKUJA SWALA LA MVUA!


Pichani ni dish ya Azam tv huku mvua ikiwa inachapa vilivyo...
maana yake ni kwamba ndani hapo picha imepotea...
Kinachotokea kwa Azam tv hata DSTV kinatokea..
Linapokuja swala la mvua Dish ndogo huwa zinaelemewa...
Hivyo kinachotakiwa ni uvumilivu wa muda mchache na mara mvua inapokata picha zinarudi kama kawaida..
Na ikitokea mvua imeisha na picha haijarudi ujue kuna namna..
Hapo ndipo utajua fundi wako alifanya kazi kwa kiwango gani...!!??
Tatizo lolote la kiufundi..
Msaada kuhusu chochote kinachohusu maDish..
Piga +255789476655 Mustapha MaDish
Share:

ZUKU SMART PLUS PACKAGE | TSH 13,000



Zijue channel zilizopo kwenye kifurushi cha zuku Smart Plus:-
Kuna jumla ya channel 40 tv
Channel 18 radio


Channel zilizopo punde ntawajuza....!!

 Msaada zaidi +255789476655
Share:

Aug 1, 2014

BEI MPYA YA AZAM TV


Kutokana na sababu za kiuendeshaji imelazimika yatokee mabadiliko katika kuuza king'amuzi cha Azam tv.
Bei mpya ya Azam tv toka leo Tarehe 1/08/2014 ni Tsh 165000/=
Inajumuisha vifaa na Ufundi.
Malipo ya mwezi ni ile ile Tsh 12500/=
Ukilipa Tsh 177500/= unapata kufungiwa kila ktu na mwezi mmoja bure,hivyo utapata miezi miwili. 



Kwa maelezo zaidi Piga : Mobile +255789476655/714973797/659161111 Mustapha MaDish
Office: +255789 476655

Jivunie kuhudumiwa nasi!
Share:

Jul 9, 2014

BVN CHANNEL - OYSTERBAY DAR ES SALAAM


Nakumbuka mwaka 2008 niliwahi kupata mteja wa channel hii,tena ilikuwa baada ya mafundi kadhaa kuambulia patupu ikiwa wameshapoteza siku kama si masaa!!
Kipindi hicho niliweza kufanikiwa kuipata kwenye Dish ya ft8,nikimaanisha c band!
Oysterbay jijini dar,wenzangu na mie wanapaita pa kishua ila sina sababu ya kubisha!
Hakuna tofauti na mteja wangu yulee wa miaka ile,kwa maana wote wametokea taifa hilo na walihitaji channel ya nchini mwao!

Kwenye KU ft4 na Receiver ya kawaida tu,Mustapha MaDish nikaileta Netherland Tanzania kwa dk zisizozidi 45,baada ya hapo kuchapa mwendo kukahusika!


Kwa mahitaji ya Mafundi/Ving'amuzi vinatumia Dish aina zote hapa ndipo jibu lako!
Piga:-0789476655/0732575718/0859161111
Email:mustaphamadish@gmail.com
Mahali:Magomeni Mapipa/Morogoro rd 

Share:

Jul 8, 2014

NILIYONAYO KWAKO...

 Baba na Mwana
Nawasikitikia sana wale wanaopiga mechi za kikubwa kisha wanakimbiana,sababu zikiwa nyingi zisizo hesabika huku mwanamke akibaki mjamzito,ujauzito ambao mwisho wake unakuwa sio mzuri sana kwa maana wapo ambao wanaamua kutoa..hapa kwenye kutoa wapo waliofanikiwa kuchota dhambi kwa wingi na wapo waliopoteza maisha wakiwa katika kutimiza hilo!
Pia wapo waliamua kwa dhati kujifungua huku akijua yeye ndiye atakayekuwa baba na yeye ndiye atakayekuwa mama..
Kwa hili wapo waliofanikiwa wachache sana ila wengi wamefail kwa kukimbilia kutoa ama kuzaa na kushindwa kumuangalia mtoto kwakuwa yupo pekee yake..
Matokeo yake idadi ya watoto wa mitaani inaongezeka...
Napenda kuchukua nafasi hii kuwapa angalizo wanawake na waschana wote kwa ujumla Mwanaume,
mimi ikiwa mmojawapo niliyeandika post hii,tuna salio la uongo la kutosha lisilopungua kukudanganya wewe ili tu niingie panapofanya wewe ukaitwa mwanamke..
Bahati mbaya hata muambiwe vipi uelewa wenu wengi wenu ni tatizo,tena tatizo kuwa..
Ila alau hata kwa mwezi mara tatu ama mbili si vibaya tukazungumza alau kukumbushana tu kwa yale machache niliyonayo kwenu wapendwa!
Share:

Jul 7, 2014

C BAND FT12 - ADA ESTATE

Sababu iliyonileta hapa

  Baba yake na Fetty

Moja kati ya wanafunzi wangu wa kwanza kwanza kuwapa ujuzi huu ni huyu ambaye anaitwa Dullah kwa sasa amekula ajira pale Multichoice Tanzania ( DSTV ).
Kutoka ku moyo najisikia faraja sana kuona nasababisha mtu au watu fulani hasa vijana wenzangu kupiga hatua moja juu ikiwa kwenye kutengeneza maisha yake na familia yake kwa ujumla!
Nashukuru hakuna aliyenisahau ijapokuwa si wote kati ya wanafunzi wang ambao tunawasiliana mara kwa mara,najua ubize unaweza ukawa umechukua nafasi yake ama mambo ya hapa na pale.
Kwanini nimemzungumzia Dullah kwasababu hii kazi ya leo ilikuwa yake,mteja alimpigia mara kadhaa kwa siku tatu lakini muda wa Dullah ulikuwa mdogo hivyo kutokana na ushirika mzuri ndipo akaileta mezani kwangu ili tumalize tatizo la huyu mteja!
C band hii si ile iliyozoeleka na mafundi wengi ft6 ama ft8 hii ni ft12.
Nami nilienda nikijua ni ft6 kama ambavyo Dullah alidhani,hata spana ilinilazimu kurudi tena ofisini kuchukua kwa maana zile nilizobeba hazikuwa na uwezo wowote wa c kufungua hata kufunga tu.
Hapa angeenda ndugu yangu lazima angehitaji twende sote kwa maana Dish hizi zinahitaji uwezo wa ziada!
Kwanini naitwa MUSTAPHA MADISH ndipo nikadumisha umwamba wangu kisha tukachapa mwendo!
Share:

#FundiKalipua

Najivunia Tanzania yangu




Powered by Blogger.

Fanya kuni Follow Instagram

YOTE YANAYOHUSU VING'AMUZI TUKUTANE INSTAGRAM

Habari mdau wa Digital tv kiujumla! Najua alau kipo nilichowasaidia kupitia hii blog na wakati mwengine pengine siwasaidii kwa wakati na...

Nitumie Email

Name

Email *

Message *

Idadi ya Watembeleaji

Slider

FAHAMU KWA KINA: Kifaa kinachopokea matangazo ya Digital kinaitwa KISIMBUZI sio KING'AMUZI..

Culture

Wisata

Favourite

Event

Gallery

News Scroll

USHAURI | MSAADA KIUFUNDI | KUNUNUA PIGA/WHATSAPP +255673378129

Post zilizokupita